Mtazamohalisi

Monday, January 10, 2011

Jicho La Dunia Na Mustakbali wa Sudan

               Bashir kuchukua madeni yote ya Sudan Kusini

Rais wa Sudan, Omar Hassan al-Bashir amesema kuwa yuko tayari kuchukua madeni yote ya nchi hiyo iwapo eneo la Sudan Kusini litajitangazia uhuru wake baada ya kura ya maoni. Taarifa hiyo imetolewa leo na rais wa zamani wa Marekani, Jimmy Carter alipozungumza na kituo cha televisheni cha CNN.

Iwapo ahadi hiyo itathibitishwa, itakuwa ni ishara muhimu ya mapatano kutoka kwa Rais Bashir na itainua mzigo mkubwa wa fedha za serikali katika eneo la Kusini katika siku za mwanzo za uhuru wake unaotarajiwa. Bwana Carter amesema kuwa amezungumza na Rais Bashir ambaye amesema deni lote lazima lipelekwe Sudan Kaskazini na siyo Kusini.

Wakati hayo yakijiri Wasudan Kusini wameingia katika siku ya pili ya kupiga kura ya maoni ya kuamua iwapo wajitenge na Kaskazini na kuwa taifa huru, zoezi litakaloenda hadi tarehe 15 ya mwezi huu wa Januari. Aidha, kwa upande mwingine, watu zaidi ya 20 wameuawa katika mapigano ya Wasudan wenye asili ya Kiarabu wa kabila la Misseria na jamii ya Ngok Dinka katika eneo lenye mzozo la Abyei.
Chanzo: Dw

Sudan Taifa Kubwa kuliko yote Afrika linaelekea kugawanyika pande mbili kutokana na kura ya maoni inayoendelea Sudan ya Kusini .Angalia video upate picha ni wapi Sudan inaelekea


No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...