Mtazamohalisi

Monday, January 10, 2011

Gharama za Maisha na Ajira Ni Hatari Kwa watawala

Serikali nyingi zimejikuta katika wakati mgumu kutimiza ahadi kwa wananchi wao hasa masuala mazima ya kupanda gharama za maisha na ajira kwa vijana hasa wale wanaomaliza masomo yao ya elimu ya juu.Kupanda kwa gharama za maisha na ajira kwa vijana imekuwa ni jambo linahatarisha uwepo wa serikali.


Ukiyatizama masuala haya kwa makini utagundua kunamguso kwa kila jamii toka pande zote za dunia ila hutofautiana njia zakuyatatua.

Ninachotaka kufungua macho kwa serikali yetu ya Tanzania ni kutafuta njia mbadala za kujiwezesha kujikwamua toka dimbwi zito la umaskini na kusababisha sauti ya mnyonge kuchoka kuvumilia kuona wakubwa wakiji nafasi .

Inapasa kubadilishana uzoefu toka kwa marafiki zetu wa kimataifa ili kufikia lengo la kumkwamua mnyonge ,hebu  rudisha kumbukumbu za uchaguzi wa mawaka 2010 utagundua ni kutokana na hasira za wananchi ndiyo maana vyama vya upinzani vikapata viti vingi bungeni.

Inasemekana kwa matokeo ya uchaguzi mkuu CCM imeathirika hasa suala zima la posho toka bilioni 1 kwa mwezi hadi milioni 800 na kupelekea chama hicho kuchukua hatua za kurekebisha matumizi ya posho hiyo kwa kufuta posho kwa baadhi ya taasisi zake na watendaji kwenye chama.

Hapa tunapata picha ya kuwa CCM isipokuwa makini 2015 mambo yanaweza kubadilika zaidi ikiwa hatua madhubuti ya kurekebisha maisha ya mtanzania hazitachukuliwa.

Nchi kama ya  Falme ZA Kiarabu(UAE) imetunga sheria kwa ajili ya kupambana na tatizo la ajira, wakati nchi nyengine kama Algeria na Tunisia  hali imekuwa mbaya kwa vijana kuingia mitaani kulazimisha serikali zao kuangalia kupanda kwa gharama za maisha na ukosefu wa ajira.


Anger in Algeria sparks fresh riots
Uploaded by euronews-en. - Up-to-the minute news videos.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...