Mtazamohalisi

Wednesday, January 26, 2011

Palestina yajibu kuhusu 'nyaraka za siri'

Maafisa wa Palestina wameishutumu al-Jazeera kwa kupotosha, baada ya kutoa taarifa za siri zilizokusudia kuonyesha nchi hiyo kuwa na maridhiano makubwa na Israel.

Rais Mahmoud Abbas alisema siri hizo zimechanganya kwa makusudi misimamo ya Palestina na Israel.

Nyaraka hizo zinasema kuwa Palestina iliikubalia Israel kubaki na eneo kubwa la mashariki mwa Israel wanalomiliki kinyume cha sheria- jambo ambalo Israel imelikataa.

BBC imeshindwa kuthibitisha binafsi nyaraka hizo.

Al-Jazeera ilisema ina rekodi 16,076 za siri za mikutano, barua pepe, na mawasiliano baina ya Palestina, Israeli na viongozi wa Marekani, baina ya mwaka 2000-2010.

soma zaidi....... BBC

Kupitia Nyaraka zenyewe gonga hapa http://english.aljazeera.net/palestinepapers/

Maoni Ya Wachambuzi

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...