Mtazamohalisi

Friday, November 19, 2010

Papa Benedict XVI Azitaka Nchi Tajiri Kutokandamiza Nchi Maskini


Kiongozi wa Kiroho Wa Kanisa Katoliki
Papa Benedict XVI

Papa Benedict XVI amesema ana wasiwasi wa mgogoro wa kiuchumi kwa mataifa tajiri kufanya ushirikiano utakao athiri mataifa maskini.Alikuwa akielezea ni makosa gani yaliyotikisa uchumi wa dunia na jinsi ya mataifa yatakavyo ondokana na mgogoro huo, alisema hayo mbele ya umati wa watu katika Viwanja vya Mtakatifu Petro siku ya Jumapili.Benedict alitoa kauli hiyo baada ya kilele  cha mkutano wa G20 uliokuwa Seoul, ambao ulikuwa umetingwa na tofauti  juu ya fedha na biashara.Anasema anafadhaishwa kwa pengo kubwa kati ya nchi  matajiri na maskini, na kwamba mataifa yenye viwanda vingi huhamasisha utumiaji wa mfumo wa maisha wenye kuathiri mazingira na watu maskini..Benedict ameshauri uwiano mpya katika sekta ya kilimo, sekta ya viwanda na sekta ya huduma  ili kufikia maendeleo endelevu hivyo hakutakuwa na ukosefu wa ajira au chakula
 Chanzo:  http://www.wtol.com/Global/story.asp?S=13503953

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...