Mtazamohalisi

Friday, November 12, 2010

Malikia Elizabeth ajiunga na facebook, na kukutana na kashfa

Malikia Elizabeth wa Uingereza
Hivi karibuni, Queens Elizabeth II alijiunga na facebook na siku moja baada ya kujiunga katika tovuti hii ya jamii ukurasa wake ulijaa maoni machafu kutoka kwa watu . Walengwa wakuu walikuwa Carmilla na Charles na picha zao zilishambuliwa kwa maoni ya matusi.
Ukurasa  huu wa Familia ya Kifalme ya Uingereza, ulizinduliwa Novemba 8 pamoja na akaunti ya Twitter na Flickr. Wakati watu zaidi ya 220,000 "waliipenda", picha 28 katika albamu zilishambuliwa kwa maoni ya aibu na matusi.Familia ya kifalme ina wafuasi zaidi ya 75,500 kwenye Twitter na huweka picha mpya katika akaunti yake  ya Flickr kila siku. Pia ina channel kwenye Youtube

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...