Mtazamohalisi

Saturday, November 13, 2010

Mjue Lucas Radebe


Lucas Radebe





 Na Rashid Seif:
katika lugha ya kiswahili unasoma kama lucas Ghadebe,
lucas radebe amekulia katika familia ya watoto 11 katika maisha magumu ya moja ya sehemu zilizokuwa na machafuko makubwa ya kisiasa za ubaguzi wa rangi huko soweto(south western townships).hii ilimpelekea kuja kuwa mmoja katika wachezaji walioheshimika katika ligi kuu ya uingereza na kuwa muafrika kusini wa kwanza kucheza mechi nyingi kuliko wote kwenye timu ya taifa bafana bafana akiwa ameichezea mara 70.
Radebe alinyanyukia kuwa mchezaji muhimu na maarufu mara baada ya kuchaguliwa kuwa nahodha wa timu ya leeds united mwaka 1998.akichukuwa jukumu la kuiongoza timu yenye vijana na wachezaji wengine wenye uzoefu wa ligi kuu.
chini ya uongozi wake radebe leeds united kutoka yorkshire ilinyanyukia kuwa moja ya timu kali katika ligi ya uingereza .Radebe mchango wake haukuwa tu katika uongozi wake bali pia usakataji wake safi wa kandanda usio na utata dhidi ya washambuliaji wa timu pinzani ambao ulimfanya aheshimike duniani na wanasoka wenzake.
HAPO MWANZONI
alikulia katika ukanda wa 4 wa mji wa DIEPKLOOF katika kitongoji cha soweto nje ya jiji la johannesburg.Radebe akishuhudia machafuko ya kisiasa akiwa na umri wa miaka 15 wazazi wake walimpeleka akaishi katika mji wa BOPHUTHASWANA ambao ni mmoja kati ya miji iliyotengwa kwa ajili ya watu weusi katika kipindi cha siasa za ubaguzi wa rangi.alianza kucheza mpira kama sehemu ya kujishughulisha akianza kama mlinda mlango kabla hajabadili kuchezea nafasi ya kiungo na kujiunga na timu ya ICL iliyokuwa ikichezea ligi iliyojulikana kama ligi ya boputhaswana .
mwaka 1989 kipaji chake kilgundulika na timu na moja ya timu kongwe barani afrika ijulikanayo kama kaizer chiefs ambayo alitia mkataba nayo.wakimtaka achezee kama mlinzi wa kati badala ya kiungo....inaendelea

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...