Mtazamohalisi

Saturday, October 16, 2010

TBC Habari za Tanzania.

ITV na Habari za Tanzania.

Yasijirudie Ya Uchaguzi Mkuu 2010 kwenye Uchaguzi Mkuu 2015

Rais Jakaya M.Kikwete

viongozi wa vyama vya siasa nchi

Kukataa mdahalo
Napinga kitendo cha CCM kukataa midahalo kwa madai wananchi wanajua mazuri waliyofanya na watakayofanya.
Hii haikubaliki kwani bado umewanyima wananchi fursa nzuri ya "kuchambua mchele na chuya".

Vyama kuwasahau wapiga kura
Hii mara nyingi inatokea baada ya uchaguzi, vyama vinaacha kukita mizizi katika maeneo walikoshinda au kushindwa. Kufanya hivyo hakuleti picha nzuri kwa wananchi, kwani wao huonekana muhimu tu wakati wa kuomba kura.

Vyama kutokuwa na mipango ya muda mrefu
Mbali na CCM inajulikana na kila mtu kuwa Rais Jakaya Kikwete anamaliza muda wake,hivyo kuna harakati za kumtafuta mrithi wake.
Na kwa utaratibu wa CCM chama hakina mtu ila kina wenyewe nakwa mtindo huo ,mfumo wa uongozi upo wazi hivyo chama hakimtegemei mtu ila kinajitegemea kutokana na mfumo wake.
Kuhusu vyama vya siasa hilo nalo muhimu kulitambua, chama si mali ya mtu bali chama kinabakia kuwa ni wanachama hivyo basi wajenge misingi mizuri yakuachiana madaraka.Kuhusu mipango mengine vyama lazima viweke misingi imara ya kuingia katika serikali za mitaa kabla uchaguzi mkuu hii itasaidia kujua jinsi gani wanakubalika ili wafanye marekebisho yakisera yatakayoweza kuwashawishi wapiga kura.

Ahadi kwa watu wenye kuhitaji msaada maalum
Tumeona vyama katika nyingi ya ahadi zao wamesahau kuwa watu wenye kuhitaji msaada maalum kama viziwi,vipofu,wazee na maalbino kuwa ni muhimu katika jamii.Kwa mfano hakuna chama kilichosema nitasaidia kufungua shule au kuboresha zilizopo kwa watu wajamii hii,tumeona pia kuna uwindwaji kama wanyama kwa wazee na maalbino.Je! hili la usalama wao halizungumziki? maana haifai baadae kutaka umaarufu kupitia jamii hii.

Katika serikali za awamu zote nne zimejikita zaidi katika masuala ya miundo mbinu pamoja na maji,tunaomba mwaka 2015 iwe ahadi hizi kuwa ni basi maana nijukumu la Serikali kulitekeleza hilo nasio mambo yakutaka kudai kura.Muhimu kwa kila mgombea kuja na nini? atafanya kuondoa tatizo la ajira na mipango ya kupunguza umaskini,ujinga na maradhi.
Itaendelea sehemu ya pili..................

Mtazamo halisi(Hekima,Maarifa na Busara)

Wengiwetu tumelala Wengiwetu tumeamka,basi zinduka kwa "Mtazamohalisi" .
Mtazamohalisi ni blog yenye lengo la kuelimisha jamii,kwakufungua Maarifa mapya
yenye kujenga.
Kwa kuwa mtandao wa habari ni mpana, ushirikiano ni muhim ili kufikia lengo
lakufikisha ujumbe kwa jamii.
Kuna ambayo tunajua basi pokea,na kwako kuna ambayo unajua tutapokea.
" Jamii moja ,hujengwa kwa umoja".

Kwajina lake manani,muumba yetu dunia
hakika yake nishani,viumbe kujivunia
akili zakila fani,hakika kajaalia
twakuomba rahmani,ukweli kusimamia.
"Ni mtazamo halisi,wastara haumbuki".

Ni mtazamo halisi,wastara haumbuki
tumia yako nafasi,fursa hii shiriki
kutoa hakufilisi,hasa kutoa kwahaki
hidaya ya almasi,pokea kwa halaiki.
"Ni mtazamo halisi,wastara haumbuki".

Hekima kubwa thamani,maarifa na busara
mazuri yalo maoni,hujenga ikawa dira
yawe yatokea pwani,yawe yatokea bara
kwa kuwa jambo yakini,hakuna zuri hasara
"Ni mtazamo halisi,wastara haumbuki".

Karibu hii baraza,tujue yanayojiri
elimu yako mwangaza,si vema ikawa siri
shauri kutengeneza,tupate kujiajiri
wema wako kuwekeza,haitokuwa sifuri.
"Ni mtazamo halisi,wastara haumbuki".

Kaditama ndiyo mwisho,mtazamo kufikisha
ijenge leo kwa kesho,makosa kusahihisha
mbaya roho ya korosho,mazuri kuyafifisha
mtazamo suluhisho,sasa taa tumewasha.
"Ni mtazamo halisi,wastara haumbuki".
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...