Mtazamohalisi

Thursday, January 27, 2011

Mlinzi wa Hitler Bado Wamo


Rochus Misch mlinzi wa Hitler kwa muda wa miaka 5 alishuhudia
Hitler akijiua.

Zaidi ya miaka 65 tangu kwisha kwa vita ya pili ya dunia mlinzi wa mwisho wa Hitler anasema kwa hivi sasa hawezi kujibu e-mails kutokana na umri wake.

Rochus Misch,miaka 93 alishuhudia Hitler akijiua mara baada ya kuona kifaru cha jeshi la Urusi kimkaribia.Aliwahi kubadilishana uzoefu na Christopher McQuarrie,mwandishi aliyetengeneza Valkyrie filamu ya mwaka 2008 ikielezea jinsi Hitler alivyojiua.

Mcheza sinema wa Hollywood ,Tom Cruise ambaye aliigiza katika filamu hiyo hakutaka kukutana na Misch na kuliambia gazeti la Los Angeles Times kuwa"shetani ni shetani,haijalishi umri aliokuwa nao".

Amenukuliwa na gazeti la Berliner Kurier ya kwamba hawezi kujibu barua pepe anazotumiwa kutokana na umri aliokuwa nao.

Mwezi January 16 ,1945 kufuatia Ujerumani kushindwa vitani Misch na wasaidizi wa karibu wa Hitler walikimbilia Führerbunker katika jiji la Berlin. Nakujitokeza kwake mara baada ya vita, alijikuta akitiwa mikononi na Jeshi Jekundu . Aliachiwa huru mwaka 1954, na tangu wakati huo na hadi sasa Misch anaishi katika jiji la Berlin.

Kwakujua alivyokutana na Hitler na majukumu yake endelea......Hitler

Watch Valkyrie Trailer

Hitler Private resident

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...