Mtazamohalisi

Friday, December 17, 2010

Mwinyi:Kwanini Mnaharakia Katiba Mpya?

Rais mstaafu wa awamu ya pili Ali Hassan Mwinyi amesema haoni umuhimu wa katiba mpya kwa sasa,nakuwataka wanaotoa madai ya katiba mpya kueleza maeneo gani ya kurekebishwa kwenye katiba ya sasa.

Rais Mstaafu,Ali Hassan Mwinyi

Alikuwa akijibu swali kwenye mahojiano na waandishi wa habari lililomtaka kujua msimamo wake juu ya kauli za madai ya katiba mpya.Mwinyi alisema"hakubaliani na wazo la kuwa na katiba mpya kwani kwasasa si muda muafaka".

Alisema"kabla ya kubadili katiba ya sasa,Watanzania wajiulize wenyewe ni kwa manufaa ya nani na kwa lengo gani lakutaka mabadiliko ".Hata hivyo,Mwinyi alisema ipo nafasi ya mazungumzo,lakini akapingana na wale wanaotoa madai ya haraka ,kama vile nchi imekosa kitu muhimu.

  Wakati Mwinyi akiyasema hayo, Profesa Lipumba mwenyekiti wa chama cha CUF amewataka watanzania kuungana katika madai ya katiba mpya. Alisema katiba mpya itasaidia kuwa na demokrasia ya kweli itakayo kuwa msingi kwa muelekeo wa maendeleo ya taifa kwani umuhimu wake kwasasa ni kwa faida ya vizazi vya sasa na baadae.

Habari kamili ,gonga hapa Guardian

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...