Mtazamohalisi

Wednesday, December 29, 2010

Bei Mpya Za umeme Hizi Hapa

SHIRIKA la Umeme nchini (TANESCO) limeainisha gharama mpya kwa watumiaji wa umeme zitakazoanza kutozwa kuanzia mwezi Januari mwakani.

Taarifa iliyotolewa kwenye vyombo vya habari na Ofisi ya Uhusiano wa Tanessco jijini Dar es Salaam jana ilianisha kuwa gharama hizo mpya zimegawanyika katika makundi matatu kulingana na mahitaji ya matumizi ya umeme.

Makundi hayo ni pamoja na watumiaji wa nishati hiyo kwa matumizi ya majumbani ambapo gharama ya chini kutoka 0-50 kWh/mo utauzwa kwa gharama ya sh 60 badala ya sh 49 ya sasa, tofauti yake ikiwa sh 11.

Kwa upande wa matumizi ya umeme ya kawaida bei ya matumizi kwa gharama za nishati kwa uniti imepanda kutoka sh 129 hadi kufikia Sh 157 ikiwa imeongezeka kwa sh 28.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kadhalika kwa upande wa mahitaji ya juu ya msongo mdogo, gharama za nishati kwa uniti imepanda kutoka sh 85 hadi sh 94 ikiwa imepanda kwa sh 9 zaidi.

Kadhalika mahitaji ya juu ya msongo mkubwa, gharama za nishati kwa uniti ambao ulikuwa ukiuzwa sh 79 sasa utauzwa sh 84 tofauti ikiwa ni sh tano.

Kwa upande wa Shirika la Umeme Zanzibar gharama za nishati kwa uniti kwa gharama mpya ya umeme itakuwa ni sh 83 badala ya sh 75 gharama hizo zikiwa zimepanda kwa sh 8.

Watumiaji ambao wameonekana kuumizwa katika gharama hizi mpya ni wale wa matumizi madogo madogo ya nyumbani na wenye matumizi ya kawaida ambao wamepandishiwa kwa zaidi ya Sh 10.

Kwa muhibu wa taarifa za TANESCO, hatua hiyo ya ongezeko la gharama imefikiwa baada ya gharama hizo kuidhinishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (EWURA).

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...