Mtazamohalisi

Sunday, November 28, 2010

Mgogoro Wa Uongozi Waibuka Katika Chama cha soka cha Zambia (FAZ)

Kalusha Bwalya
Kalusha Bwalya
Kundi hilo limesema kamati inayoongozwa na Rais wa FAZ Kalusha Bwalya, haishiki tena hatamu za uongozi.
Wamesema kamati iliyopita imejiondoa yenyewe baada ya wajumbe wake wanne kujiuzulu siku ya Jumamosi.Nahodha wa zamani wa timu ya Taifa ya Zambia, Kalusha Bwalya, aliwarejesha baadhi ya wanachama wa kamati yake baada ya wengine kujiondoa, ili kuweza kuwa na wajumbe wanaohitajika.
Mkutano wa siku ya Jumamosi ni wa kuidhinisha hatua hiyo na mwakilishi wa Fifa atahudhuria.
Lakini wajumbe watatu kati ya wanne waliowekwa na Bwalya wamekataa uteuzi huo
Kundi hilo la upinzani linajumuisha maafisa waandamizi kwa mchezo wa soka nchini Zambia, wakiwemo mkuu wa chama wa cha waamuzi na wawakilishi wa vilabu kadhaa.
Kamati hiyo mpya imesema wajumbe wake wamechaguliwa kwa ajili ya kufanya kazi kwa muda tu na uchaguzi mpya unatakiwa kufanyika ndani ya siku 90.
Chanzo:BBC-Swahili

Wakati hayo yakiendelea ,Timu ya ya Tanzania The Kilimanjaro Stars imeanza vibaya mashindano ya chalenji baada ya kufungwa bao moja kwa nunge dhidi ya Zambia.Rais Jakaya Kikwete, akipiga mpira ikiwa ni ishara ya kuzindua rasmi michuano ya CECAFA Tusker Challenge Cup, yaliyoanza jijini Dar es Salaam jana jioni katika Uwanja wa Taifa kati ya Timu ya Kilimanjaro Stars ya Tanzania na Zambia, Kilimanjrao imefungwa bao 1-0.Kiungo mshambuliaji wa Kilimanjaro, Mrisho Ngasa akimnyanyasa beki wa Zambia wakati wa mchezo huo .

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...