Mtazamohalisi

Saturday, December 25, 2010

Nazi Zao Yatima Hana Mzazi Hana Mlezi


Zao la Mnazi kwa biashara tukiamua tunaweza.

Nikianza kwa kunukuu maneno ya Rais Kikwete kuwa zao la minazi limepatwa na " Ugojwa usiotibika kwa sasa ",nakuwataka wakulima wa zao la mnazi kulima kokoa kama zao mbadala .Wazo kama hili si geni ,kwani hapo nyuma wakulima huko Mwanza walitakiwa kubadilisha zao la pamba kwa kahawa .

Inaniwia vigumu kukubaliana na Rais hasa pale alipowahakikishia wakulima wa zao la  minazi kuwa atawapa wataalamu kushirikiana nao ili kuweza kufanikisha zoezi hili la kubadilisha Mnazi kwa Kokoa, na ndiyo hapo sera ya kilimo kwanza ninapohisi kushindwa.

Lengo kuu la kilimo kwanza ni kumkomboa mkulima mdogo toka kilimo cha kuchumia tumbo hadi kilimo chenye kunyanyua kipato cha mkulima na serikali . Na ndipo hapo ninakuwa na shaka na mkulima wa minazi kumuona kuwa ni yatima hana mzazi wala mlezi.

Minazi mingi iliyopo imetokana na mashamba ya kurithi ambayo huenda tumerithi toka kwa wazee wetu ama mara baada ya harakati za ukombozi wananchi kujimilikisha kama matunda ya uhuru.

Kutokana na umri mrefu na kutoboreshwa mashamba kutokana na uwezo duni au tamaa za wenye mashamba kwa kuangalia mavuno bila kutahadhari uboreshwaji wa zao hilo kwa kukuza miche mipya na uwekaji wa mbolea , zao hili limejikuta siku hadi siku likiwa linatokomea.

Miaka ya 80 hadi 90 zao hili lilikuwa likishughulikiwa na Mradi wa Kitaifa wa Kuendeleza Zao la Mnazi , vipi iwezekane kutoa wataalamu kuwezesha kubadilishwa zao moja kwenda lengine na kusiwezekane kutoa wataalamu wa kuendeleza na kuboresha zao lililopo.

Ushauri wangu kwa wizara husika hasa ya kilimo na mazingira,jaribuni kufanya utafiti kujua jinsi gani ya kuokoa utowekaji wa zao la mnazi na pia ili serikali ijiridhishe haina budi kuchukua uzoefu wa nchi nyengine mfano wa  Sri lanka , kwani kisiwa hichi kinafaidika sana na zao la Mnazi.

Ukitazama athari iliyopo ni kuwa,zao la mnazi likiboreshwa litanyanyua kiwango cha maisha kwani nazi hutumika sana kwa mapishi,kutoa mafuta na ni kiburudisho cha koo na uboreshwaji wake utanyanyua uchumi kwa nchi na wananchi .

Zao la Mnazi ni alama kuu katika ukanda wa pwani ya Afrika Mashariki na ukiangalia kwa makini  kutokomea kwake ni sawa na kuondoa meno halisi na kuyabadili kwa meno bandia.Kutokana na umri mrefu na kutoboreshwa mashamba kutokana na uwezo duni au tamaa za wenye mashamba kwa kuangalia mavuno bila kutahadhari uboreshwaji wa zao hilo kwa kukuza miche mipya na uwekaji wa mbolea , zao hili limejikuta siku hadi siku likiwa linatokomea.

Miaka ya 80 hadi 90 zao hili lilikuwa likishughulikiwa na Mradi wa Kitaifa wa Kuendeleza Zao la Mnazi , vipi iwezekane kutoa wataalamu kuwezesha kubadilishwa zao moja kwenda lengine na kusiwezekane kutoa wataalamu wa kuendeleza na kuboresha zao lililopo.

Ushauri wangu kwa wizara husika hasa ya kilimo na mazingira,jaribuni kufanya utafiti kujua jinsi gani ya kuokoa utowekaji wa zao la mnazi na pia ili serikali ijiridhishe haina budi kuchukua uzoefu wa nchi nyengine mfano wa  Sri lanka, kwani kisiwa hichi kinafaidika sana na zao la Mnazi.

Ukitazama athari iliyopo ni kuwa,zao la mnazi likiboreshwa litanyanyua kiwango cha maisha kwani nazi hutumika sana kwa mapishi,kutoa mafuta na ni kiburudisho cha koo na uboreshwaji wake utanyanyua uchumi kwa nchi na wananchi .

Zao la Mnazi ni alama kuu katika ukanda wa pwani ya Afrika Mashariki na ukiangalia kwa makini kutokomea kwake ni sawa na kuondoa meno halisi na kuyabadili kwa meno ya bandia.

Majembe yaondolewa barabarani

Serikali imeiagiza Mamlaka ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra), kuvunja mkataba na Kampuni ya Udalali ya Majembe Auction Mart ya jijini Dar es Salaam Desemba 31, mwaka huu.

Majembe ilipewa na Sumatra mkataba wa uwakala wa kusimamia shughuli za daladala jijini Dar es Salaam kwa miaka miwili kuanzia mapema mwaka huu.

Akizungumza na Waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu, alisema kuvunjwa kwa mkataba huo kutasaidia kupunguza kero zinazosababishwa na Majembe.

Nundu alisema wameamua kuuvunja mkataba huo kutokana na Majembe kuendelea kukiuka sheria na kanuni walizopewa wakati wa kabla ya kuanza kufanya kazi za uwakala.

Kwa Mujibu wa Waziri huyo, Majembe ilianza kufanya kazi ambazo haziwahusu na ambazo hawana ujuzi nazo, ikiwa ni pamoja na zile za usalama barabarani.

Alisema zipo baadhi ya kazi zinazotakiwa kufanya na askari wa kikosi cha usalama barabarani, lakini kinyume chake zimekuwa zikifanywa na Majembe, jambo ambalo ni kuingilia kazi zisizowahusu.

" Hii siyo sawa, hatutakiwi kuweka watu watufanyie kazi wasizo na uzoefu nazo…lazima tuweke mfumo madhubuti utakaotusaidia kutatua matatizo, si kuweka weka tu, watu wasio na utaalamu," alisisitiza.

Alisema baadhi ya kazi ambazo ni kinyume na sheria zinazofanywa na Majembe ni pamoja na kukagua magurudumu ya magari, leseni, bima, taa za magari na vioo.

Waziri huyo alisema ikiwa Sumatra watahitaji kuendelea kufanya kazi na Majembe, wanatakiwa wawape mafunzo maofisa wake kwanza kuhusu namna kufuata sheria za usalama barabarani.

Sumatra iliipa Kampuni hiyo mkataba huo kwa lengo la kuboresha usafiri wa umma na kuondoa kero kwa wakazi wa Dar es Salaam, kusimamia, kufuatia na kufanya ukaguzi wa utekelezaji wa masharti ya leseni.

Kabla Majembe haijapewa mkataba huo, wakazi wa Dar es Salaam walikuwa wakilalamikia vitendo vya ukiukwaji wa sheria vilivyokuwa vikifanywa na daladala kama kukatisha safari, kushusha na kupakia abiria katika maeneo yasiyo na vituo, makondakta na madereva kutovaa sare, kutoza nauli za juu, matusi na kukataa kuwabeba wanafunzi.

Moja ya sababu ambazo hivi karibuni zilikuwa zikilalamikiwa na wamiliki wa mabasi ya mikoani na daladala dhidi ya Sumatra ni kuiruhusu Majembe kuweka wafanyakazi kufanya kazi za barabarani.

Mapema mwezi huu, wamiliki wa mabasi walitishia kugoma pamoja na mambo mengine, wakitaka kampuni hiyo isijihusishe na kazi za barabarani bila kuwepo na askari wa kikosi cha usalama barabarani..

Wakati huo huo; Serikali imetangaza kuwaondoa mara moja wapiga debe katika vituo vyote vya mabasi nchini.

Nundu alizitaka mamlaka zinazohusika kuandaa utaratibu wa kuwatambua wafanyakazi na mawakala wa makampuni ya mabasi kwa kuwapatia vitambulisho maalum.

Alisema utaratibu wa kuhakikisha wapiga debe wanaondoka katika vituo vya mabasi unatakiwa kufanyika sasa na kwamba ifikapo Januari 15, mwakani, utaratibu wa kutoa vitamburisho kwa wafanyakazi na mawakala unatakiwa uwe umekamilika.

" Ninaagiza kwamba kuanzia sasa ninataka kuona wapiga debe wote wameondolewa katika vituo vyote vya mabasi, na zoezi hili linatakiwa kufanyika haraka iwezekanavyo,” alisema.

Aliongeza kuwa wapigadebe wamekuwa kero kubwa kwa wasafiri hususani wa mikoani kusumbuliwa wanapokwenda kukata tiketi na wakati mwingine kuwaibia.

Kwa upande mwingine, Nundu alisema kuna umuhimu wa kuwepo kwa matuta barabarani ili kupunguza ajali zinazotokana na mwendo kasi.

Alisema Wizara yake kwa kushirikiana na ya Ujenzi, itachukua hatua mwafaka ili kuhakikisha ujenzi wa matuta barabarani unafuata viwango.

Alisema ukosefu wa matuta barabarani pia umekuwa ukisababisha uharibifu wa mabasi na hivyo kuongeza gharama za uendeshaji.
Chanzo: Nipashe

Ujumbe wa X-Mass



Zitto Kabwe:Aeleza Kulikoni Yake


Mbunge wa Kigoma kaskazini,
Mheshimiwa Zitto Kabwe

NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Zitto Kabwe amesema kuwa hajapewa sumu kama ilivyokuwa imedaiwa huku akisisitiza kuwa hakuna binadamu anayeweza kufanya hivyo.Pia mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini, amesema hana nia wala mpango wa kukihama chama hicho.

Bw. Kabwe aliyasema hayo juzi wakati akiwahutubia mamia ya wananchi Mkoa wa Kigoma katika mkutano wake wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya kawawa ndani ya Manispaa ya Kigoma ujiji.

Alisema kuwa migogoro inayoendelea ndani ya chama chake isiwafanye wananchi wa Kigoma kuwa na hofu yeyote na hata yale yanayoandikwa na vyombo vya habari pia yasiwanyime rah,a waendelee kukisimamia chama chao.

"Wananchi wenzangu msiwe na wasiwasi, mimi ni mzima kabisa, yameandikwa mengi katika vyombo vya habari, mara nimepewa sumu, nataka niwahakikishie hizo habari si za kweli, mimi sijapewa sumu na hakuna binadamu anayeweza kunipa sumu, tuendelee kufanya kazi na kukijenga cha chetu," alisema Kabwe.

Siku za karubuni kumekuwapo na mgogoro ndani ya CHADEMA kutokana na mbunge huyo kutofautiana na wabunge wenzake kuhusu msimamowa kususia hotuba ya Rais jakaya Kikwete bungeni, hali iliyosababisha chama hicho kuundama kamati ya kuzungumza naye kumpa ushauri.hatua hiyo ilichukuliwa siku chache baada ya wabunge wenzake kupiga kura ya kutokuwa na imani naye, kama Naibu Kiongozi wa Kambi ya upinzani bungeni.

Wakati wabunge hao wanachukua uamuzi huo, Bw. Kabwe aliugua ghafla na kulazwa katika Hospitali ya Aga Khan akisumbuliwa na tumbo, na baadhi ya vyombo vya habari vililiripoti kuwa amelishwa sumu, ingawa madaktari walisema ni tumbo lake lilikuwa tu limechafuka.

Katika hatua nyingine Zitto aliitaka Wizara ya Tawala za Mikoa na Serekali za Mitaa (TAMISEMI) kuitisha uchaguzi wa meya wa Kigoma/Ujiji haraka ndani ya wiki mmoja uliokuwa umesimamishwa wiki iliyopita kutokana na mgogoro wa mgawanyo wa madiwani wa viti maalumu.

"Halmashauri zingine tayari zimeshafanya uchaguzi na wamepata meya, na kazi za kuleta maendeleo wameshaanza, sasa wao wanapozidi kutucheleshea sisi kufanya uchaguzi, wajue na kazi ya kuleta maendeleo katika manispaa yetu inazidi kuchelewa," alisema Bw. Kabwe.

Mbunge huyo amewataka viongozi wa vyama mbalimbali nchini kutumia fursa walizozipata katika kuleta maendeleo ya jamii na sio kuendekeza uadui na serikali kuu.
Chanzo: Majira

Friday, December 24, 2010

Ruzuku: CCM milioni 800/-, Chadema 200/-, CUF 117/-


Msajili wa Vyama vya Siasa,John Tendwa
Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, ametangaza viwango vya mgawo wa ruzuku kwa vyama vilivyotimiza sifa, baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, huku kiwango cha mgawo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ilichokuwa ikipata kila mwezi, kikiwa kimeshuka.


Licha ya CCM kuvipita vyama vingine katika viwango vya mgawo uliotangazwa jana na Tendwa, kiwango cha mgawo wake wa ruzuku, kimeshuka kutoka Shilingi bilioni moja ilizokuwa ikipata kila mwezi katika kipindi cha miaka mitano iliyopita kufikia Sh. milioni 800 inazopata hivi sasa.

Kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi, ruzuku hiyo hutolewa kwa chama kilichofikisha kuanzia asilimia tano ya kura za urais na kwa uwiano wa wabunge na madiwani, ambao chama ‘kilivuna’ katika uchaguzi huo.

Mbali na CCM, vyama vingine, ambavyo vinapata ruzuku, baadhi vikilingana na vingine vikitofautiana sifa ya kupata ruzuku hiyo, ni Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi, UDP na TLP. Viwango vya mgawo wa ruzuku hiyo, vilitangazwa na Tendwa alipozungumza na NIPASHE katika mahojiano maalum ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana.

Alisema ruzuku hiyo ilianza kutolewa na ofisi yake kwa vyama hivyo, kuanzia Novemba, baada ya Uchaguzi Mkuu uliofanyika nchini Oktoba 31, mwaka huu na ule uliofanyika baadaye katika baadhi ya majimbo kukamilisha uchaguzi huo.

“CCM imeshuka kwa ruzuku. Huko nyuma ilikuwa inapata Shilingi bilioni moja, lakini sasa inapata Sh. milioni 818,” alisema Tendwa.

Hata hivyo, alisema ruzuku kwa uwiano wa madiwani, haijaanza kutolewa kwa vile bado hawajapata takwimu za madiwani, ambao kila chama kilipata, katika uchaguzi huo. “Tunasubiri tuweze kuwa na data za madiwani. Hatuwezi kutoa ruzuku za madiwani bila kupata data. Kwa mfano CCM kuna madiwani wamejiuzulu. Kila mgawo (wa ubunge na madiwani) una fungu lake,” alisema Tendwa. Alisema CCM inapata kiwango hicho, kutokana na kupata asilimia 60.40 ya kura za urais katika uchaguzi huo, ambazo ni sawa na Sh. milioni 354 na asilimia 77 ya wabunge (sawa na Sh. milioni 460) kwa mwezi.

Pia alisema licha ya Chama cha Wananchi (CUF) kupata kura katika majimbo mengi ya uchaguzi, kimepata kiwango kidogo cha mgawo wa ruzuku kulinganisha na Chadema. Alisema hali hiyo inatokana na baadhi ya majimbo kiliyovuna wabunge, kama vile ya kisiwani Pemba kuwa na wapigakura wachache waliokiunga mkono katika uchaguzi huo.

“CUF ilipeleka nguvu kubwa Pemba, lakini huwezi kulinganisha na idadi ya wapigakura kama wa Dar es Salaam,” alisema Tendwa.

Kutokana na hali hiyo, alisema CUF sasa inapata Sh. milioni 117.4, kutokana na kupata asilimia 9.80 ya kura za urais (sawa na Sh. milioni 57.9) na asilimia 10 ya wabunge (sawa na Sh. milioni 56). Alisema katika mgawo huo, Chadema inapata Sh. milioni 203.6, kutokana na kupata asilimia 24 ya kura za urais (sawa na Sh. milioni 146) na asilimia 9.62 ya wabunge (sawa na Sh. milioni milioni 56).

Tendwa alisema vyama vya NCCR-Mageuzi, UDP na TLP havipati ruzuku ya urais kwa vile vilipata chini ya asilimia tano ya kura za urais.

Hata hivyo, alisema NCCR-Mageuzi inapata ruzuku ya Sh. milioni 10, kutokana na kupata asilimia 1.08 ya wabunge wakati UDP na TLP alisema vinapata ruzuku ya Sh. milioni 2.4 kutokana na kupata asilimia 0.42 ya kura za ubunge kila kimoja.

Alisema iwapo viwango vya mgawo wa ruzuku ya madiwani itaongezeka kwa chama husika, viwango hivyo navyo pia vitaongezeka.

Kuhusu fomu za gharama za uchaguzi, ambazo wagombea wanatakiwa kujaza, alisema tarehe ya mwisho, ambayo zinatakiwa ziwe zimerejeshwa ofisini kwake, ni Januari 30, mwakani na kwamba, yeyote atakayekiuka ataadhibiwa kwa mujibu wa sheria. “Wanatakiwa waeleze katika hizo fomu walitumia nini, kiasi gani na kutoka wapi. Wathibitishe kwa risiti,” alisema Tendwa.

Akijibu swali kama kuna mgombea yeyote, ambaye hakujaza fomu, alisema hakuna, isipokuwa aliyekuwa mgombea ubunge kupitia TLP Jimbo la Mtama, mkoani Lindi, Ndaka Wolfugang ndiye aliyechelewa kujaza fomu hiyo.

Kutokana na kasoro hiyo, alisema ofisi yake (Msajili) ilimwekea pingamizi Wolfugang, lakini akarudishwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuwania nafasi hiyo kwa maelezo kwamba, kuchelewa kwake kujaza fomu hiyo, kulitokana na kuwekewa pingamizi na aliyekuwa mgombea kupitia CCM, Bernard Membe, ambalo baadaye lilitupwa.
Chanzo: Nipashe

Thursday, December 23, 2010

Christmas Shoes-Nawatakia Maandalizi Mema Ya Krismasi

Nasikitika tukielekea kwenye sherehe ya krismasi wapo watu mikono yao imejaa damu,na kuwa ni wao ndiyo wenye dhamana na haki juu ya maisha ya viumbe wengine.


Hebu Tusahau machungu hayo,kwa kuonyesha kujali kwa umpendae

Umuhimu wa Vyeti Vya Kuzaliwa

Mara nyingi,umuhimu wa vyeti vya kuzaliwa hauji mpaka kuwe na jambo la kisheria linalokukabili. Kutokana na umuhimu wake ni vyema wazazi na vijana mliofikia umri wa kujitegemea kuanza kulifikiria, kwani athari yake unaweza kupoteza haki zako za msingi kama raia na hata kutiliwa shaka uraia wako.

Naandika haya kwa ushahidi mkubwa wa mambo yalivyojitokeza nyuma hasa ukiwa unakumbuka kunyang'anywa uraia wa Jenerali Twaha Ulimwengu na Marehemu Ali Nabwa.

Kuhifadhi cheti cha kuzaliwa ni muhimu kwani ushahidi wake unatambulika kisheria,kumbuka wakati wa mchakato wa kutafuta wagombea wa ubunge wa CCM kulijitokeza mgogoro baada ya Mgombea toka Nzega kukataliwa na chama chake kwa madai ya kutokuwa raia.

 Hussein Bashe ilimlazimu si tu kumuhatarisha uanachama wake katika CCM bali kubwa kuliko yote ni haki nzima ya uraia kama Mtanzania, kwa kuwa alithibitisha uraia wake wa kuzaliwa kwa kigezo hicho Idara ya Uhamiaji ilijiridhisha kuwa ni raia halali.

Leo hii,licha ya uthibitisho wa kuzaliwa ,masomo na nyadhifa mbali mbali alizopitia Marekani, Rais Barack Obama wapo watu wanaodai kutaka uthibitisho wake wa kuzaliwa huko Honolulu,Hawaii.

Picha inayonijia ni kuwa kuhifadhi vyeti vya kuzaliwa ni muhimu kwa ajili kupata haki zako za msingi za kisheria kama raia.

Ijapokuwa Obama na familia yake wapo Hawaii ambako ina aminika ndiko alikozaliwa  katika mapumziko ya Krismasi,lakini swali la uhalali wa cheti cha kuzaliwa kwake huko Honolulu ,Hawaii bado ni tete.


Benitez apigwa chini Inter

Inter Milan ya Italia imethibitisha kuwa imemfukuza kazi meneja Rafael Benitez, miezi sita tu baada ya kuteuliwa kuiongoza klabu hiyo.

Hatua hiyo imekuja baada ya Benitez kutaka kuungwa mkono ndani ya bodi ya wakurugenzi kununua wachezaji, kufuatia klabu hiyo kushinda kombe la dunia la vilabu, kwa kuifunga TP Mazembe siku ya Jumamosi.

Badala yake, Inter, ambayo inasuasua katika nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi ya Serie A, imeamua kumfukuza kazi Benitez.
Benitez
'Jino la pembe' Moratti na Benitez
Benitez alichukua kazi hiyo San Siro kutoka kwa Jose Mourinho.

Mourinho, ambaye aliondoka Inter na kwenda Real Madrid ya Uhispania, aliiongoza timu hiyo kuchukua ubingwa wa ligi ya Italia na klabu bingwa Ulaya msimu uliopita na kumuachia Benitez kazi ngumu ya kufuata nyayo zake.

Benitez, alichukua majukumu ya San Siro wiki moja baada ya kuondoka Liverpool ya England Juni 3. Ingawa amekuwa na majeruhi kadhaa, lakini imeonekana kuwa mbinu zake hazijaweza kumsaidia.

Ingawa Inter ina kiporo cha mechi mbili dhidi ya timu zilizo juu yake, imeshinda mechi sita tu kati ya mechi 15 za ligi.
katika kutetea ubingwa wao wa klabu bingwa, Inter imeweza kumaliza katika nafasi ya pili ya makundi, nyuma ya Tottenham ya England, na kuiacha katika wakati mgumu kwani itapambana na Bayern Munich katika raundi ya timu 16.

Ingawa Inter imeshinda Kombe la Dunia la Vilabu kwa kuichapa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, mafaniko hayo hayakumfanya Benitez kutotoa dukuduku lake baada ya mchezo huo wa fainali
Soma zaidi.....BBC


Wednesday, December 22, 2010

Nundu Aitaka Mamlaka Ya Usimamizi wa Bandari Kufanya kazi Kiufanisi

SERIKALI imeiagiza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), kwa kushirikiana na Kamati ya Kuboresha huduma bandarini kuhakikisha kwamba kuanzia sasa muda wa uondoshaji wa kontena katika Bandari ya Dar es Salaam unapungua ili TPA iendelee na jukumu lake la kuboresha huduma hiyo na kuleta ufanisi zaidi.

Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu ameitaka TPA kuanza mara moja kujenga na kuimarisha miundombinu ya bandari kwa kuzingatia mpango mkuu wa Mamlaka na kwamba mpango huo ni dira ya kuendeleza na hatimaye kufikiwa kwa lengo la nchi la kuifungua kibiashara ndani na nje ya nchi.

Nundu aliyasema hayo jana Dar es Salaam katika majumuisho ya ziara yake ya siku mbili ya kutembelea TPA ili kuona na kujifunza mambo muhimu ya uendeshaji na uendelezaji wa Bandari ya Dar es Salaam.

Akiongozana na Naibu wake, Dk. Athuman Mfutakamba, Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ephraim Mgawe na viongozi wengine wa bandari, Waziri Nundu alipata pia fursa ya kutembelea baadhi ya kampuni za kuhifadhi mizigo ya bandarini kwa lengo la kufahamu changamoto mbalimbali zinazoikabili mamlaka hiyo.


Alisema wakati ujenzi wa bandari ya Mwambani, Tanga ukiendelea, TPA inununue vifaa vitakavyoongeza ufanisi wa matumizi ya bandari hiyo na kusisitiza shirika lianze mawasiliano na uongozi wa Tanga ili maeneo ya ndani na nje ya bandari yanayotumika kwa shughuli zisizo za kibandari, zichukuliwe na kumilikishwa TPA.

Aidha, alisema mchakato wa kufanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina eneo la Kisarawe kwa ajili ya matumizi ya kuhifadhi mizigo, ufanyike mara moja hata kama ni kwa gharama za serikali na kuongeza kuwa ni vyema hilo likafanyika kabla ya mwaka wa fedha 2011/11 haujamalizika.

Alisisitiza wafanyakazi wa TPA kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma na matakwa ya wateja, na kuwa mawasiliano kati ya mamlaka na wateja yawe ya haraka na yenye tija.
Chanzo: Habari Leo

Tuesday, December 21, 2010

Kulikoni India?

Katika Miezi 6 wanachama wa baraza la usalama la UN wametembelea India
Yaahidiwa kiti cha Uanachama wa baraza la usalama la UN
Yaweka mikataba lukuki ya kibiashara,kijeshi,nishati ya nyuklia na mafuta

Made in  .............India
 
Sikiliza kibao hiki

Made In India

Upload Music
 
Cameron akiwa India-July 28,2010


Obama akiwa India- Nov 8,2010
Manmohan Singh U.S. President Barack Obama (L) waves as he is embraced by Indian Prime Minister Manmohan Singh (R) after speaking during a joint press conference at Hyderabad House on November 8, 2010 in New Delhi, India. The US President and the First Lady is on a ten day Asia tour with stops in India as well as Indonesia, South Korea and Japan.

Sarkozy(Rais wa Ufaransa)-Dec 6,2010


Wen Jiabao(Waziri Mkuu wa China)-Dec 16,2010


Medvedev(Rais wa Urusi)-Dec 21,2010

Hoseah amlipua Kikwete

 Asema anaogopa kushughulikia ufisadi wa vigogo


MTANDAO wa Wikileaks wa Marekani umeibua siri nzito kuhusu uwezo na nia ya Rais Jakaya Kikwete katika kushughulikia ufisadi, ukidai kuwa ndiye anayekwamisha kushtakiwa kwa baadhi ya vigogo serikalini wanaotuhumiwa kuhusika katika rushwa kubwa nchini.

Katika taarifa hiyo iliyochapishwa jana na gazeti la The Guardian  la Uingereza, likinuu taarifa za kibalozi za Marekani zilizoanikwa na Wikileaks, lilisema Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea, alimweleza mwanadiplomasia mmoja wa Kimarekani kwamba ugumu wa kupambana na ufisadi Tanzania unaanzia Ikulu.

Mtandao huo ulinukuu baadhi ya maelezo ya faragha kuhusu rushwa aliyoyatoa Dk. Hosea kwa mwanadiplomasia wa Kimarekani aitwaye Purnell Delly, walipokutana mwezi Julai mwaka 2007, Dar es Salaam.

Likinukuu mtandao huo, The Guardian liliandika, “Dk. Hosea alidokeza kuwa Rais Kikwete hafurahishwi na sheria kuchukua mkondo wake dhidi ya ufisadi ambao unaweza kuwatia hatiani vigogo wa ngazi za juu serikalini…. Hataki kuweka msingi wa kumwandama kiongozi yeyote miongoni mwa watangulizi wake (wastaafu).”

Linasema mwanadiplomasia huyo alisema: “Hosea alikuwa akisisitiza kwamba akiamua kuwa na makali, usalama wake binafsi utakuwa hatarini…anadai anaamini maisha yake yako hatarini, kwani amekuwa akipokea ujumbe wa vitisho kwa simu na barua na amekuwa akikumbushwa kila siku kwamba anapambana na ‘watu matajiri na wenye nguvu.’”

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Dk. Hosea alitoa maelezo yanayokatisha tamaa juu ya mustakabali wa mapambano dhidi ya ufisadi nchini na ugumu uliopo katika kuwashtaki watuhumiwa wa ufisadi mkubwa.

“Alituambia bila kufafanua... kwamba kesi zinazomhusu waziri mkuu au rais haziwezi kujadiliwa kabisa,” kilisema chombo hicho na kisha kufafanua: “Rais Kikwete hataki kumshughulikia mtangulizi wake yeyote mwenye tuhuma zinazostahili kufikishwa mahakamani.”

Dk. Hoseah anadaiwa kumueleza mwanadiplomasia huyo jinsi rushwa ilivyokithiri katika Benki Kuu ya Tanzania na visiwani Zanzibar, lakini akadokeza ugumu wa kuishughulikia kwa sababu tu wahusika wakuu ni watu ambao “hawahusiki”.

Hoseah alidokeza kuwa mambo yakiwa mabaya angeweza hata kukimbia nchi, kwa mujibu wa taarifa hiyo ikimnukuu mwanadiplomasia huyo wa Marekani.

“Ukihudhuria kwenye vikao vya juu (vya ndani), watu wanataka ujisikie kuwa wao ndio wamekuweka hapo ulipo. Wakiona huenendi na yale wanayotaka wao, basi hapo unakuwa katika hatari,” ilisema sehemu nyingine ya taarifa hiyo ikinukuu maelezo ya Dk. Hoseah.

Aidha, katika mazungumzo yao, Dk. Hoseah alimpa matumaini mwanadiplomasia huyo kwamba TAKUKURU ingeweza kuwachukulia hatua za kisheria watuhumiwa wote waliohusika katika kile alichokiita ‘dili chafu’ ya rushwa katika ununuzi wa rada ya kijeshi kutoka kampuni ya BAE ya Uingereza, hatua ambayo hata hivyo ilionekana isingeweza kutekelezwa na taasisi hiyo.

Wachambuzi wa mambo wanasema kauli hiyo ya Dk. Hoseah ilitokana na ukweli kwamba tayari wapelelezi wa Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa ya Jinai ya Uingereza (SFO) walikuwa wameshampelekea faili lote la watuhumiwa likiwa na ushahidi jambo ambalo lingeweza kumuepusha na hatari ambayo ingeweza kumfika kama uchunguzi huo ungefanywa na TAKUKURU yake.

Katika kashfa hiyo, serikali ya Tanzania inadaiwa kununua rada ya kuongozea ndege za kiraia na za kivita kutoka kampuni ya BAE System ya Uingereza kwa gharama kubwa ya dola 40 milioni, huku taarifa za uchunguzi kutoka SFO na vyanzo mbalimbali zikionyesha kuwa ununuzi huo haukuwa wa lazima na uligubikwa na rushwa.

Kashfa ya rada ilitendeka mwaka 1999, katika mazingira yaliyogubikwa na rushwa kwa watendaji serikalini ili waweze kulainisha watoa maamuzi. Kwa mujibu wa taarifa za maelezo ya Dk. Hoseah kwa mwanadiplomasia huyo, watuhumiwa zaidi wa rushwa ya rada wapo katika Wizara ya Ulinzi na jeshini.

“Dk. Hoseah aliliita suala la rada kuwa ni dili chafu na kusema inawahusu maofisa wa Wizara ya Ulinzi na vigogo wawili au mmoja wa jeshi (hawakutajwa majina),” ilieleza taarifa hiyo.

Kesi ya rada iliendelea kusikilizwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi jijini London, Uingereza .
Chanzo: Tanzania Daima

Rais Kibaki aahidi kuwalinda Wakenya baada ya watu 3 kuuwawa kwenye mlipuko Nairobi

      
    Rais wa Kenya,MwaiKibaki

Rais wa Kenya, Mwai Kibaki amesema usalama utaimarishwa msimu huu wa sikukuu ya Krisamasi kufuatia mlipuko wa bomu lililotokea jana mjini Nairobi.

Kamishna wa polisi nchini Kenya, Mathew Iteere, amesema uchunguzi umeanza kubaini kama mlipuko uliowaua watu 3 na kuwajeruhi wengine wapatao 40 mjini Nairobi jana jioni, ni shambulio la kigaidi.

Mlipuko huo uliotokea kwenye basi moja la kuelekea Kampala, Uganda. Kamishna Iteere, hakuuleza mlipuko huo kuwa shambulio la kigaidi, lakini amesema umesababishwa na kifaa cha kulipuka kilichokuwa sehemu ya mzigo wa abiria. Bwana Iteere pia amesema uchunguzi umeanza kubaini waliohusika kufanya hujuma hiyo.
Chanzo: Dw

Monday, December 20, 2010

Sitta: Nilitemwa uspika kwa hila za vigogo

Wastaafu wakibadilishana mawazo ya uongozi

Toka shoto Waziri mkuu mstaafu Edward Lowasa
na kulia ni Spika Mstaafu Samuel Sitta.

WAZIRI wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta jana alitoa kauli nyingine inayoweza kukitikisa chama chake cha CCM baada ya kueleza kuwa aliondolewa kwenye kinyang'anyiro cha kiti cha spika wa Bunge la Muungano kutokana na hila za viongozi ambao walishindwa kuhimili kasi ya utendaji wake kwenye chombo hicho cha kutunga sheria.


Sitta, ambaye alipata umaarufu baada ya kuliongoza Bunge la Tisa kwa mafanikio, ametoa kauli hiyo wiki chache baada ya kukaririwa na vyombo vya habari akisema bayana kuwa kuilipa kampuni tata ya Dowans fidia iliyoamuliwa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Kibiashara (ICC) ni sawa na kuhujumu uchumi.

Mbunge huyo wa Urambo Mashariki alijikuta akianguka kwenye kinyang'anyiro cha uspika wa Bunge la Kumi baada ya chama chake cha CCM kuamua kuwapa wanawake nafasi ya kuongoza moja ya mihimili ya nchi na hivyo kupitisha wagombea watatu wanawake katika mchakato uliompa ushindi Anne Makinda.

Jana, Sitta ambaye alikuwa akihojiwa na Mwananchi, alisema utendaji wake wa kasi na viwango uliwatisha viongozi wengi wa serikali na ndio maana wakaamua kutumia kigezo cha jinsia kumwondoa.
"Unajua nataka hili ilieleweke; juzi nilienda jimboni kwangu Urambo Mashariki nikawaeleza wapiga kura wangu kwa nini sasa mimi sio spika tena, maana wanaweza kudanganywa kama kazi imenishinda au nimefukuzwa," alisema Sitta.

"Watanzania lazima wajue mimi sijafukuzwa kazi wala sijashindwa kufanya kazi hiyo, ila kuna viongozi ambao ni wakuu wangu ndani ya chama chetu ambao wameshindwa kuendana na kasi na viwango vyangu ndio maana wakaamua kuweka sharti ambalo kamwe nisingeweza kulitimiza.

"Kigezo hicho cha jinsia walikileta katika hatua za mwisho za mchakato wa kumtafuta spika wakijua kwamba sitaweza kukitimiza na ningejua hilo mapema, nisingepeleka jina langu kuomba kuteuliwa tena."

Sitta alisema ni wazi kamba asingeweza kutimiza sharti kwamba spika aliyetakiwa safari hii ni mwanamke ndio maana hakuweza kuteuliwa tena kuwania nafsi hiyo.

"Mimi ni Sitta na nitabaki kuwa Sitita yule yule kama nilivyozaliwa na kwa vyovyote vile; nisingeweza kufanya chochote ili kuhakikisha sharti hilo nalitimiza," alisema Sitta.

Hata hivyo Sitta alisema kuwa endapo jina lake lingepitishwa, alikuwa na ukakika wa kurudi katika kiti hicho kwa kuwa asilimia kubwa ya wabunge walikuwa wameukubali utendaji wake.

Katika miaka ya mwisho ya uongozi wake wa Bunge la Tisa, Sitta alikuwa akilalamikia kuwepo kwa njama alizodai zinafanywa na mafisadi kutaka kumuangusha kwenye ubunge na wakati fulani alifikia hadi kuomba ulinzi zaidi kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda akisema anatishiwa maisha.

Sitta hajawahi kuwataka hadharani wapinazani wake, lakini baadhi ya vyombo vya habari viliwahi kumuhusisha na vita vya uwaziri mkuu, lakini akakanusha vikali akisema kama angetaka nafasi hiyo asingegombea uspika.

Sitta aliwataka wapigakura wake na Watanzania kwa ujumla kutosikitishwa na kitendo cha kuenguliwa kwenye kinyang'anyiro cha uspika, akisema kuwa anaamini bado Rais Jakaya Kikwete anawapenda watu wa Urambo na kuendelea kuwaheshimu ndio maana amemteua kushika dhamana nyingine.

"Nawaahidi Watanzania huu sio mwisho wa utendaji wangu wa kazi sasa kasi na viwango navihamishia katika Wizara hii muhimu na kwamba wananchi wasiogope tena Tanzania kuingia katika Shirikisho la Afrika Mashariki,"alisema.

Alisema akiwa Waziri wa Afrika Mashariki atahakikisha Watanzania wanafaidika na shirikisho hilo na kwamba suala la ardhi halitakuwepo kwa kuwa tahadhari zote zimechukuliwa.

Sitta alifanya ziara kwenye jimbo lake la Urambo Mashariki ambako pamoja na mambo mengine, alihudhuria mkutano wa uchaguzi wa mwenyekiti wa halmshauri ya Urambo.

Katika mkutano huo, Alhaji Adam Malunkwi wa CCM alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa halmashauri hiyo.
Kabla ya mkutano huo, Sitta, ambaye alipokewa na wapigakura wake kwa msafara wa pikipiki zaidi ya 70, magari zaidi ya 40 na vikundi mbalimbali vya hamasa, alitumia fursa hiyo kuwaeleza wapigakura hao kilichomfanya ashindwe kutetea nafasi yake ya uspika.

Sitta pia alitoa msaada wa mashine ya kusaga na kukoboa nafaka kwa kikundi cha kinamama wa Uyogo kutekeleza ahadi yake kabla ya uchaguzi mkuu

Alisema mashine hiyo itakuwa kitega uchumi chao kwa kile anachoamini kuwa ukimwezesha mama, umeiwezesha jamii.

Mbali na mashine hiyo Sitta pia alitoa msaada wa mashine ya umeme wa sola kwa ajili ya zahanati ya Uyogo.

Akikabidhi msaada huo alisema kabla ya umeme haujasambaa maeneo hayo, atahakikisha zahanati zote zinapata umeme huo kurahisisha huduma zake kwa jamii.

Chanzo: Mwananchi
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...