Mtazamohalisi

Tuesday, December 7, 2010

Julian Asange Muasisi Wa Mtandao Wa Wikileaks Ajisalimisha

Katika kile kinachoonekana kuwa tayari kujibu tuhuma zinazomkabili ,Julian Asange ambaye anakabiliwa na kesi ya ubakaji nchini Sweden amejisalimisha katika mikono ya polisi wa uingereza.

Julian Asange ambaye mtandao wake wa Wikileaks umekuwa ni mwiba mchungu kwa Marekani na mataifa makubwa kwa kutoa kashfa za kijasusi, ameita kesi inayomkabili kuwa ni njama za Marekani.Mmoja wa mawakili wa bwana Asange, Mark Stephen amesema Sweden imepikwa na Marekani, ambayo imekuwa ikichukia kwa Wikileaks kutoa nyaraka za kiujasusi.
"Amesema swali ni kuwa Sweden inatumika na upande wa tatu au ni suala la uvunjaji wa taratibu za kimaingiliano."

Julian Asange anatarajiwa kufikishwa mahakama kuu ya Westminister jijini London siku ya jumanne , ambapo tarehe ya kusafirishwa  nchini Sweden itapangwa.
Chanzo:  http://english.aljazeera.net/news/europe/2010/12/2010127103159940201.html

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...