Mtazamohalisi

Saturday, January 15, 2011

Si Risasi Bali Ni Mawe Tu Yamkimbiza Rais Wa Tunisia

Ni kisa cha kijana msomi,26 mchuuzi wa matunda katika mji wa Sidi Bouzid kuhujumiwa na polisi kwa madai ya kufanya biashara kwa njia isiyo halali na kupelekea kujitoa muhanga kwa kujiwasha moto kupinga hali ya ukosefu wa ajira na malipo madogo ya ujira.

Kujitoa muhanga kwa kijana huyo kulipelekea muamko katika mji wa Sidi Bouzid na kuamsha hisia za uchungu juu ya hali ngumu ya maisha  na ukosefu wa ajira na kupelekea umma wa Tunisia kuamua kuingia barabarani kumtaka Rais wao kujiuzulu.

Rais Zine al Abidine Ben Ali aliitawala Tunisia kidiktekta kwa miaka 23 kwa mapinduzi ya kijeshi bila kumwaga damu huku akiwaweka vizuizini wapinzani wake, kuzuia uhuru wa habari huku akishindwa kukabiliana na tatizo la ajira.

Maandamano  ya tarehe 17/12/2010 yaliandaliwa na Chama cha wafanyakazi cha Tunisia nakuchukua muda wa mwezi mmoja kwa kugharimu maisha ya watu 23 yamepelekea Rais Zine al Abidine Ben Ali kuikimbia nchi na kwenda uhamishoni Saudi Arabia .

Nchi za magharibi ambazo zilikuwa washirika wakubwa wa rais Ali zimebariki mapinduzi hayo na kuyaita hatua ya kuelekea kwenye demokrasia ya kweli huku ufaransa mtawala wa zamani wa nchi hiyo ikikataa kutoa hifadhi ya ukimbizi wa rais Ali na Mkewe.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...