Mtazamohalisi

Sunday, November 14, 2010

Kinyang'anyiro Cha Unaibu Spika ni Ndugai - CCM Na Mustapha Akonay -Chadema


Job Ndugai-CCM
MBUNGE wa Kongwa, Job Ndugai amechaguliwa na CCM kugombea Unaibu Spika wa Bunge kwa kupata ushindi wa kura  197 za ndiyo  kati ya 199 zilizopigwa, huku moja ikiharibikana nyingine ikimkataa. Alipigiwa kura ya ndiyo au hapana kutokana na wagombea wawilikujitoa, hivyo kubaki pekee.Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Itikadi na Uenezi, John Chiligati, alisema leo kuwa, mkutano wa Kamati ya Wabunge wa CCM imempa ushindi wa kishindo Ndugai, aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge lililopita.

Mustapha Akonay -Chadema
 Kwa upande wake, CHADEMA imemteua Mbunge wake wa jimbo la  Mbulu, Mustapha Akonay, kuwania unaibu spika.
Uchaguzi wa Naibu Spika wa Bunge utafanyika Jumanne ijayo, ambapo kesho saa 10 jioni ni siku ya mwisho ya kuwasilisha majina ya wagombea wa nafasi hiyo katika Ofisi ya Bunge mjini Dodoma.  

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...