Mtazamohalisi

Saturday, December 11, 2010

Obama Na Kisa Cha Lipstick

Atumia ushawishi wa Cliton kukubalika

Katika hali isiyo kawaida Rais wa Marekani ,Barack Obama amejikuta katika wakati mgumu mbele ya waandishi wa habari. Tukio hili limetokea leo mara baada ya kikao cha dharura na rais wa zamani wa marekani Bill Cliton.

Kama kawaida ilifika muda wa kuzungumza na waandishi wa habari kuelezea juu ya mazungumzo yao.
Na ndipo likaibuka jibu la Obama kumtaka Bill Cliton kuelezea umuhimu wa kukubaliana na Rais Obama juu ya makubaliano yake na chama cha Republican kuhusu kuendelea kutumia sheria ya upunguzaji wa kodi kwa watu wakipato cha juu iliyotumika wakati wa utawala wa George Bush.

Ila jambo lilochukua picha nzima ni tukio la Rais Obama kumuwacha pekee Bill Cliton kukabiliana na maswali ya waandishi wa habari huku yeye akienda kujumuika na Mkewe. Rais Obama aliomba dharura kwa Bill Cliton kwa kumwambia aendelea kwani mkewe Michelle Obama  alikuwa akimsubiri muda mrefu na anachelea kumkwaza.


Swali ambalo wengi wanajiuliza vipi Obama amuwachie Bill Cliton kuendelea kujibu maswali ya waandishi wa habari katika hali ngumu kama hii.Wachambuzi wamekifananisha kitendo hicho na kisa cha lipstick.
Inasemekana  ilitokea mwaka 1961 wakati Muigizaji wa Filamu Eddie Fisher alipomruhusu mkewe  Elizabeth Tailor kwenda Rome akijumuika na muigizaji mwenzie Richard Burton kwenda kuigiza katika filamu gonga hapa Cleopatra  hali yeye akibaki Los Angeles.

Hatimaye mapinduzi ya mapenzi yakaibuka,kwani kitendo cha Fisher kubaki Los Angeles kilimkutanisha na muigizaji wakike wa TV ya Ernie Kovac,Sue Kennedy .Na huko Rome Elizabeth Taylor alifungua ukurasa mpya wa mahusiano wa mapenzi na Richard Burton.

Nini kiliutambulisha ulimwengu juu ya mapinduzi haya ya mapenzi ni kitendo cha Sue Kennedy kuchukua Lipstick nyumbani kwa Elizabeth Taylor na Richard Burton na kumpa rafiki yake wa karibu na hapo ndiyo kosa kwani rafiki yake aliitoa siri kwa shangazi yake ambaye ni mwandishi.

Hatimaye talaka zikatembea na uhusiano mpya wa ndoa ukachanua baina ya Elizabeth Taylor na Richard Burton nahuku Eddie Fisher akijichukulia mazima Sue Kennedy.

Chanzo: michelemalkin.com

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...