Kwa mujibu wa uwezo aliopewa chini ya Vifungu 42 (1) na (2), 43 (1) na (2) na 47 vya Katiba ya Zanzibar ya Mwaka 1984, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein ameunda Wizara 16 na kuwateua Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi, Mawaziri na Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:
1. Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Ikulu.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi-
Mhe. Dr. Mwinyihaji Makame
2. Ofisi ya Rais (Fedha, Uchumi na Mipango ya Maendeleo)
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Fedha, Uchumi, na Mipango ya Maendeleo)
Mhe. Omar Yussuf Mzee
3. Ofisi ya Rais, (Utumishi wa Umma na Utawala Bora)-
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Utumishi wa Umma na Utawala Bora)
Mhe. Haji Omar Kheri
4. Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Kwanza wa Rais
Mhe. Fatma Abdulhabib Fereji.
5. Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais-
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais
Mhe. Mohammed Aboud Mohammed
6. Wizara ya Katiba na Sheria
Mhe. Aboubakar Khamis Bakary.
7. Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano
Mhe. Hamad Masoud Hamad
8. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali
Mhe. Ramadhan Abdulla Shaaban
9. Wizara ya Afya
Mhe. Juma Duni Haji
10. Wizara ya Ustawi wa Jamii na Maendeleo ya Wanawake na Watoto
Mhe. Zainab Omar Mohammed
11. Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo
Mhe. Abdilahi Jihad Hassan
12. Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati-
Mhe. Ali Juma Shamhuna
13. Wizara ya Kilimo na Maliasili
Mhe. Mansoor Yussuf Himid
14. Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko
Mhe. Nassor Ahmed Mazrui
15. Wizara ya Mifugo na Uvuvi
Mhe. Said Ali Mbarouk
16. Wizara ya Kazi, Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi na Ushirika
Mhe. Haroun Ali Suleiman
17. Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri Asiekuwa na Wizara Maalum
Mhe. Suleiman Othman Nyanga
18. Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri Asiekuwa na Wizara Maalum
Mhe. Haji Faki Shaali
19. Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi na Waziri Asiekuwa na Wizara Maalum
Mhe. Machano Othman Said
Aidha Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohammed Shein ameteua Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:
1. Naibu Waziri, Wizara ya Miundombinu na Mawasiliano
Mhe. Issa Haji Ussi
2. Naibu Waziri, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali
Mhe. Zahra Ali Hamad
3. Naibu Waziri, Wizara ya Afya
Mhe. Dr. Sira Ubwa Mamboya
4. Naibu Waziri, Wizra ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo,
Mhe. Bihindi Hamad Khamis
5. Naibu Waziri, Wizara ya Ardhi, Makaazi, Maji na Nishati
Mhe. Haji Mwadini Makame
6. Naibu Waziri, Wizara ya Biashara, Viwanda na Masoko,
Mhe. Thuwaiba Edington Kissasi
Waheshimiwa wote waliotajwa wanatarajiwa kuapishwa hapo kesho jioni katika viwanja vya Ikulu mjini Zanzibar.
Naomba kuwasilisha
Chanzo:Mzalendo.net