Mbunge wa Jimbo La Katavi-Mh.Mizengo Pinda Waziri Mkuu Mteule |
Kwa mujibu wa sheria ya nchi, inasubiriwa bunge kuthibitisha uteuzi wake hii leo .
Wakati huo huo, leo ndio siku ya kumchagua naibu spika wa bunge la jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Wagombea wa nafasi ya Unaibu spika ni Mh.Job Ndugai kwa tiketi ya CCM na Mh.Mustapha Akonay toka CHADEMA.
Ikiwa bunge litampitisha Mh.Mizengo Pinda ,Waziri Mkuu ataapishwa kesho ikulu ndogo ya Chamwino.
Na mchakato wa kupata baraza la mawaziri utafuata baada ya mashauriano baina ya Rais, Makamu wa Rais na Waziri Mkuu.
Baraza la Mawaziri linatarajiwa kutangazwa siku ya Ijumaa.
No comments:
Post a Comment