Mtazamohalisi

Friday, December 31, 2010

Kali Za Funga Mwaka

Huko Afrika kusini,kumekuwa na heka heka za mwisho kwa raia wa Zimbabwe kujiandikisha kisheria.
Raia Wazimbabwe atakaye kuwa hajajiandikisha atajikuta anarudishwa nchini Zimbabwe.

Mwezi Aprili ,2009 serikali ya Afrika kusini ilitoa ruhusa kwa Wazimbabwe kuingia nchi hiyo bila kibali kufuatia hali mbaya ya kisiasa na kiuchumi.Kusamehemewa Viza kwa Wazimbabwe,kulikuja kutokana na mazungumzo baina ya nmawaziri wa mambo ya ndani wa Zimbabwe na mwenzake wa Afrika kusini.



Huko Uhispania,wanawake wajawazito wamejikuta wakiharakisha kujifungua ili kuweza kupata posho toka serikalini.
Mabadiliko ya sheria ya mafao ya uzazi yataanza rasmi tarehe mosi 2011,ambapo serikali ya Uhispania imetangaza kusimamisha rasmi utoaji wa posho ya US$ 3000.
Kudidimia uchumi wa Uhispania kumepelekea serikali kusimamisha
posho ya ulezi .

Lengo la utoaji wa posho hiyo,ambayo ilianza rasmi mwaka 2007 lilikuwa ni kuwahamasisha raia wa Uhispania kuongeza vizazi ili kukabiliana tatizo la uhaba wa watu .

"Ili Uhispania kuendelea, inahitaji kuwa familia zenye watoto wengi.Na familia itabidi ihitaji misaada zaidi ili kuweza kuwa na watoto wengi na vyanzo vingi ili kumudu ulezi", Zapatero aliliambia bunge mwaka huo.
Zaidi soma .Aljazeera

Estonia tarehe 1/1/2011 itakuwa mwanachama wa 17 wa muungano wa sarafu wa ulaya,ni nchi ya kwanza toka Muungano wa nchi za soviet kujiunga na umoja wa Ulaya na Nato mwaka 2004.



Brazil -Kwa heri Lula ,karibu Dilma Roussef
Anaanza kazi rasmi tarehe 1/1/2011.
Mwanamke wa kwanza kuwa rais,nchini Brazil

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...