Mtazamohalisi

Friday, December 31, 2010

Kali Za Funga Mwaka

Huko Afrika kusini,kumekuwa na heka heka za mwisho kwa raia wa Zimbabwe kujiandikisha kisheria.
Raia Wazimbabwe atakaye kuwa hajajiandikisha atajikuta anarudishwa nchini Zimbabwe.

Mwezi Aprili ,2009 serikali ya Afrika kusini ilitoa ruhusa kwa Wazimbabwe kuingia nchi hiyo bila kibali kufuatia hali mbaya ya kisiasa na kiuchumi.Kusamehemewa Viza kwa Wazimbabwe,kulikuja kutokana na mazungumzo baina ya nmawaziri wa mambo ya ndani wa Zimbabwe na mwenzake wa Afrika kusini.



Huko Uhispania,wanawake wajawazito wamejikuta wakiharakisha kujifungua ili kuweza kupata posho toka serikalini.
Mabadiliko ya sheria ya mafao ya uzazi yataanza rasmi tarehe mosi 2011,ambapo serikali ya Uhispania imetangaza kusimamisha rasmi utoaji wa posho ya US$ 3000.
Kudidimia uchumi wa Uhispania kumepelekea serikali kusimamisha
posho ya ulezi .

Lengo la utoaji wa posho hiyo,ambayo ilianza rasmi mwaka 2007 lilikuwa ni kuwahamasisha raia wa Uhispania kuongeza vizazi ili kukabiliana tatizo la uhaba wa watu .

"Ili Uhispania kuendelea, inahitaji kuwa familia zenye watoto wengi.Na familia itabidi ihitaji misaada zaidi ili kuweza kuwa na watoto wengi na vyanzo vingi ili kumudu ulezi", Zapatero aliliambia bunge mwaka huo.
Zaidi soma .Aljazeera

Estonia tarehe 1/1/2011 itakuwa mwanachama wa 17 wa muungano wa sarafu wa ulaya,ni nchi ya kwanza toka Muungano wa nchi za soviet kujiunga na umoja wa Ulaya na Nato mwaka 2004.



Brazil -Kwa heri Lula ,karibu Dilma Roussef
Anaanza kazi rasmi tarehe 1/1/2011.
Mwanamke wa kwanza kuwa rais,nchini Brazil

Australia-Sura Tatu Zakaribisha Mwaka Mpya

Kaskazini Ya Australia Yakumbwa na Mafuriko
Ukubwa wa eneo la Kaskazini ni sawa na nchi
ya Ujerumani na Ufaransa kwa pamoja au kwa
nchi kama Marekani ni eneo zima la Texas.
Watu takribani 200000 waokolewa


Kusini Mashariki ya Australia yakubwa na ongezeko kubwa la joto

Hatimaye Mji wa Sydney wafurahia Ujio wa mwaka mpya

Thursday, December 30, 2010

Waziri Akataa Kuuziwa Mkaa Korogwe


Waziri wa Maliasili na Utalii,Ezekiel Maige

Wauza mkaa katika eneo la kijiji cha Chekeleni, wilayani Korogwe mkoani Tanga, walivamia gari la Waziri wa Maliasili na Utalii, Ezekiel Maige, baada ya kusimama ghafla katika eneo hilo na kutaka wamuuzie mkaa wao, wakifikiri ni mteja wa kawaida.


Hata hivyo, ndoto za wafanyabiashara hao ziliyeyuka ghafla, baada ya kubaini kwamba, Waziri Maige si mteja kama walivyofikiria, bali alisimama hapo kutaka kuona kama wanauza mkaa huo kihalali.

Baada ya kugundua kwamba wanayemshawishi anunue mkaa wao ndiye Waziri wa Maliasili na Utalii, wafanyabiashara hao waliokuwa wamepanga maguni ya mkaa pembezoni mwa barabara, waliamua kutimua mbio na kuacha mkaa wao, huku waliobaki katika eneo hilo, wakikana kujihusisha na biashara hiyo.

Waandishi wa habari waliokuwa kwenye msafara wa Waziri Maige, walipata fursa ya kuzungumza na baadhi ya wananchi ambapo walidai kuwa wamekuwa wakiuza mkaa kwa Shilingi 7,500 kwa gunia moja.

Wananchi hao walisema kuwa wamekuwa wakiuza mkaa huo kila siku ili waweze kujipatia ridhiki na kwamba baadhi ya maafisa misitu wamekuwa wakiwaomba chochote (rushwa) ili wawaruhusu kuendesha biashara hiyo ikiwa ni pamoja na kutoa ushuru wa Sh. 1,000.

“Hata hivyo, tunashindwa kuelewa maana mara waje watu wengine na kujiita watu wa TRA, tunawapa ushuru na tunaposhindwa kutoa wanachukua mkaa na kuondoka nao. Mara nyingine wanakuja watu wa halmashauri tunatoa ushuru gunia Sh. 1,000,” alisema mwananchi mmoja na kuoinyesha risiti ya magunia 50.

Mwenyekiti wa kijiji hicho, Athuman Said, alirusha lawama kwa baadhi ya watumishi wa serikali kwamba wao ndio chanzo cha ushuru wa mazao ya misitu kupotea kwa sababu wamekuwa hawatekelezi majukumu yao ipasavyo.

Hata hivyo, mwenyekiti huyo ameishauri serikali kuwabana wachoma mkaa ili waweze kutoa ushuru badala ya kuwabana wafanyabiashara wadogo wadogo tu.

Kwa upande wake, Waziri Maige, aliagiza kwamba maafisa misitu wahakikishe kila anayefanya biashara ya mkaa anatoa ushuru wa Shilingi. 2,000 kwa gunia moja na kwamba wasimamie ipasavyo sheria namba 14 ya mwaka 2004, inayohusu mazao ya misitu.

Waziri Maige aliwataka wananchi kuhakikisha pindi wanaponunua mkaa wapewe risti, ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza na kwamba wakikutwa wakiwa hawana risti watakamatwa kwa mjibu wa sheria.

Waziri Maige aliwaambia wananchi hao kuwa kudai risiti kutasaidia kukusanya mapato ya serikali kwa kiwango kinachotakiwa kwani wakwepaji wa ushuru watakuwa wamedhibitiwa.

“Wananchi wahakikishe pindi wanapouziwa mkaa wapewe risti na muuzaji huyo, maana ukikamtwa huna risiti ni kosa. Na hali hiyo itasaidi kuwabana wakwepaji wa ushuru na hivyo kukusanya mapato ya serikali vizuri,” alisema Waziri Maige, ambaye tangu alipoteuliwa kushika wadhifa huo mwezi uliopita, amekuwa akichukua hatua za kubana wizi wa rasilimali za nchi.
Chanzo: Nipashe

Rais Wa Zamani Wa Israel Apatikana Na Hatia Ya Ubakaji


Rais wa zamani wa Israel,Moshe Katsav

Rais wa zamani wa Israel Moshe Katsav amepatikana leo na hatia ya makosa mawili ya ubakaji, ikiwa ni kilele cha kashfa iliyojitokeza miaka minne iliyopita ambayo ililishangaza taifa hilo la Kiyahudi. Rais huyo wa zamani anakabiliwa sasa na hukumu ya kwenda jela miaka minane.


Wakati mahakama hiyo mjini Tel Aviv ikitoa hukumu hiyo, ambapo pia imemhukumu Katsav kwa madai ya bughdha za kingono, vitendo vinavyovuka mipaka na kuzuwia sheria kuchukua mkondo wake, rais huyo wa zamani mwenye umri wa miaka 65 ambaye alionekana dhahiri kufadhaika, alikuwa akinong'ona tu, "hapana , hapana".

Hukumu hiyo inakuja baada ya kuendeshwa kesi hiyo ambayo imechukua mwaka mmoja na nusu na kujumuisha madai ambayo ni ya kuhuzunisha, yakimuonesha Katsav kuwa ni mbakaji ambaye mara kwa mara huwasumbua wafanyakazi wanawake katika ofisi yake.

Kiongozi huyo wa zamani wa nchi anashutumiwa kwa kumbaka mara mbili mwanamke mmoja ambaye ametambuliwa kwa jina la "Aleph" wakati akiwa waziri wa utalii, na kuwafanyia usumbufu kingono na kuwabughudhi wanawake wengine wawili wakati akiwa rais. Katsav amesema kuwa hana hatia wakati wote wa uchunguzi wa kesi hiyo ya ubakaji na usumbufu wa kingono.

Awali alikubali makubaliano ya kutoa maelezo yake mahakamani ambayo yangemfanya kukubali madai madogo madogo na kulipa faini ili waendesha mashtaka watupilie mbali madai ya ubakaji, lakini baadaye alibadili msimamo wake, na kufanya makubaliano hayo kuwa batili na kusema anataka kusafisha jina lake mahakamani.

Alilazimika kujiuzulu kama rais , akakabidhi ofisi kwa hasimu wake Shimon Peres. Katsav amewashutumu wahanga wake kwamba wanajaribu kumwendea kinyume na kudai kuwa alikuwa mhanga wa juhudi za kumchafulia jina zinazofanywa na kundi la waendesha mashtaka na vyombo vya habari bila ya yeye kuweza kujitetea. Mwanawe wa kiume Boaz Katsav, baada ya kutolewa hukumu hiyo amesema kuwa baba yake hana hatia.

Tunataka kukata rifaa. Na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu, kila mmoja atatambua kuwa baba yangu , rais wa nane wa taifa la Israel hana hatia.

Waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amesema kuwa ni siku ya masikitiko kwa taifa la Israel na raia wake, lakini ameisifu kesi hiyo kuwa ni ishara ya nguvu za mfumo wa sheria wa nchi hiyo.
Chanzo: Dw

Wednesday, December 29, 2010

Bei Mpya Za umeme Hizi Hapa

SHIRIKA la Umeme nchini (TANESCO) limeainisha gharama mpya kwa watumiaji wa umeme zitakazoanza kutozwa kuanzia mwezi Januari mwakani.

Taarifa iliyotolewa kwenye vyombo vya habari na Ofisi ya Uhusiano wa Tanessco jijini Dar es Salaam jana ilianisha kuwa gharama hizo mpya zimegawanyika katika makundi matatu kulingana na mahitaji ya matumizi ya umeme.

Makundi hayo ni pamoja na watumiaji wa nishati hiyo kwa matumizi ya majumbani ambapo gharama ya chini kutoka 0-50 kWh/mo utauzwa kwa gharama ya sh 60 badala ya sh 49 ya sasa, tofauti yake ikiwa sh 11.

Kwa upande wa matumizi ya umeme ya kawaida bei ya matumizi kwa gharama za nishati kwa uniti imepanda kutoka sh 129 hadi kufikia Sh 157 ikiwa imeongezeka kwa sh 28.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kadhalika kwa upande wa mahitaji ya juu ya msongo mdogo, gharama za nishati kwa uniti imepanda kutoka sh 85 hadi sh 94 ikiwa imepanda kwa sh 9 zaidi.

Kadhalika mahitaji ya juu ya msongo mkubwa, gharama za nishati kwa uniti ambao ulikuwa ukiuzwa sh 79 sasa utauzwa sh 84 tofauti ikiwa ni sh tano.

Kwa upande wa Shirika la Umeme Zanzibar gharama za nishati kwa uniti kwa gharama mpya ya umeme itakuwa ni sh 83 badala ya sh 75 gharama hizo zikiwa zimepanda kwa sh 8.

Watumiaji ambao wameonekana kuumizwa katika gharama hizi mpya ni wale wa matumizi madogo madogo ya nyumbani na wenye matumizi ya kawaida ambao wamepandishiwa kwa zaidi ya Sh 10.

Kwa muhibu wa taarifa za TANESCO, hatua hiyo ya ongezeko la gharama imefikiwa baada ya gharama hizo kuidhinishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA).

Dk. Slaa Aacha Kilio CCM

USHINDI mwembamba wa Chama cha Mapinduzi (CCM) uliosababisha ruzuku yake kuporomoka, umekiweka chama hicho mahali pabaya baada ya watendaji wake kushindwa kulipana mishahara.

Chama hicho tawala kimefikia hatua ya kushindwa kuwalipa watendaji wake hasa wale wa nchini na kupunguza matumizi baada ya ruzuku yake kushuka kutoka zaidi ya sh bilioni moja hadi sh milioni 800,000 baada ya mgombea urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willbrod Slaa kupunguza kura za Rais Jakaya Kikwete kwa kiwango kikubwa.

Habari kutoka ndani ya makao makuu ya CCM, zinasema chama hicho kimepunguza matumizi yake kwa kiasi kikubwa na mara nyingi Katibu Mkuu wa chama hicho, Yusuf Makamba, amekuwa akiwaambia watendaji hao kwamba hali hiyo inatokana na kupungua kwa ruzuku.

'Sasa hivi hakuna cha vocha wala pesa za posho kama zamani. Tunaambiwa tujitolee, watendaji wa chini waliokuwa wakipelekewa pesa kila mwezi, kama hawawezi kujiendesha, wasitegemee pesa toka makao makuu,' alisema mmoja wa maafisa wa chama hicho, ofisi ndogo ya Lumumba, Dar es Salaam.

Mbali ya kushindwa kulipana mishahara, habari zaidi zinasema watu walioathirika na kimbunga cha Dk. Slaa ni taasisi za CCM ambazo ndizo zilikuwa kinara wa kumpinga Dk. Slaa wakati wa kampeni.

Taasisi hizo zinazomegewa ruzuku kila mwezi mgao wao umepungua na kuna uwezekano wa baadhi yao kufutiwa kabisa.

Baadhi ya taasisi zinazopata ruzuku toka makao makuu ya CCM ni pamoja na kundi la muziki wa dansi, kwaya na maigizo la Tanzania One Theatre (TOT), Radio Uhuru, Kampuni ya Magazeti ya Uhuru na Mzalendo, jumuiya za chama ambazo ni Umoja wa Vijana (UVCCM), Jumuiya ya Wanawake (UWT) na Jumuiya ya Wazee CCM (TAPA).

'Kwanza TOT, magazeti ya Uhuru na Mzalendo na Radio Uhuru, yanaweza kufutiwa kabisa ruzuku maana hakuna maana ya kuwapa ruzuku kama wanapaswa kujiendesha kibiashara na wanapata faida. Mpango huo umeanza kujadiliwa sana pale makao makuu,' alisema mmoja wa makada wa CCM ambaye ni mjumbe wa Halmashauri Kuu.

CCM inapata kiwango sh milioni 800 kutokana na kupata asilimia 60.40 ya kura za urais katika uchaguzi huo, ambazo ni sawa na sh milioni 354 na asilimia 77 ya wabunge (sawa na sh milioni 460) kwa mwezi.

CHADEMA inapata sh milioni 203.6, kwa kupata asilimia 24 ya kura za urais (sawa na sh milioni 146) na asilimia 9.62 ya wabunge (sawa na sh milioni 56) wakati CUF, sasa inapata sh milioni 117.4, kutokana na kupata asilimia 9.80 ya kura za urais (sawa na sh milioni 57.9) na asilimia 10 ya wabunge (sawa na sh milioni 56).

NCCR-Mageuzi inapata ruzuku ya sh milioni 10 kutokana na kupata asilimia 1.08 ya wabunge wakati UDP na TLP vinapata ruzuku ya sh milioni 2.4 kwa kupata asilimia 0.42 ya kura za ubunge kila kimoja.

Kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi, ruzuku hiyo hutolewa kwa chama kilichofikisha kuanzia asilimia tano ya kura za urais na kwa uwiano wa wabunge na madiwani, ambao chama kilivuna katika uchaguzi huo.

Ruzuku hiyo ilianza kutolewa Novemba, baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika nchini Oktoba 31, mwaka huu na ule uliofanyika baadaye katika baadhi ya majimbo kukamilisha uchaguzi huo.

Katika uchaguzi mkuu uliopita, Rais Kikwete alipata ushindi mwembamba wa kura milioni tano, sawa na asilimia 61.17, akifuatiwa na Dk. Slaa aliyepata kura 2,271,941, sawa na asilimia 26.34, wakati mgombea wa CUF Profesa Ibrahim Lipumba aliambulia kura 695,667, sawa na asilimia 8.

Chanzo: Tanzania Daima

Monday, December 27, 2010

Sitta Asubiria Taarifa Rasmi Kuhusu Hoja Ya Mgeja

Vinara wakukemea ufisadi

Waziri wa ushirikiano wa Afrika Mashariki,Spika wa
mstaafu Samuel Sitta akiwa na Mbunge wa SameMashariki
Bi Anna Kilango.

WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amesema amasubiri kwa hamu hoja binafsi iliyoahidiwa kuwasilishwa Halmashauri Kuu ya CCM na Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja,.

Alhamisi iliyopita, Mgeja alimtuhumu Sitta kuwa anaendeleza mgawanyiko ndani ya CCM na kumtaka afute kauli yake kuwa aliondolewa uspika kwa mizengwe, la sivyo atawasilisha hoja binafsi Nec kumtaka athibitishe. 
“Sitta anapaswa kufuta kauli yake kuwa, aliondolewa kwa hila…kikao kilichofanya uamuzi kuhusu nafasi ya uspika ni Kamati Kuu ya CCM. Kwa hiyo anamaanisha wajumbe wa kikao hicho wana hila naye.

Kusema hivyo kutasababisha baadhi ya wanachama kukosa imani na kikao hicho,” alisema Mgeja. 
Akizungumza na gazeti hili juzi, Sitta alisema ingawa hajapata taarifa rasmi kuhusu hoja za Mgeja, anaisubiri kwa hamu.

“Siwezi kuzungumzia kwa kina taarifa ya Mgeja kwa kuwa sijaipata vizuri, lakini ninaisubiri kwa hamu hoja yake hiyo,’’ alisema Sitta ambaye alikuwa Spika wa Bunge la Tisa.

Wakati Sitta akisita kujibu hoja ya Mgeja, Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango, amemshangaa Mwenyekiti huyo wa CCM Mkoa wa Shinyanga, akisema alichosema hakiwezekani.
Pia, Kilango alipuuza msimamo wa Mgeja akisema hauna mashiko: "Hoja binafsi zinapelekwa bungeni tu, sio kwenye vikao vya chama. Vikaoni zinaletwa ajenda, sasa huoni haya ni maajabu?"

“Huyu mwenyekiti asituvuruge, tunatakiwa kujua chama kinaelekea wapi na tumefikaje hapa,” alisema Kilango na kueleza kuwa anaamini Mgeja katumwa, huku akiongeza:

"Ni bora pia atwambie (Mgeja) ametumwa na nani kwa kuwa anachozungumza ni kudanganya umma."

Kilango ambaye alikuwa akizungumza kwenye mahojiano maalumu na gazeti hili nyumbani kwake jijini Dar es Salaam jana, alisema anamshangaa mwenyekiti huyo kumwandama Sitta, badala ya kutafakari jinsi alivyopoteza majimbo manne ya ubunge mkoani Shinyanga.

"Huyu anataka tumkate panya mkia halafu aendelee kuishi badala ya kumkata kichwa ili kumaliza tatizo," alisema Kilango akimaanisha kuwa Mgeja anataka kukwepa hoja ya msingi kwa kuanza kuzungumzia mambo yasiyomhusu.

"Namsihi Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete, asikubali kuwa na viongozi ndani ya chama ambao wanataka kumkata panya mkia badala ya kumkata shingo ili afe," alisema Kilango.

Alisema hivi sasa CCM inatakiwa kuokoa chama kwa kufanya tathmini kujua chanzo cha wananchi kuwakataa, lakini sio kuzungumzia mambo yasiyo na msingi.

Desemba 19, mwaka huu, Sitta alitoa kauli nyingine inayoweza kutikisa CCM baada ya kueleza kuwa, aliondolewa kwenye kinyang'anyiro cha Spika wa Bunge kutokana na hila za viongozi, ambao walishindwa kuhimili kasi ya utendaji wake kwenye chombo cha kutunga sheria.

Mbunge huyo wa Urambo Mashariki, alijikuta akianguka kwenye kinyang'anyiro hicho baada ya CCM kwa kile kilichoelezwa kuwapa wanawake nafasi ya kuongoza moja ya mihimili ya nchi.
Chanzo: Mwananchi.

Sunday, December 26, 2010

JK AMTEUA MOHAMED CHANDE OTHMAN KUWA JAJI MKUU MPYA

                                                                                                      

                                    UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
                      DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
                                  Telephone: 255-22-2114512, 2116539
                                       E-mail: press@ikulu.go.tz
                                  Website: www.mawasilianoikulu.go.tz
                                       Fax: 255-22-2113425


                                       PRESIDENT’S OFFICE,
                                       THE STATE HOUSE,
                                        P.O. BOX 9120,
                                        DAR ES SALAAM.
                                        Tanzania.


                           TAARIFA YA IKULU
Rais Jakaya Mrisho Kikwete, amemteua Jaji Mohamed Chande Othman kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, kuanzia tarehe 28 Disemba, 2010.

Jaji Othman anachukua nafasi ya Jaji Augustino Ramadhani anayestaafu kwa mujibu wa sheria tarehe 27 Disemba, 2010.

Jaji Othman amekuwa Jaji wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufaa kwa muda miaka saba(7).

Kwa sasa Jaji Othman ni Jaji wa Mahakama ya Rufaa na pia ni mtaalamu binafsi juu ya hali ya Haki za Binadamu huko Kusini mwa Sudan, hadi mwezi Agosti 2011.

Jaji Othman alizaliwa tarehe 1 Januari, 1952, ana shahada ya kwanza ya Sheria (LLB) ya Chuo Kikuu cha Dar-Es-Salaam na Shahada ya Uzamili (MA) kutoka katika Chuo Kikuu cha Webster, Geneva-Uswisi.

Amewahi kuwa Makamu wa Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Rwanda huko Arusha na amewahi kushika nafasi sawa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali huko Timor Mashariki.

Jaji Othman pia, amewahi kufanya kazi ndani na nje ya nchi katika Mashirika mbalimbali ya Kitaifa na Kimataifa kama vile Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) na Shirika la Msalaba Mwekundu.

Jaji Othman ataapishwa kesho tarehe 27 Disemba, 2010 katika viwanja vya Ikulu saa 4:00 asubuhi.

                                      Michael P. Mwanda,
                                      Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi,
                                                 Ikulu.
                                          DAR ES SALAAM.
                                          26 Disemba, 2010

Saturday, December 25, 2010

Nazi Zao Yatima Hana Mzazi Hana Mlezi


Zao la Mnazi kwa biashara tukiamua tunaweza.

Nikianza kwa kunukuu maneno ya Rais Kikwete kuwa zao la minazi limepatwa na " Ugojwa usiotibika kwa sasa ",nakuwataka wakulima wa zao la mnazi kulima kokoa kama zao mbadala .Wazo kama hili si geni ,kwani hapo nyuma wakulima huko Mwanza walitakiwa kubadilisha zao la pamba kwa kahawa .

Inaniwia vigumu kukubaliana na Rais hasa pale alipowahakikishia wakulima wa zao la  minazi kuwa atawapa wataalamu kushirikiana nao ili kuweza kufanikisha zoezi hili la kubadilisha Mnazi kwa Kokoa, na ndiyo hapo sera ya kilimo kwanza ninapohisi kushindwa.

Lengo kuu la kilimo kwanza ni kumkomboa mkulima mdogo toka kilimo cha kuchumia tumbo hadi kilimo chenye kunyanyua kipato cha mkulima na serikali . Na ndipo hapo ninakuwa na shaka na mkulima wa minazi kumuona kuwa ni yatima hana mzazi wala mlezi.

Minazi mingi iliyopo imetokana na mashamba ya kurithi ambayo huenda tumerithi toka kwa wazee wetu ama mara baada ya harakati za ukombozi wananchi kujimilikisha kama matunda ya uhuru.

Kutokana na umri mrefu na kutoboreshwa mashamba kutokana na uwezo duni au tamaa za wenye mashamba kwa kuangalia mavuno bila kutahadhari uboreshwaji wa zao hilo kwa kukuza miche mipya na uwekaji wa mbolea , zao hili limejikuta siku hadi siku likiwa linatokomea.

Miaka ya 80 hadi 90 zao hili lilikuwa likishughulikiwa na Mradi wa Kitaifa wa Kuendeleza Zao la Mnazi , vipi iwezekane kutoa wataalamu kuwezesha kubadilishwa zao moja kwenda lengine na kusiwezekane kutoa wataalamu wa kuendeleza na kuboresha zao lililopo.

Ushauri wangu kwa wizara husika hasa ya kilimo na mazingira,jaribuni kufanya utafiti kujua jinsi gani ya kuokoa utowekaji wa zao la mnazi na pia ili serikali ijiridhishe haina budi kuchukua uzoefu wa nchi nyengine mfano wa  Sri lanka , kwani kisiwa hichi kinafaidika sana na zao la Mnazi.

Ukitazama athari iliyopo ni kuwa,zao la mnazi likiboreshwa litanyanyua kiwango cha maisha kwani nazi hutumika sana kwa mapishi,kutoa mafuta na ni kiburudisho cha koo na uboreshwaji wake utanyanyua uchumi kwa nchi na wananchi .

Zao la Mnazi ni alama kuu katika ukanda wa pwani ya Afrika Mashariki na ukiangalia kwa makini  kutokomea kwake ni sawa na kuondoa meno halisi na kuyabadili kwa meno bandia.Kutokana na umri mrefu na kutoboreshwa mashamba kutokana na uwezo duni au tamaa za wenye mashamba kwa kuangalia mavuno bila kutahadhari uboreshwaji wa zao hilo kwa kukuza miche mipya na uwekaji wa mbolea , zao hili limejikuta siku hadi siku likiwa linatokomea.

Miaka ya 80 hadi 90 zao hili lilikuwa likishughulikiwa na Mradi wa Kitaifa wa Kuendeleza Zao la Mnazi , vipi iwezekane kutoa wataalamu kuwezesha kubadilishwa zao moja kwenda lengine na kusiwezekane kutoa wataalamu wa kuendeleza na kuboresha zao lililopo.

Ushauri wangu kwa wizara husika hasa ya kilimo na mazingira,jaribuni kufanya utafiti kujua jinsi gani ya kuokoa utowekaji wa zao la mnazi na pia ili serikali ijiridhishe haina budi kuchukua uzoefu wa nchi nyengine mfano wa  Sri lanka, kwani kisiwa hichi kinafaidika sana na zao la Mnazi.

Ukitazama athari iliyopo ni kuwa,zao la mnazi likiboreshwa litanyanyua kiwango cha maisha kwani nazi hutumika sana kwa mapishi,kutoa mafuta na ni kiburudisho cha koo na uboreshwaji wake utanyanyua uchumi kwa nchi na wananchi .

Zao la Mnazi ni alama kuu katika ukanda wa pwani ya Afrika Mashariki na ukiangalia kwa makini kutokomea kwake ni sawa na kuondoa meno halisi na kuyabadili kwa meno ya bandia.

Majembe yaondolewa barabarani

Serikali imeiagiza Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), kuvunja mkataba na Kampuni ya Udalali ya Majembe Auction Mart ya jijini Dar es Salaam Desemba 31, mwaka huu.

Majembe ilipewa na Sumatra mkataba wa uwakala wa kusimamia shughuli za daladala jijini Dar es Salaam kwa miaka miwili kuanzia mapema mwaka huu.

Akizungumza na Waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu, alisema kuvunjwa kwa mkataba huo kutasaidia kupunguza kero zinazosababishwa na Majembe.

Nundu alisema wameamua kuuvunja mkataba huo kutokana na Majembe kuendelea kukiuka sheria na kanuni walizopewa wakati wa kabla ya kuanza kufanya kazi za uwakala.

Kwa Mujibu wa Waziri huyo, Majembe ilianza kufanya kazi ambazo haziwahusu na ambazo hawana ujuzi nazo, ikiwa ni pamoja na zile za usalama barabarani.

Alisema zipo baadhi ya kazi zinazotakiwa kufanya na askari wa kikosi cha usalama barabarani, lakini kinyume chake zimekuwa zikifanywa na Majembe, jambo ambalo ni kuingilia kazi zisizowahusu.

" Hii siyo sawa, hatutakiwi kuweka watu watufanyie kazi wasizo na uzoefu nazo…lazima tuweke mfumo madhubuti utakaotusaidia kutatua matatizo, si kuweka weka tu, watu wasio na utaalamu," alisisitiza.

Alisema baadhi ya kazi ambazo ni kinyume na sheria zinazofanywa na Majembe ni pamoja na kukagua magurudumu ya magari, leseni, bima, taa za magari na vioo.

Waziri huyo alisema ikiwa Sumatra watahitaji kuendelea kufanya kazi na Majembe, wanatakiwa wawape mafunzo maofisa wake kwanza kuhusu namna kufuata sheria za usalama barabarani.

Sumatra iliipa Kampuni hiyo mkataba huo kwa lengo la kuboresha usafiri wa umma na kuondoa kero kwa wakazi wa Dar es Salaam, kusimamia, kufuatia na kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa masharti ya leseni.

Kabla Majembe haijapewa mkataba huo, wakazi wa Dar es Salaam walikuwa wakilalamikia vitendo vya ukiukwaji wa sheria vilivyokuwa vikifanywa na daladala kama kukatisha safari, kushusha na kupakia abiria katika maeneo yasiyo na vituo, makondakta na madereva kutovaa sare, kutoza nauli za juu, matusi na kukataa kuwabeba wanafunzi.

Moja ya sababu ambazo hivi karibuni zilikuwa zikilalamikiwa na wamiliki wa mabasi ya mikoani na daladala dhidi ya Sumatra ni kuiruhusu Majembe kuweka wafanyakazi kufanya kazi za barabarani.

Mapema mwezi huu, wamiliki wa mabasi walitishia kugoma pamoja na mambo mengine, wakitaka kampuni hiyo isijihusishe na kazi za barabarani bila kuwepo na askari wa kikosi cha usalama barabarani..

Wakati huo huo; Serikali imetangaza kuwaondoa mara moja wapiga debe katika vituo vyote vya mabasi nchini.

Nundu alizitaka mamlaka zinazohusika kuandaa utaratibu wa kuwatambua wafanyakazi na mawakala wa makampuni ya mabasi kwa kuwapatia vitambulisho maalum.

Alisema utaratibu wa kuhakikisha wapiga debe wanaondoka katika vituo vya mabasi unatakiwa kufanyika sasa na kwamba ifikapo Januari 15, mwakani, utaratibu wa kutoa vitamburisho kwa wafanyakazi na mawakala unatakiwa uwe umekamilika.

" Ninaagiza kwamba kuanzia sasa ninataka kuona wapiga debe wote wameondolewa katika vituo vyote vya mabasi, na zoezi hili linatakiwa kufanyika haraka iwezekanavyo,” alisema.

Aliongeza kuwa wapigadebe wamekuwa kero kubwa kwa wasafiri hususani wa mikoani kusumbuliwa wanapokwenda kukata tiketi na wakati mwingine kuwaibia.

Kwa upande mwingine, Nundu alisema kuna umuhimu wa kuwepo kwa matuta barabarani ili kupunguza ajali zinazotokana na mwendo kasi.

Alisema Wizara yake kwa kushirikiana na ya Ujenzi, itachukua hatua mwafaka ili kuhakikisha ujenzi wa matuta barabarani unafuata viwango.

Alisema ukosefu wa matuta barabarani pia umekuwa ukisababisha uharibifu wa mabasi na hivyo kuongeza gharama za uendeshaji.
Chanzo: Nipashe

Ujumbe wa X-Mass



Zitto Kabwe:Aeleza Kulikoni Yake


Mbunge wa Kigoma kaskazini,
Mheshimiwa Zitto Kabwe

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Zitto Kabwe amesema kuwa hajapewa sumu kama ilivyokuwa imedaiwa huku akisisitiza kuwa hakuna binadamu anayeweza kufanya hivyo.Pia mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini, amesema hana nia wala mpango wa kukihama chama hicho.

Bw. Kabwe aliyasema hayo juzi wakati akiwahutubia mamia ya wananchi Mkoa wa Kigoma katika mkutano wake wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya kawawa ndani ya Manispaa ya Kigoma ujiji.

Alisema kuwa migogoro inayoendelea ndani ya chama chake isiwafanye wananchi wa Kigoma kuwa na hofu yeyote na hata yale yanayoandikwa na vyombo vya habari pia yasiwanyime rah,a waendelee kukisimamia chama chao.

"Wananchi wenzangu msiwe na wasiwasi, mimi ni mzima kabisa, yameandikwa mengi katika vyombo vya habari, mara nimepewa sumu, nataka niwahakikishie hizo habari si za kweli, mimi sijapewa sumu na hakuna binadamu anayeweza kunipa sumu, tuendelee kufanya kazi na kukijenga cha chetu," alisema Kabwe.

Siku za karubuni kumekuwapo na mgogoro ndani ya CHADEMA kutokana na mbunge huyo kutofautiana na wabunge wenzake kuhusu msimamowa kususia hotuba ya Rais jakaya Kikwete bungeni, hali iliyosababisha chama hicho kuundama kamati ya kuzungumza naye kumpa ushauri.hatua hiyo ilichukuliwa siku chache baada ya wabunge wenzake kupiga kura ya kutokuwa na imani naye, kama Naibu Kiongozi wa Kambi ya upinzani bungeni.

Wakati wabunge hao wanachukua uamuzi huo, Bw. Kabwe aliugua ghafla na kulazwa katika Hospitali ya Aga Khan akisumbuliwa na tumbo, na baadhi ya vyombo vya habari vililiripoti kuwa amelishwa sumu, ingawa madaktari walisema ni tumbo lake lilikuwa tu limechafuka.

Katika hatua nyingine Zitto aliitaka Wizara ya Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa (TAMISEMI) kuitisha uchaguzi wa meya wa Kigoma/Ujiji haraka ndani ya wiki mmoja uliokuwa umesimamishwa wiki iliyopita kutokana na mgogoro wa mgawanyo wa madiwani wa viti maalumu.

"Halmashauri zingine tayari zimeshafanya uchaguzi na wamepata meya, na kazi za kuleta maendeleo wameshaanza, sasa wao wanapozidi kutucheleshea sisi kufanya uchaguzi, wajue na kazi ya kuleta maendeleo katika manispaa yetu inazidi kuchelewa," alisema Bw. Kabwe.

Mbunge huyo amewataka viongozi wa vyama mbalimbali nchini kutumia fursa walizozipata katika kuleta maendeleo ya jamii na sio kuendekeza uadui na serikali kuu.
Chanzo: Majira

Friday, December 24, 2010

Ruzuku: CCM milioni 800/-, Chadema 200/-, CUF 117/-


Msajili wa Vyama vya Siasa,John Tendwa
Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, ametangaza viwango vya mgawo wa ruzuku kwa vyama vilivyotimiza sifa, baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, huku kiwango cha mgawo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ilichokuwa ikipata kila mwezi, kikiwa kimeshuka.


Licha ya CCM kuvipita vyama vingine katika viwango vya mgawo uliotangazwa jana na Tendwa, kiwango cha mgawo wake wa ruzuku, kimeshuka kutoka Shilingi bilioni moja ilizokuwa ikipata kila mwezi katika kipindi cha miaka mitano iliyopita kufikia Sh. milioni 800 inazopata hivi sasa.

Kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi, ruzuku hiyo hutolewa kwa chama kilichofikisha kuanzia asilimia tano ya kura za urais na kwa uwiano wa wabunge na madiwani, ambao chama ‘kilivuna’ katika uchaguzi huo.

Mbali na CCM, vyama vingine, ambavyo vinapata ruzuku, baadhi vikilingana na vingine vikitofautiana sifa ya kupata ruzuku hiyo, ni Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi, UDP na TLP. Viwango vya mgawo wa ruzuku hiyo, vilitangazwa na Tendwa alipozungumza na NIPASHE katika mahojiano maalum ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana.

Alisema ruzuku hiyo ilianza kutolewa na ofisi yake kwa vyama hivyo, kuanzia Novemba, baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika nchini Oktoba 31, mwaka huu na ule uliofanyika baadaye katika baadhi ya majimbo kukamilisha uchaguzi huo.

“CCM imeshuka kwa ruzuku. Huko nyuma ilikuwa inapata Shilingi bilioni moja, lakini sasa inapata Sh. milioni 818,” alisema Tendwa.

Hata hivyo, alisema ruzuku kwa uwiano wa madiwani, haijaanza kutolewa kwa vile bado hawajapata takwimu za madiwani, ambao kila chama kilipata, katika uchaguzi huo. “Tunasubiri tuweze kuwa na data za madiwani. Hatuwezi kutoa ruzuku za madiwani bila kupata data. Kwa mfano CCM kuna madiwani wamejiuzulu. Kila mgawo (wa ubunge na madiwani) una fungu lake,” alisema Tendwa. Alisema CCM inapata kiwango hicho, kutokana na kupata asilimia 60.40 ya kura za urais katika uchaguzi huo, ambazo ni sawa na Sh. milioni 354 na asilimia 77 ya wabunge (sawa na Sh. milioni 460) kwa mwezi.

Pia alisema licha ya Chama cha Wananchi (CUF) kupata kura katika majimbo mengi ya uchaguzi, kimepata kiwango kidogo cha mgawo wa ruzuku kulinganisha na Chadema. Alisema hali hiyo inatokana na baadhi ya majimbo kiliyovuna wabunge, kama vile ya kisiwani Pemba kuwa na wapigakura wachache waliokiunga mkono katika uchaguzi huo.

“CUF ilipeleka nguvu kubwa Pemba, lakini huwezi kulinganisha na idadi ya wapigakura kama wa Dar es Salaam,” alisema Tendwa.

Kutokana na hali hiyo, alisema CUF sasa inapata Sh. milioni 117.4, kutokana na kupata asilimia 9.80 ya kura za urais (sawa na Sh. milioni 57.9) na asilimia 10 ya wabunge (sawa na Sh. milioni 56). Alisema katika mgawo huo, Chadema inapata Sh. milioni 203.6, kutokana na kupata asilimia 24 ya kura za urais (sawa na Sh. milioni 146) na asilimia 9.62 ya wabunge (sawa na Sh. milioni milioni 56).

Tendwa alisema vyama vya NCCR-Mageuzi, UDP na TLP havipati ruzuku ya urais kwa vile vilipata chini ya asilimia tano ya kura za urais.

Hata hivyo, alisema NCCR-Mageuzi inapata ruzuku ya Sh. milioni 10, kutokana na kupata asilimia 1.08 ya wabunge wakati UDP na TLP alisema vinapata ruzuku ya Sh. milioni 2.4 kutokana na kupata asilimia 0.42 ya kura za ubunge kila kimoja.

Alisema iwapo viwango vya mgawo wa ruzuku ya madiwani itaongezeka kwa chama husika, viwango hivyo navyo pia vitaongezeka.

Kuhusu fomu za gharama za uchaguzi, ambazo wagombea wanatakiwa kujaza, alisema tarehe ya mwisho, ambayo zinatakiwa ziwe zimerejeshwa ofisini kwake, ni Januari 30, mwakani na kwamba, yeyote atakayekiuka ataadhibiwa kwa mujibu wa sheria. “Wanatakiwa waeleze katika hizo fomu walitumia nini, kiasi gani na kutoka wapi. Wathibitishe kwa risiti,” alisema Tendwa.

Akijibu swali kama kuna mgombea yeyote, ambaye hakujaza fomu, alisema hakuna, isipokuwa aliyekuwa mgombea ubunge kupitia TLP Jimbo la Mtama, mkoani Lindi, Ndaka Wolfugang ndiye aliyechelewa kujaza fomu hiyo.

Kutokana na kasoro hiyo, alisema ofisi yake (Msajili) ilimwekea pingamizi Wolfugang, lakini akarudishwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwania nafasi hiyo kwa maelezo kwamba, kuchelewa kwake kujaza fomu hiyo, kulitokana na kuwekewa pingamizi na aliyekuwa mgombea kupitia CCM, Bernard Membe, ambalo baadaye lilitupwa.
Chanzo: Nipashe

Thursday, December 23, 2010

Christmas Shoes-Nawatakia Maandalizi Mema Ya Krismasi

Nasikitika tukielekea kwenye sherehe ya krismasi wapo watu mikono yao imejaa damu,na kuwa ni wao ndiyo wenye dhamana na haki juu ya maisha ya viumbe wengine.


Hebu Tusahau machungu hayo,kwa kuonyesha kujali kwa umpendae

Umuhimu wa Vyeti Vya Kuzaliwa

Mara nyingi,umuhimu wa vyeti vya kuzaliwa hauji mpaka kuwe na jambo la kisheria linalokukabili. Kutokana na umuhimu wake ni vyema wazazi na vijana mliofikia umri wa kujitegemea kuanza kulifikiria, kwani athari yake unaweza kupoteza haki zako za msingi kama raia na hata kutiliwa shaka uraia wako.

Naandika haya kwa ushahidi mkubwa wa mambo yalivyojitokeza nyuma hasa ukiwa unakumbuka kunyang'anywa uraia wa Jenerali Twaha Ulimwengu na Marehemu Ali Nabwa.

Kuhifadhi cheti cha kuzaliwa ni muhimu kwani ushahidi wake unatambulika kisheria,kumbuka wakati wa mchakato wa kutafuta wagombea wa ubunge wa CCM kulijitokeza mgogoro baada ya Mgombea toka Nzega kukataliwa na chama chake kwa madai ya kutokuwa raia.

 Hussein Bashe ilimlazimu si tu kumuhatarisha uanachama wake katika CCM bali kubwa kuliko yote ni haki nzima ya uraia kama Mtanzania, kwa kuwa alithibitisha uraia wake wa kuzaliwa kwa kigezo hicho Idara ya Uhamiaji ilijiridhisha kuwa ni raia halali.

Leo hii,licha ya uthibitisho wa kuzaliwa ,masomo na nyadhifa mbali mbali alizopitia Marekani, Rais Barack Obama wapo watu wanaodai kutaka uthibitisho wake wa kuzaliwa huko Honolulu,Hawaii.

Picha inayonijia ni kuwa kuhifadhi vyeti vya kuzaliwa ni muhimu kwa ajili kupata haki zako za msingi za kisheria kama raia.

Ijapokuwa Obama na familia yake wapo Hawaii ambako ina aminika ndiko alikozaliwa  katika mapumziko ya Krismasi,lakini swali la uhalali wa cheti cha kuzaliwa kwake huko Honolulu ,Hawaii bado ni tete.


Benitez apigwa chini Inter

Inter Milan ya Italia imethibitisha kuwa imemfukuza kazi meneja Rafael Benitez, miezi sita tu baada ya kuteuliwa kuiongoza klabu hiyo.

Hatua hiyo imekuja baada ya Benitez kutaka kuungwa mkono ndani ya bodi ya wakurugenzi kununua wachezaji, kufuatia klabu hiyo kushinda kombe la dunia la vilabu, kwa kuifunga TP Mazembe siku ya Jumamosi.

Badala yake, Inter, ambayo inasuasua katika nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi ya Serie A, imeamua kumfukuza kazi Benitez.
Benitez
'Jino la pembe' Moratti na Benitez
Benitez alichukua kazi hiyo San Siro kutoka kwa Jose Mourinho.

Mourinho, ambaye aliondoka Inter na kwenda Real Madrid ya Uhispania, aliiongoza timu hiyo kuchukua ubingwa wa ligi ya Italia na klabu bingwa Ulaya msimu uliopita na kumuachia Benitez kazi ngumu ya kufuata nyayo zake.

Benitez, alichukua majukumu ya San Siro wiki moja baada ya kuondoka Liverpool ya England Juni 3. Ingawa amekuwa na majeruhi kadhaa, lakini imeonekana kuwa mbinu zake hazijaweza kumsaidia.

Ingawa Inter ina kiporo cha mechi mbili dhidi ya timu zilizo juu yake, imeshinda mechi sita tu kati ya mechi 15 za ligi.
katika kutetea ubingwa wao wa klabu bingwa, Inter imeweza kumaliza katika nafasi ya pili ya makundi, nyuma ya Tottenham ya England, na kuiacha katika wakati mgumu kwani itapambana na Bayern Munich katika raundi ya timu 16.

Ingawa Inter imeshinda Kombe la Dunia la Vilabu kwa kuichapa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, mafaniko hayo hayakumfanya Benitez kutotoa dukuduku lake baada ya mchezo huo wa fainali
Soma zaidi.....BBC


Wednesday, December 22, 2010

Nundu Aitaka Mamlaka Ya Usimamizi wa Bandari Kufanya kazi Kiufanisi

SERIKALI imeiagiza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), kwa kushirikiana na Kamati ya Kuboresha huduma bandarini kuhakikisha kwamba kuanzia sasa muda wa uondoshaji wa kontena katika Bandari ya Dar es Salaam unapungua ili TPA iendelee na jukumu lake la kuboresha huduma hiyo na kuleta ufanisi zaidi.

Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu ameitaka TPA kuanza mara moja kujenga na kuimarisha miundombinu ya bandari kwa kuzingatia mpango mkuu wa Mamlaka na kwamba mpango huo ni dira ya kuendeleza na hatimaye kufikiwa kwa lengo la nchi la kuifungua kibiashara ndani na nje ya nchi.

Nundu aliyasema hayo jana Dar es Salaam katika majumuisho ya ziara yake ya siku mbili ya kutembelea TPA ili kuona na kujifunza mambo muhimu ya uendeshaji na uendelezaji wa Bandari ya Dar es Salaam.

Akiongozana na Naibu wake, Dk. Athuman Mfutakamba, Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ephraim Mgawe na viongozi wengine wa bandari, Waziri Nundu alipata pia fursa ya kutembelea baadhi ya kampuni za kuhifadhi mizigo ya bandarini kwa lengo la kufahamu changamoto mbalimbali zinazoikabili mamlaka hiyo.


Alisema wakati ujenzi wa bandari ya Mwambani, Tanga ukiendelea, TPA inununue vifaa vitakavyoongeza ufanisi wa matumizi ya bandari hiyo na kusisitiza shirika lianze mawasiliano na uongozi wa Tanga ili maeneo ya ndani na nje ya bandari yanayotumika kwa shughuli zisizo za kibandari, zichukuliwe na kumilikishwa TPA.

Aidha, alisema mchakato wa kufanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina eneo la Kisarawe kwa ajili ya matumizi ya kuhifadhi mizigo, ufanyike mara moja hata kama ni kwa gharama za serikali na kuongeza kuwa ni vyema hilo likafanyika kabla ya mwaka wa fedha 2011/11 haujamalizika.

Alisisitiza wafanyakazi wa TPA kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma na matakwa ya wateja, na kuwa mawasiliano kati ya mamlaka na wateja yawe ya haraka na yenye tija.
Chanzo: Habari Leo

Tuesday, December 21, 2010

Kulikoni India?

Katika Miezi 6 wanachama wa baraza la usalama la UN wametembelea India
Yaahidiwa kiti cha Uanachama wa baraza la usalama la UN
Yaweka mikataba lukuki ya kibiashara,kijeshi,nishati ya nyuklia na mafuta

Made in  .............India
 
Sikiliza kibao hiki

Made In India

Upload Music
 
Cameron akiwa India-July 28,2010


Obama akiwa India- Nov 8,2010
Manmohan Singh U.S. President Barack Obama (L) waves as he is embraced by Indian Prime Minister Manmohan Singh (R) after speaking during a joint press conference at Hyderabad House on November 8, 2010 in New Delhi, India. The US President and the First Lady is on a ten day Asia tour with stops in India as well as Indonesia, South Korea and Japan.

Sarkozy(Rais wa Ufaransa)-Dec 6,2010


Wen Jiabao(Waziri Mkuu wa China)-Dec 16,2010


Medvedev(Rais wa Urusi)-Dec 21,2010

Hoseah amlipua Kikwete

 Asema anaogopa kushughulikia ufisadi wa vigogo


MTANDAO wa Wikileaks wa Marekani umeibua siri nzito kuhusu uwezo na nia ya Rais Jakaya Kikwete katika kushughulikia ufisadi, ukidai kuwa ndiye anayekwamisha kushtakiwa kwa baadhi ya vigogo serikalini wanaotuhumiwa kuhusika katika rushwa kubwa nchini.

Katika taarifa hiyo iliyochapishwa jana na gazeti la The Guardian  la Uingereza, likinuu taarifa za kibalozi za Marekani zilizoanikwa na Wikileaks, lilisema Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea, alimweleza mwanadiplomasia mmoja wa Kimarekani kwamba ugumu wa kupambana na ufisadi Tanzania unaanzia Ikulu.

Mtandao huo ulinukuu baadhi ya maelezo ya faragha kuhusu rushwa aliyoyatoa Dk. Hosea kwa mwanadiplomasia wa Kimarekani aitwaye Purnell Delly, walipokutana mwezi Julai mwaka 2007, Dar es Salaam.

Likinukuu mtandao huo, The Guardian liliandika, “Dk. Hosea alidokeza kuwa Rais Kikwete hafurahishwi na sheria kuchukua mkondo wake dhidi ya ufisadi ambao unaweza kuwatia hatiani vigogo wa ngazi za juu serikalini…. Hataki kuweka msingi wa kumwandama kiongozi yeyote miongoni mwa watangulizi wake (wastaafu).”

Linasema mwanadiplomasia huyo alisema: “Hosea alikuwa akisisitiza kwamba akiamua kuwa na makali, usalama wake binafsi utakuwa hatarini…anadai anaamini maisha yake yako hatarini, kwani amekuwa akipokea ujumbe wa vitisho kwa simu na barua na amekuwa akikumbushwa kila siku kwamba anapambana na ‘watu matajiri na wenye nguvu.’”

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Dk. Hosea alitoa maelezo yanayokatisha tamaa juu ya mustakabali wa mapambano dhidi ya ufisadi nchini na ugumu uliopo katika kuwashtaki watuhumiwa wa ufisadi mkubwa.

“Alituambia bila kufafanua... kwamba kesi zinazomhusu waziri mkuu au rais haziwezi kujadiliwa kabisa,” kilisema chombo hicho na kisha kufafanua: “Rais Kikwete hataki kumshughulikia mtangulizi wake yeyote mwenye tuhuma zinazostahili kufikishwa mahakamani.”

Dk. Hoseah anadaiwa kumueleza mwanadiplomasia huyo jinsi rushwa ilivyokithiri katika Benki Kuu ya Tanzania na visiwani Zanzibar, lakini akadokeza ugumu wa kuishughulikia kwa sababu tu wahusika wakuu ni watu ambao “hawahusiki”.

Hoseah alidokeza kuwa mambo yakiwa mabaya angeweza hata kukimbia nchi, kwa mujibu wa taarifa hiyo ikimnukuu mwanadiplomasia huyo wa Marekani.

“Ukihudhuria kwenye vikao vya juu (vya ndani), watu wanataka ujisikie kuwa wao ndio wamekuweka hapo ulipo. Wakiona huenendi na yale wanayotaka wao, basi hapo unakuwa katika hatari,” ilisema sehemu nyingine ya taarifa hiyo ikinukuu maelezo ya Dk. Hoseah.

Aidha, katika mazungumzo yao, Dk. Hoseah alimpa matumaini mwanadiplomasia huyo kwamba TAKUKURU ingeweza kuwachukulia hatua za kisheria watuhumiwa wote waliohusika katika kile alichokiita ‘dili chafu’ ya rushwa katika ununuzi wa rada ya kijeshi kutoka kampuni ya BAE ya Uingereza, hatua ambayo hata hivyo ilionekana isingeweza kutekelezwa na taasisi hiyo.

Wachambuzi wa mambo wanasema kauli hiyo ya Dk. Hoseah ilitokana na ukweli kwamba tayari wapelelezi wa Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa ya Jinai ya Uingereza (SFO) walikuwa wameshampelekea faili lote la watuhumiwa likiwa na ushahidi jambo ambalo lingeweza kumuepusha na hatari ambayo ingeweza kumfika kama uchunguzi huo ungefanywa na TAKUKURU yake.

Katika kashfa hiyo, serikali ya Tanzania inadaiwa kununua rada ya kuongozea ndege za kiraia na za kivita kutoka kampuni ya BAE System ya Uingereza kwa gharama kubwa ya dola 40 milioni, huku taarifa za uchunguzi kutoka SFO na vyanzo mbalimbali zikionyesha kuwa ununuzi huo haukuwa wa lazima na uligubikwa na rushwa.

Kashfa ya rada ilitendeka mwaka 1999, katika mazingira yaliyogubikwa na rushwa kwa watendaji serikalini ili waweze kulainisha watoa maamuzi. Kwa mujibu wa taarifa za maelezo ya Dk. Hoseah kwa mwanadiplomasia huyo, watuhumiwa zaidi wa rushwa ya rada wapo katika Wizara ya Ulinzi na jeshini.

“Dk. Hoseah aliliita suala la rada kuwa ni dili chafu na kusema inawahusu maofisa wa Wizara ya Ulinzi na vigogo wawili au mmoja wa jeshi (hawakutajwa majina),” ilieleza taarifa hiyo.

Kesi ya rada iliendelea kusikilizwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi jijini London, Uingereza .
Chanzo: Tanzania Daima

Rais Kibaki aahidi kuwalinda Wakenya baada ya watu 3 kuuwawa kwenye mlipuko Nairobi

      
    Rais wa Kenya,MwaiKibaki

Rais wa Kenya, Mwai Kibaki amesema usalama utaimarishwa msimu huu wa sikukuu ya Krisamasi kufuatia mlipuko wa bomu lililotokea jana mjini Nairobi.

Kamishna wa polisi nchini Kenya, Mathew Iteere, amesema uchunguzi umeanza kubaini kama mlipuko uliowaua watu 3 na kuwajeruhi wengine wapatao 40 mjini Nairobi jana jioni, ni shambulio la kigaidi.

Mlipuko huo uliotokea kwenye basi moja la kuelekea Kampala, Uganda. Kamishna Iteere, hakuuleza mlipuko huo kuwa shambulio la kigaidi, lakini amesema umesababishwa na kifaa cha kulipuka kilichokuwa sehemu ya mzigo wa abiria. Bwana Iteere pia amesema uchunguzi umeanza kubaini waliohusika kufanya hujuma hiyo.
Chanzo: Dw

Monday, December 20, 2010

Sitta: Nilitemwa uspika kwa hila za vigogo

Wastaafu wakibadilishana mawazo ya uongozi

Toka shoto Waziri mkuu mstaafu Edward Lowasa
na kulia ni Spika Mstaafu Samuel Sitta.

WAZIRI wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta jana alitoa kauli nyingine inayoweza kukitikisa chama chake cha CCM baada ya kueleza kuwa aliondolewa kwenye kinyang'anyiro cha kiti cha spika wa Bunge la Muungano kutokana na hila za viongozi ambao walishindwa kuhimili kasi ya utendaji wake kwenye chombo hicho cha kutunga sheria.


Sitta, ambaye alipata umaarufu baada ya kuliongoza Bunge la Tisa kwa mafanikio, ametoa kauli hiyo wiki chache baada ya kukaririwa na vyombo vya habari akisema bayana kuwa kuilipa kampuni tata ya Dowans fidia iliyoamuliwa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Kibiashara (ICC) ni sawa na kuhujumu uchumi.

Mbunge huyo wa Urambo Mashariki alijikuta akianguka kwenye kinyang'anyiro cha uspika wa Bunge la Kumi baada ya chama chake cha CCM kuamua kuwapa wanawake nafasi ya kuongoza moja ya mihimili ya nchi na hivyo kupitisha wagombea watatu wanawake katika mchakato uliompa ushindi Anne Makinda.

Jana, Sitta ambaye alikuwa akihojiwa na Mwananchi, alisema utendaji wake wa kasi na viwango uliwatisha viongozi wengi wa serikali na ndio maana wakaamua kutumia kigezo cha jinsia kumwondoa.
"Unajua nataka hili ilieleweke; juzi nilienda jimboni kwangu Urambo Mashariki nikawaeleza wapiga kura wangu kwa nini sasa mimi sio spika tena, maana wanaweza kudanganywa kama kazi imenishinda au nimefukuzwa," alisema Sitta.

"Watanzania lazima wajue mimi sijafukuzwa kazi wala sijashindwa kufanya kazi hiyo, ila kuna viongozi ambao ni wakuu wangu ndani ya chama chetu ambao wameshindwa kuendana na kasi na viwango vyangu ndio maana wakaamua kuweka sharti ambalo kamwe nisingeweza kulitimiza.

"Kigezo hicho cha jinsia walikileta katika hatua za mwisho za mchakato wa kumtafuta spika wakijua kwamba sitaweza kukitimiza na ningejua hilo mapema, nisingepeleka jina langu kuomba kuteuliwa tena."

Sitta alisema ni wazi kamba asingeweza kutimiza sharti kwamba spika aliyetakiwa safari hii ni mwanamke ndio maana hakuweza kuteuliwa tena kuwania nafsi hiyo.

"Mimi ni Sitta na nitabaki kuwa Sitita yule yule kama nilivyozaliwa na kwa vyovyote vile; nisingeweza kufanya chochote ili kuhakikisha sharti hilo nalitimiza," alisema Sitta.

Hata hivyo Sitta alisema kuwa endapo jina lake lingepitishwa, alikuwa na ukakika wa kurudi katika kiti hicho kwa kuwa asilimia kubwa ya wabunge walikuwa wameukubali utendaji wake.

Katika miaka ya mwisho ya uongozi wake wa Bunge la Tisa, Sitta alikuwa akilalamikia kuwepo kwa njama alizodai zinafanywa na mafisadi kutaka kumuangusha kwenye ubunge na wakati fulani alifikia hadi kuomba ulinzi zaidi kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda akisema anatishiwa maisha.

Sitta hajawahi kuwataka hadharani wapinazani wake, lakini baadhi ya vyombo vya habari viliwahi kumuhusisha na vita vya uwaziri mkuu, lakini akakanusha vikali akisema kama angetaka nafasi hiyo asingegombea uspika.

Sitta aliwataka wapigakura wake na Watanzania kwa ujumla kutosikitishwa na kitendo cha kuenguliwa kwenye kinyang'anyiro cha uspika, akisema kuwa anaamini bado Rais Jakaya Kikwete anawapenda watu wa Urambo na kuendelea kuwaheshimu ndio maana amemteua kushika dhamana nyingine.

"Nawaahidi Watanzania huu sio mwisho wa utendaji wangu wa kazi sasa kasi na viwango navihamishia katika Wizara hii muhimu na kwamba wananchi wasiogope tena Tanzania kuingia katika Shirikisho la Afrika Mashariki,"alisema.

Alisema akiwa Waziri wa Afrika Mashariki atahakikisha Watanzania wanafaidika na shirikisho hilo na kwamba suala la ardhi halitakuwepo kwa kuwa tahadhari zote zimechukuliwa.

Sitta alifanya ziara kwenye jimbo lake la Urambo Mashariki ambako pamoja na mambo mengine, alihudhuria mkutano wa uchaguzi wa mwenyekiti wa halmshauri ya Urambo.

Katika mkutano huo, Alhaji Adam Malunkwi wa CCM alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa halmashauri hiyo.
Kabla ya mkutano huo, Sitta, ambaye alipokewa na wapigakura wake kwa msafara wa pikipiki zaidi ya 70, magari zaidi ya 40 na vikundi mbalimbali vya hamasa, alitumia fursa hiyo kuwaeleza wapigakura hao kilichomfanya ashindwe kutetea nafasi yake ya uspika.

Sitta pia alitoa msaada wa mashine ya kusaga na kukoboa nafaka kwa kikundi cha kinamama wa Uyogo kutekeleza ahadi yake kabla ya uchaguzi mkuu

Alisema mashine hiyo itakuwa kitega uchumi chao kwa kile anachoamini kuwa ukimwezesha mama, umeiwezesha jamii.

Mbali na mashine hiyo Sitta pia alitoa msaada wa mashine ya umeme wa sola kwa ajili ya zahanati ya Uyogo.

Akikabidhi msaada huo alisema kabla ya umeme haujasambaa maeneo hayo, atahakikisha zahanati zote zinapata umeme huo kurahisisha huduma zake kwa jamii.

Chanzo: Mwananchi

Saturday, December 18, 2010

Pinda Avunja Ukimya Kuhusu Katiba Mpya

Aeleza kuhusu Dowans
Ofisi ya kadhi
Mkataba wa Tido Mhando

Friday, December 17, 2010

Angalia Athari Ya Mabadiliko Ya Hali Ya Hewa

Mashariki Ya Kati(Dec 13,2010)


Ulaya Viwanja Vya ndege ,shule na huduma nyengine zimesimama
(dec 18,2010 )

Cancun Na Kutofikiwa Makubaliano Ya Mabadiliko Ya Hali Ya Hewa

Ikiwa ni muendelezo wa mikutano mingi kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa kama wa Kyoto,Copehagen na kwa mara nyengine  mkutano wa Cancun, Mexico umeendeleza kile kinachoonekana kufeli kwa makubaliano baina ya nchi tajiri na maskini kuhusu upunguzaji wa uzalishaji wa kaboni kwa digrii 4 kabla 2060.

Inasemekana 20% ya uzalishaji wa kaboni dunia inatoka Nchi zinazoendelea kutokana na uchomaji misitu hali nchi zilizoendelea zikiwa vinara wa uzalishaji wa kaboni kutokana na matumizi ya viwanda.

Benki ya dunia kama mdhamini wa mabadiliko ya hali ya hewa duniani imekutwa na kashfa ya kutokuwa makini katika mambo yake hasa linapokuja suala la uchumi na nchi matajiri.Ni taasisi inayoendeshwa na mataifa tajiri  na kuzinyima sauti nchi maskini kwenye maamuzi makubwa ya uchumi wa dunia.
                   
 

 WIKILEAKS ilipiga msumari wa dau pale ilipotoa kashfa kuhusu nchi matajiri kutumia pesa za kuchangia kupunguza mabadiliko ya hali ya hewa kwa nchi maskini kama rushwa ili kudhoofisha lengo la nchi tajiri kupunguza uzalishaji wa kaboni. Pesa hizi zinatolewa na nchi tajiri na kusimamiwa na Benki ya dunia,taasisi ambayo nchi maskini hazina imani nayo kutokana na uendeshwaji wake kutokuwa wa kidemokrasia.

Kabla ya mkutano wa Cancun nchi kama Marekani ilitishia kujitoa mkutanoni  kama matakwa yake hayata timizwa,Japan nayo ikisisitiza utekelezwaji wa makubaliano ya Kyoto hali Urusi ikishinikiza kuwa kama Japan haita ahidi  zaidi ya makubaliano ya Kyoto basi na wao hawako tayari.

Ingawa kulikuwa na shinikizo kubwa toka Marekani,nchi zinazoendelea na Ngo's ilikufikia mkataba mwengine unaolingana na ule wa Kyoto.Lakini juhudi hizo hazikuleta mabadiliko yoyote na kubaki kukubalina kutokubaliana.

Ikiwa maafikiano hayatafikiwa ili kutekeleza lengo la upunguzaji wa uzalishaji wa kaboni duniani kwa digrii 4 kabla ya mwaka 2060,watu na viumbe wengi duniani wataendelea kuathirika na mabadiliko ya hali ya hali ya hewa ambayo hawakuya sababisha kutokana na usaliti wa viongozi wao.

Mkataba wa Kyoto ndiyo mkataba rasmi unaotambulikana na umoja wa mataifa. na kutofikiwa makubaliano baina ya nchi tajiri na maskini ,mkataba wa Kyoto unaelekea kufa taratibu.
Chanzo:  Conspiracy

Athari ya mabadiliko ya hali hewa(The day after tomorrow)

Rais Sarkozy amemtaka Gbagbo angatuke

Rais wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy amemtaka kiongozi aliyeng'ang'ania madarakani nchini Ivory Coast Laurent Gbagbo aondoke kabla ya mwisho wa wiki, la sivyo atakabiliwa na vikwazo vya Muungano wa Ulaya.

Rais Sarkozy
Rais wa Ufaransa, Nicolas Sarkozy

Bw.Gbagbo amepinga miito ya Kimataifa ya kung'atuka madarakani kufuatia uchaguzi wa Rais uliomalizika mwezi uliopita.


Yeye pamoja na kiongozi wa upinzani Alassane Ouattara walidai kuwa wameshinda na kuzusha wasiwasi wa uwezekano wa kuzuka mapigano ya nchini.

Wafuasi wa Ouattara wanasema watafanya maandamano mitaani, siku moja baada ya miliyo ya risasi katika mji mkuu Abidjan.

Rais Sarkozy ameonya kwa kusema kuwa majaliwa ya Bw.Gbagbo na mke wake ni jukumu lao kwa sasa. Na ikiwa ifikao mwisho wa wiki hii hawajaachilia hatamu za uongozi wanaoshikilia kinyume cha chaguo la raia wa Ivory Coast, wataorodheshwa jina kwa jina kwenye orodha ya watu waliopigwa marufuku na Muungano wa Ulaya.

Afisa wa ngazi ya juu wa Marekani naye amenukuliwa akisema kuwa Bw.Gbagbo amepewa mda wa kutosha aondoke la sivyo atawekewa vikwazo vya kusafiri na pia vikwazo vya fedha zake.

Afisa ambaye hakutambulishwa amesema kuwa Gbagbo na familia yake wana nyumba kadhaa katika nchi nyingi ambako angeweza kuhamia lakini asipotii masharti haya huenda akapoteza fursa hiyo na nyumba hizo kuwa marufuku kwake.

Mwandishi wa BBC amesema kuwa hili litawashangaza raia wengi wa Ivory Coast ambao hawakujua siri hiyo wakimuona Gbagbo kama mzalendo anayepigania na kuipenda nchi yake bila kuwa na mali nje.

Watu ishirini waliuawa siku ya alhamisi wakati wafuasi wa Bw Ouattara walipojaribu kuandamana wakielekea kituo cha televisheni ya Taifa na kukabiliana na vikosi vinavyomtii Bw.Gbagbo.

Msemaji wa Bw.Gbagbo alisema kuwa waandamanaji 10 na askari 10 wa jeshi waliuawa.
Maofisa wa kambi ya Bw.Ouattara walitaja idadi ya wafu kuwa 30 na zaidi.

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeonya kuwa pande zote mbili zitawajibishwa chini ya sheria ya Kimataifa kwa shambulio lolote dhidi ya raia.

Umoja wa Mataifa pamoja na viongozi wa Umoja wa Afrika na nchi za magharibi wamemuunga mkono Bw.Ouattara kama mshindi wa Uchaguzi uliofanywa huko Ivory Coast.

Chanzo: BBC

Larry King Astaafu Baada Ya Miaka 25 ya CNN-Larry King Live

Atakumbukwa kwa kipindi chake cha mahojiano na watu Maarufu
Maswali yake yaliibua siri nyingi zilizofichika.

Katika muda wa miaka 53 ya utangazaji,King amefanya mahojiano 53000 kati ya hizo 6120 zipo kwenye kumbukumbu za CNN.Amepata tuzo mbalimbali za kuendesha mahojiano na miongoni mwao ni tuzo ya GUINESS kwa kushikilia rekodi ya muda  mrefu ya kuendesha kipindi  na kwa kufata muda .

Akikumbushia jinsi mazingira wakati anaanza kufanya kazi alisema"wakati ninaanza miaka 25 iliyopita katika ofisi ndogo katika jiji la Washington sikudhani kama itanichukua muda mrefu au kumaliza kama hivi".

Larry King atakuwa akiwajibika kwenye shughuli muhimu za CNN.

Zaidi: CNN


Kwa heri Larry King Nyayo zako ni ngumu kuzifuta


Mrithi wake ni Mwandishi wa habari za Udaku wa Uingereza Piers Morgan
Maarufu Marekani kama Jaji wa America's Got Talent

Mwinyi:Kwanini Mnaharakia Katiba Mpya?

Rais mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi amesema haoni umuhimu wa katiba mpya kwa sasa,nakuwataka wanaotoa madai ya katiba mpya kueleza maeneo gani ya kurekebishwa kwenye katiba ya sasa.

Rais Mstaafu,Ali Hassan Mwinyi

Alikuwa akijibu swali kwenye mahojiano na waandishi wa habari lililomtaka kujua msimamo wake juu ya kauli za madai ya katiba mpya.Mwinyi alisema"hakubaliani na wazo la kuwa na katiba mpya kwani kwasasa si muda muafaka".

Alisema"kabla ya kubadili katiba ya sasa,Watanzania wajiulize wenyewe ni kwa manufaa ya nani na kwa lengo gani lakutaka mabadiliko ".Hata hivyo,Mwinyi alisema ipo nafasi ya mazungumzo,lakini akapingana na wale wanaotoa madai ya haraka ,kama vile nchi imekosa kitu muhimu.

  Wakati Mwinyi akiyasema hayo, Profesa Lipumba mwenyekiti wa chama cha CUF amewataka watanzania kuungana katika madai ya katiba mpya. Alisema katiba mpya itasaidia kuwa na demokrasia ya kweli itakayo kuwa msingi kwa muelekeo wa maendeleo ya taifa kwani umuhimu wake kwasasa ni kwa faida ya vizazi vya sasa na baadae.

Habari kamili ,gonga hapa Guardian

Thursday, December 16, 2010

Fainali Za FIFA CWC 2010 Ni TP Mazembe Vs Inter Milan -Mazembe Fahari Ya Afrika

Fainali itachezwa Jumamosi 18/12/2010
Sherehe kama hii tunaitaka tena


Inter milan 3 vs Seongnam Ilhwa Chunma F.C 0


Wakati huo huoTanzania imepanda chati kwa nafasi nane katika viwango vya ubora wa soka kwa mujibu wa Shirikisho la Soka la Kimataifa, Fifa vilivyotangazwa jana.

Hii imetokana na kutwaa ubingwa wa Cecafa Tusker Challenge Cup ambayo yanatambulika na Fifa kama ni miongoni mwa mechi za kirafiki za kimataifa.Habari kamili gonga hapa  Mwananchi

John Tendwa Ataka Katiba Mpya Kabla Mambo Hayajaharibika


Msajili wa vyama vya siasa,John Tendwa
Mwangwi wa kudai katiba mpya umezidi kusikika kila kona ya nchi baada ya Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa juzi kuvunja ukimya na kusema kuwa iundwe katiba mpya sasa kabla mambo hayajaharibika. Msajili huyo, ambaye ni mwajiriwa wa Serikali, alionyesha ujasiri mkubwa juzi aliposema bila kutafuna maneno kuwa kinyume na katiba iliyopo sasa, katiba mpya inayotakiwa lazima itokane na mapendekezo ya mkutano wa kitaifa wa kikatiba utakaojumuisha watu wa kada mbalimbali.

Kauli hiyo ya mlezi wa vyama vya siasa nchini ni nzito mno, kwa maana ya kutolewa na mtu mwenye mamlaka ya kusimamia shughuli za vyama vilivyoanzishwa kisheria mwaka 1992 kufanya kazi za siasa zenye lengo la kutoa changamoto kwa chama kilicho madarakani. Kauli kama hiyo inapotolewa na kiongozi wa juu serikalini inaifanya serikali yenyewe ione umuhimu wa kutafakari kwa kina madai ya kuwapo katiba mpya ambayo yametolewa na kada mbalimbali nchini mwetu.

Akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania (TDC), Tendwa alisema kuwa katiba ya sasa ya Tanzania pamoja na nchi nyingine katika Afrika Mashariki bado zina misingi ya kikoloni na akaongeza kuwa maendeleo yaliyopo katika nchi hizo pengine yangekuwa makubwa zaidi iwapo nchi hizo zingekuwa na katiba zinatokana na matakwa ya wananchi wenyewe.

Msimamo huo wa Msajili unakuja siku chache baada ya viongozi wa ngazi za juu, wakiwamo mawaziri wakuu wastaafu, majaji, wanasheria, vyama vya siasa na wanaharakati kusema kuwa katiba iliyopo sasa haikidhi mahitaji ya sasa, hivyo lazima iandikwe upya kwa kuzingatia matakwa ya wananchi walio wengi.

Msimamo wa kiongozi huyo pia umekuja muda mfupi baada ya Waziri wa Sheria na Katiba, Celina Kombani kusema kuwa serikali haina fedha za kuandika katiba mpya, hivyo zoezi la kuifanyia marekebisho katiba iliyopo litaendelea kufanyika pale tu unapokuwapo umuhimu wa kufanya hivyo. Alisema wanaodai katiba mpya ni watu wa barabarani ambao alidai hawana uelewa wa kutosha kuhusu masuala ya katiba na sheria.

Ndio maana tunasema kuwa katika mazingira hayo, kauli ya Tendwa ambaye pia ni mwanasheria na mwajiriwa wa serikali hiyohiyo iliyomwajiri Waziri Kombani, ni nzito kiasi cha kuibua maswali mengi kuhusu iwapo Serikali ya Rais Kikwete na chama chake cha CCM vina msimamo wa pamoja juu ya suala hilo, kwani wengi wanajiuliza hivi sasa iwapo kweli msimamo wa waziri huyo kuhusu kuwapo au kutokuwapo umuhimu wa katiba mpya ni wa chama chake na serikali yake au ni wake binafsi.

Utata kuhusu suala hilo umezidishwa na kauli ya Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, John Chiligati ambaye aliliambia gazeti dada la The Citizen juzi kuwa chama hicho kiko tayari kukaa na vyama vya upinzani kuzungumzia suala hilo, lakini akaonya kuwa vyama hivyo vipeleke mapendekezo thabiti badala ya kile alichokiita ‘blabla za kisiasa’ alizodai zinafanywa na vyama hivyo hivi sasa.

Sisi tunadhani kuwa kauli hiyo ya Chiligati inathibitisha kuwapo tatizo moja kubwa ndani ya chama chake. Tatizo hilo ni CCM kudhani kuwa katiba iliyopo hivi sasa ni mali yake na yeyote anayezungumzia kuifuta na kuandika mpya ni adui mkubwa anayekitakia chama hicho maangamizi makubwa. Ni dhana itokanayo na kile Jaji Mark Bomani anachokiita woga usio na msingi wa chama hicho kupoteza madaraka.

Ndio maana tunasema kuwa tunahitaji viongozi katika CCM au Serikali yake kama Msajili John Tendwa asaidie kuwafafanulia na kuwatoa hofu viongozi wa chama hicho kwamba katiba iliyopo ni ya wananchi wote na kwamba kuandika katiba mpya itakayokidhi matakwa ya wakati huu kutaepusha utengano na machafuko katika siku za usoni.
Chanzo:  Mwananchi

Wednesday, December 15, 2010

Sherehe Za Ashura Zageuka Mauaji

Mauaji ya kujitolea Muhanga
Zaidi Ya watu 35 wauawa

Zaidi ya watu 35 wameuawa baada ya mshambuliaji wa kujitoa mhanga kujilipua wakati waumini wa kishia walipokuwa kwenye shughuli zao kwenye mji wa Chabahar kusini mashariki mwa Iran.

Afisa wa Shirika la Hilali nyekundu Mahamoud Mozafar amesema mshambuliaji huyo alijiripua katika eneo la kati ambapo waumini hao walikuwa wakifanya ibada ya kuadhimisha siku ya mwisho ya Ashura.

Kundi la Jundallah limedai kuhusika na shambulio hilo.Kundi hilo katika kipindi cha muongo mmoja uliyopita limekuwa likihusika na mashambulio kadhaa dhidi ya vikosi vya usalama nchini Iran.

Mkuu wa kamati ya mambo ya Nje ya Bunge la Iran Alaeddin Borujerdi amezishutumu idara za kijasusi za Uingereza na Marekani kuhusika na shambulio hilo.

Mjini London Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza Alistair Burt amesema ameshtushwa na shambulio hilo na kwamba inalaani vikali.
Chanzo: Dw

World Club Championship-TP Mazembe Yatinga Fainali

Yaifunga Internacional Ya Brazil 2-0
Timu Ya Kwanza Toka Afrika Kutinga Fainali
Yasubiri Mshindi Baina ya Inter milan na Seongnam Ilhwa(Korea kusini)

Mambo yalijiri kama hivi

ICC yataja watuhumiwa wa ghasia Kenya

Mwendesha mashtaka mkuu wa mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu - International Criminal Court (ICC) imetaja majina ya Wakenya sita anaowatuhumu kuhusika kupanga vurugu zilizotokea baada ya uchaguzi mkuu nchini humo mwaka 2007.

Ghasia baada ya uchaguzi mkuu Kenya
 Ghasia baada ya uchaguzi mkuu Kenya
Naibu Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri wa Fedha Uhuru Kenyatta, ni mmoja ya waliotajwa.

Takriban watu 1,200 waliuawa na zaidi ya wengine 500,000 walizihama nyumba zao kufuatia ghasia hizo.

Siku ya Jumatatu Rais Mwai Kibaki, alitangaza serikali itaendesha uchunguzi wake, hatua ambayo wapinzani wake wameiona ni sawa na jaribio la kuzuia watuhumiwa kupelekwa The Hague.

Ghasia hizo zilizuka baada ya wafuasi wa Bw Kibaki, kutuhumiwa walijaribu kuvuruga uchaguzi.
Uhasama huo ulimalizika baada ya Bw Kibaki na mpinzani wake kisiasa Raila Odinga walipokubaliana kuunda serikali ya mseto na Bw Odinga akawa Waziri Mkuu.

Waziri wa Viwanda Henry Kosgey, naye ametajwa na Bw Ocampo.
Waziri wa Elimu aliyesimamishwa William Ruto, Mkuu wa uendeshaji wa Radio Kass FM, Joshua Arap Sang, katibu wa Baraza la Mawaziri Francis Kirimi Muthaura na na Mkuu wa zamani wa jeshi la polisi Mohammed Hussein Ali, nao majina yao yametajwa na Bw Ocampo.

Polisi nchini Kenya wamewekwa katika hali ya hadhari iwapo baada ya kutangazwa majina hayo kunaweza kuibuka ghasia mpya.


Kila mmoja kati ya hao sita, watatumiwa hati ya kuitwa mahakamani, lakini wakigoma au wakijaribu kuingilia uchunguzi, mathalan kuwatisha mashahidi, Bw Ocampo amesema ataomba kibali cha hati ya kuwakamata.

Swali lililopo ni iwapo waliotuhumiwa hao watajisalimisha au watawekewa kinga na wanasiasa na kukwepa mkono wa sheria.

Katika taarifa yake baada ya tangazo hilo la Bw Ocampo, Rais Mwai Kibaki amesema ana matumaini Mahakama hiyo ya Kimataifa, mchakato wake utatimiza wajibu wake kwa maslahi ya taifa la Kenya.

Rais Kibaki amesema, kama taifa ni lazima walenge mahitaji ya taifa ya maridhiano na kusameheana.

Amewahakikishia Wakenya kwamba serikali imeimarisha ulinzi nchi nzima.
Chanzo: BBC

Tuesday, December 14, 2010

Sepp Blatter awaasa mashoga Qatar 2022

Rais wa Fifa Sepp Blatter, ametania kwamba mashabiki wa soka ambao ni mashoga watakaokwenda kwenye Kombe la Dunia mwaka 2022 nchini Qatar, hawana budi "kujizuia kufanya mambo yao ya ngono."

Sepp Blatter
Rais wa Fifa,Sepp Blatter

Makundi ya kutetea haki za mashoga, wameshutumu uamuzi wa kupeleka mashindano hayo ya Kombe la Dunia katika nchi ambayo ushoga ni marufuku.

Lakini Blatter, akatania kwa kusema: "Ningependa kusema, mashabiki wa soka walio mashoga, wajizuie na mambo yao watakapokuwa Qatar."


Na katika taarifa ambayo ni kali zaidi, Blatter amesema: "Nina hakika wakati wa mashindano ya Kombe la Dunia yatakapofanyika Qatar, hakutakuwa na matatizo."

Hata hivyo mchezaji nyota wa zamani wa NBA John Amaechi, ambaye alijitangaza rasmi kuwa shoga mwaka 2007, ameshutumu vikali kauli hiyo ya Blatter.

Qatar ambayo ni nchi ya Kiislamu, ilipata nafasi ya kuandaa Kombe la Dunia mwaka 2022, wakizishinda Australia, Japan, Korea Kusini n Marekani, wakati wajumbe wa kamati ya utendaji ya Fifa walipopiga kura tarehe 2 mwezi huu wa Desemba.

Tangu wakati huo Fifa imekuwa ikishutumiwa kutokana na uamuzi wao wa kupeleka mashindano hayo kwa mara ya kwanza eneo la Mashariki ya Kati.

Wasiwasi umeibuka kuhusu kuandaa mashindano hayo wakati wa miezi ya kiangazi katika nchi ambayo joto linakuwa la kiwango cha juu cha nyuzi joto 40 vipimo vya centrigrade hadi nyuzijoto 50, huku sheria ikikataza unywaji wa pombe hadharani.

Makundi ya kutetea haki za mashoga na mashoga wenyewe, pia wameonesha wasiwasi wao kuhusiana na kuruhusiwa watu wanaoendekeza vitendo hiyo wanaopenda soka, kwenda Qatar na wamelaani uamuzi wa Fifa na wametangaza kususia shughuli zote zinazohusiana na Kombe la Dunia mwaka 2022.
Chanzo : BBC



Rais Jakaya Kikwete Ahidi Kuinua Kiwango Cha Michezo Tanzania

Apokea kombe la ubingwa wa tusker challenge cup 2010
Afanya tafrija ya chakula cha mchana na wachezaji na viongozi
wa tff
Atunukiwa tuzo ya TASWA kwa mchango wake katika michezo


Hivi ndivyo Kilimanjaro Stars walivyowapa raha wa Tanzania

Maalim Seif: Pelekeni madai yenu Mahakama ya Afrika


Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar
Seif Sharif Hamadi

Watanzania, jumuia za kiraia na mashirika mbalimbali yameaswa kupeleka mashauri yao katika Mahakama ya Afrika inayoshughulika na haki za binadamu iliyoko jijini Arusha, pale wanapohisi kuwa haki zao za kibinadamu zimekiukwa.


Wito huo ulitolewa jana jijini Dar es Salaam na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Seif Sharif Hamad, alipokuwa akifungua semina ya uhamasishaji wa jumuia za haki za binadamu nchini, iliyoandaliwa na Mahakama ya Afrika kuhusu haki za binadamu kwa kushirikiana na serikali na Jumuia ya wanasheria nchini (TLS).
Alisema mahakama hiyo inapewa mamlaka na protokali yake, kuipa nguvu Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu ili kulinda haki za watu na za makundi Afrika, kwa kutoa hukumu za kukazia na mamlaka ya kutoa ushauri pale inapoombwa na nchi mwanachama,AU yenyewe,chombo chake au chombo inachokitambua.

“Ndiyo maana nasema raia katika ujumla wao,jumuia za watu na ,makundi mbalimbali yawasilishe mashauri yao katika mahakama hii pale wanapohisi kutotendewa haki na mamlaka yeyote ile”alisema.

Hamad alisema kuwa pamoja na mahakama hiyo kuwa tayari kupokea mashauri toka mwaka 2008,inasikitisha kuona kwamba mpaka sasa imeshapokea shauri moja tu,kitu ambacho hakikubaliki.

Naye Rais wa Mahakama hiyo, Jaji Gerard Niyungeko, aliviasa vyombo vya habari kujikita katika utoaji wa habari zilizo sahihi,kama zilivyo zenye kuhabarisha na zilizotolewa kwa wakati kuhusu matukio na maendeleo ya ulimwengu,kwa kuwa bila ya kufanya hivyo jamii itabaki bila ya kuhabarishwa au ikapata habari zilizopotoshwa.
Chanzo: Nipashe

Monday, December 13, 2010

EPL: Men Against Boys

Man United 1 Vs Arsenal 0


Chelsea held to a Draw by Spurs


Liverpool no comment


Spain Premera division
Barca Threats


Madrid business done

Ahmadinejad amfuta kazi Mottaki

Rais wa Iran Mahmoud Ahmadinejad amemuachisha kazi Waziri wa Mambo ya Nje Manouchehr Mottaki Jumatatu, wakati waziri huyo akiwa kwenye ziara huko Senegal.

Rais wa Iran Mahmoud Ahmadinejad
Rais wa Iran Mahmoud Ahmadinejad

Rais wa Iran Mahmoud Ahmadinejad amemuachisha kazi Waziri wa Mambo ya Nje Manouchehr Mottaki Jumatatu, wakati waziri huyo akiwa kwenye ziara huko Senegal.

Bwana Ahmadinejad alimuachisha kazi Mottaki Jumatatu na kumteuwa mkuu wa nyuklia nchini Iran, Ali Akbar Salehi kama waziri mpya wa mambo ya nje kwa sasa. Shirika rasmi la habari la Iran Mehr linaripoti kwamba Bwana Ahmadinejad alituma barua kwa Mottaki akimshukuru kwa kazi yake.

Salehi anajulikana kama mshirika wa karibu wa rais. Zaidi ya mwaka mmoja uliopita vyombo vya habari vya Iran viliripoti mifarakano kati ya Mottaki na wabunge wa Iran. Ripoti hizo zilisema wabunge wa Iran walisema kwamba Mottaki hakuwa mahiri au mwakilishi shupavu kwa Iran kwenye jukwaa la kimataifa.

Walimshinikiza Mottaki kujiuzulu kama vikwazo zaidi vya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa vingewekwa katika kujibu program ya nyuklia ya nchini humo, na mzunguko wa nne wa vikwazo hivyo viliwekwa mwezi Juni. Duru za kimataifa zinaonesha vikwazo hivyo vinaharibu mno uchumi wa Iran.

Chanzo: Voa

Zitto,Shibuda Waundiwa Kamati


Mbunge wa Kigoma kaskazini, Zitto Kabwe, akijuliwa hali na mbunge
wa Maswa Magharibi, John Shibuda, wakati alipolazwa katika hospitali
ya Agha Khan jijini Dar es salaam

WAKATI Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ikitarajiwa kutoa msimamo wa chama hicho juu ya masuala mbalimbali ikiwemo hali ya kisiasa nchini na ndani ya chama hicho, imeelezwa kuwa Mbunge wa

Kigoma Kaskazini Bw. Zitto Kabwe ametakiwa kujipima mwenyewe kisha ajiuzulu, baada ya kupigiwa kura ya kutokuwa na imani na wabunge wa chama hicho.

Imeelezwa kuwa kura za kutokuwa na imani naye, zilizopigwa wiki iliyopita na wabunge wa CHADEMA katika kikao cha kamati yao, kilichofanyika Mjini Bagamoyo, hakizumwondoa moja kwa moja katika cheo chake cha naibu mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni, bali ilikuwa ni ishara ya kuwa watu anaowaongoza bungeni hawana imani naye tena hivyo kumtaka afikirie mwenyewe kisha achukue uamuzi wa kujiuzulu kabla wabunge hao hawajachukua hatua za kinidhamu juu yake.

Habari kutoka ndani ya chama hicho zimebainisha pia kuwa Kamati Kuu iliyoketi mwisho wa juma katika kikao maalumu, imeunda kamati kwa ajili ya kumshauri Bw. Zitto, baada ya wajumbe kuona kuwa kuna umuhimu wa kumsaidia ushauri nasaha kutokana na mwenendo wake ndani ya chama hicho.Vyanzo mbalimbali vimesema kamati hiyo inajumuisha Profesa Mwesiga Baregu, Dkt. Mkumbo Kitila, Shida Salum na mwanachama mwingine wa chama hicho.

Mbali ya kubainika kwa suala hilo, pia habari kutoka vyanzo mbalimbali vya kuaminika zimeeleza kuwa Kamati Kuu ya CHADEMA, imeunda kamati nyingine kumchunguza Mbunge wa Maswa Magharibi, Bw. John Shibuda, kutokana na tuhuma zilizowasilishwa na kamati ya wabunge, iliyokutana wiki
iliyopita Mjini Bagamoyo.

"Nafikiri hilo la Zitto waandishi wamwelipotosha kwa kiasi kikubwa, mimi ninavyojua walichofanya wabunge wale ni kupiga kura ya kutokuwa na imani naye (Zitto), kisha mwenyewe apime uzito wa uamuzi huo kuwa watu anaowaongoza hawana imani naye, kisha mwenyewe ajiuzulu, kabla wabunge wenyewe hawajachukua hatua za kinidhamu juu yake.

"Hata hivyo uamuzi huo wa kuchukua hatua za kinidhamu ikiwemo hata kumwondoa katika cheo hicho, imo katika mamlaka ya Kamati ya Wabunge wa CHADEMA, yaani Party Caucus, wanayo mamlaka hayo kabisa wakiona kuna haja ya kufanya hivyo, baada ya yeye kushindwa kuchukua hatua yoyote hasa kujiuzulu maana ni kiongozi wao wenyewe, hivyo haihusiani na chombo kingine ndani ya chama."Kumbuka pia kuwa naye ataitwa kama alivyoitwa wengine kuhojiwa juu ya kutotekeleza maamuzi halali ya kikao ya kuingia ukumbini siku ya ufunguzi wa bunge kama

ilivyokuwa imeamuriwa...lakini cheo hajavuliwa, mwenyewe apime kisha ajiuzulu," kilisema moja ya chanzo chetu cha habari.

Chanzo chetu kikiwa na tahadhari ya kutotaka kufafanua masuala mengi, pia kilisema kuwa Kamati Kuu ya CHADEMA imeona kuna umuhimu kukaa na Bw. Zitto kisha apatiwe ushauri juu ya mwenendo wake wa kisiasa akiwa kama mmoja wa viongozi waandamizi wa chama hicho, ambapo mbali ya kuwa ni naibu mkuu wa kambi rasmi ya upinzani bungeni pia ni naibu katibu mkuu wa chama hicho kwa upande wa Tanzania Bara.

Nafasi hiyo ya naibu katibu mkuu bara, inamfanya kuwa mmoja wa watu wawili wanaomsaidia Katibu Mkuu Dkt. Willibrod Slaa, mwingine akiwa ni Hamad Mussa Yusuf, kwa Zanzibar, lakini nafasi ya naibu mkuu wa kambi ya upinzani bungeni, inamfanya kuwa msaidizi wa Mkuu wa Kambi, Bw. Freeman Mbowe.

Kwa upande wa suala la Bw. Shibuda, vyanzo vyetu vilieleza kuwa mbunge huyo ambaye alihamia CHADEMA kutoka Chama Cha Mapinduzi, siku chache kabla ya kampeni za uchaguzi kuanza, baada ya kubwagwa katika kura za maoni, atachunguzwa kwa tuhuma kadhaa, ikiwa ni pamoja na kutotii maagizo na maamuzi kikao halali cha chama, kulaumu na kulalamikia nje ya chama maagizo na maamuzi hayo, kujaribu au kutaka kuleta mgawanyiko ndani ya chama.

"Bw. Shibuda alisema hana kosa wala hana haja ya kuomba msamaha, chanzo hicho kilisema wabunge walikuwa wazi kabisa kwake, wakimwambia asifikiri wanamwogopa, asifikiri kuwa wao hawakushinda uchaguzi...maana amekuwa akijigamba kuwa yeye ametumwa na watu wa Maswa.Juhudi za gazeti hili kuwapata viongozi wa chama hicho kuzungumzia taarifa hizo hazikuzaa matunda jana.

Chanzo: Majira
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...