Mtazamohalisi

Saturday, November 27, 2010

Kijana Wa Kisomali Akamatwa Katika Tukio La Kigaidi.

This image provided by the Mauthnomah County Sheriff's Office shows Mohamed Osman Mohamud, 19, arrested and charged with attempted use of a weapon of   
   Mtuhumiwa wa Ugaidi Mohamed
       Osman Mohamud,19

Mohamed Osman Mohamud,mzaliwa wa somalia mwenye uraia wa Marekani amekamatwa na makachero wa FBI akiwa katika harakati za kulipumua bomu kwenye gari aliloliegesha karibu kabisa na mkusanyiko wa watu waliokuwa wakiwasha taa katika mti wa Krismasi.

Taarifa za kijasusi ziliwafikia majasusi wa FBI toka kwa mtu wa karibu wa mtuhumiwa huyo nakufatilia nyendo zake kwa ushahidi zaidi,Mohamed aliwekwa kizuizini baada ya jaribio lake la kutumia simu kulipulia gari aliloliegesha kufeli kwa kujikuta amejilengesha kwa makachero wa FBI.

Mtuhumiwa anatarajiwa kufikishwa mahakama kuu ya Portland huko Oregon siku ya Jumatatu kwa mashtaka ya utumiaji wa silaha za maangamizi.Kwa mujibu wa sheria huenda mtuhumiwa akahukumiwa maisha na kulipa faini ya dola 250'000.

Wakati huo huo ,Waziri wa mambo ya nje wa somalia Mohamed Abdullahi Omaar amesema "serikali yake ipo tayari kutoa ushirikiano ili tukio kama hilo lisiweze kujitokeza tena.kwani tukio hilo si tu limeiathiri  familia ya Mohamud bali pia bali hata wahanga waliokusudiwa kushambuliwa.

Maelfu ya wasomali wamepata hifadhi nchini Marekani tangu  mwaka 1991 wakati utawala wa sheria ulipoanguka.
Chanzo: http://www.msnbc.msn.com/id/40389899/ns/us_news-security/
Full story Video

Rais Obama Apigwa Kiwiko Akicheza Mpira Wa Kikapu

Ashonwa kwa nyuzi 12
Aliyemuumiza anaitwa Rey Decerega


Kutoka vyanzo mbali mbali vya habari leo asubuhi Rais wa Marekani Barack Obama amepatwa na jeraha la mdomoni kufuatia kupigwa kiwiko na mchezaji wa upande mwengine katika mazoezi ya Mpira wa Kikapu ambayo yalijumuisha ndugu na marafiki zake.

Rais Obama ilibdi ashonwe kwa nyuzi 12 baada ya kujeruhiwa na Rey Decerega.Taarifa toka Ikulu ya Marekani imemnukuu Bwana Decerega akisema"leo amefahamu kama rais ni mahiri na ni mwanamichezo mzuri.Nimefurahi kucheza nae Mpira wa kikapu asubuhi hii.Natumaini atarudi tena kiwanjani hivi karibuni".Bwana Rey Decerega ni mfanyakazi wa taasisi ya kihispania katika Congress.

Ikulu ya Marekani imetoa majina ya ndugu wa rais waliocheza nae Mpira wa Kikapu na miongoni mwao ni mpwa wake Avery Robinson,Waziri wa elimu Arne Duncan na Reggie Love  msaidizi binafsi wa Obama ,ambaye anacheza katika chuo kikuu cha Duke,lakini haikuetoa majina ya wachezaji wengine.

Habari nyengine inatupasha kuwa askari mstaafu  amewekwa kizuizini kwa kutishia kumuua rais Obama.
Akutwa na silaha 16 nyumbani kwake ,ni mstaafu mwenye miaka 78

Image: Michael Stephen Bowden
Aliyetishia kumuua Rais Obama,Askari Mstaafu
Bwana Michael Stephen Bowden,78
Taarifa hiyo ya kiapo cha kuua imetolewa na idara ya ujasusi imesema Bwana Michael Bowden aliwekwa kizuizini  mwanzoni mwa mwezi huu.Wakati Bowden alipomuambia muuguzi mmoja katika zahanati maalumu ya wastaafu iliyopo South Carolina kwamba"nafikiri kwenda Washington,kumuua rais kwa kuwa hajafanya jitihada za kuwasaidia wamarekani weusi". Alitamka hayo wakati muuguzi alipomuuliza ya kuwa kama alishawahi kujitoa muhanga,baadaye iligundulikana Bwana Bowden hana hatia ya kujitoa muhanga.
Chanzo: http://www.msnbc.msn.com/id/40379129/ns/us_news-crime_and_courts/

Utekelezaji Wa Katiba Kenya Mashakani


Wabunge wa Kenya

Mchakato wa utekelezwaji wa katiba mpya nchini Kenya, umepata pigo kubwa baada ya wabunge kukataa kuidhinisha makamishna wa tume mbili muhimu waliokuwa wamependekezwa.
Wabunge walisema orodha hiyo haijazingatia uwakilishi wa mikoa yote na inapaswa kurejeshwa kwa Rais Mwai Kibaki na Waziri Mkuu Raila Odinga.
Wabunge pia walikataa kuidhinisha kamati iliyopendekezwa kusimamia ugawaji wa rasilimali.
Kufuatia uamuzi huo wa wabunge, huenda ikatoa fursa kwa kwa raia yeyote wa Kenya kwenda mahakamani kuwasilisha kesi ya kutaka bunge livunjwe.
Hata hivyo wataalamu wa masuala ya sheria nchini Kenya,wanasema uamuzi huo wa wabunge huenda ukasababisha mzozo wa kisiasa na kikatiba
Akizungumza na BBC mkuu wa kitivo cha sheria cha chuo kikuu cha African Nazarene Dkt. Morris Mbondenyi amesema kuwa hatua hii itachelewesha utekelezaji wa katiba mpya.
Chanzo: BBC

Friday, November 26, 2010

Jeshi la Brazil Lapiga Hatua Katika Vita Dhidi Ya Madawa Ya Kulevya

Baada ya siku tano za operesheni dhidi ya makundi yanayofanya biashara ya madawa ya kulevya,hatimaye jeshi la Brazil limefanikiwa kuutia mkononi kitongoji cha Vila Cruzeiro katika jiji la Rio De Janeiro.Jeshi la polisi la nchi hiyo lilipeleka vifaru,helikopta,jeshi la utunguaji na wanajeshi wenye silaha nzito,wanajeshi wa majini na pia kikosi cha  akiba cha wanajeshi 17'500 .

 Katika operesheni hiyo washukiwa 30 wa usafirishaji wa madawa ya kulevya waliuawa .Hali hii imesababisha makundi ya wahalifu wa madawa ya kulevya kurudi nyuma,na huku likitolewa tangazo kwa wakaazi wa vitongoji vya Vila Cruzeiro kutotoka nje.Wengi wa wakaazi wanasema haijawahi kutokea operesheni nzito kama hiyo na imewapelekea kuhisi kuwa wamo katika uwanja wa vita.

Wakati huohuo msemaji wa jeshi la Brazil wanasema operesheni hiyo haitakoma kwani lengo halijafikiwa la kurudisha hali kuwa kama kawaida,kwani vitongoji vya Vila Cruzeiro ni maarufu kwa kutawaliwa na ghasia na biashara haramu za madawa ya kulevya.

Mwaka 2012, Brazil inatarajiwa kuwa mwenyeji wa michezo ya olimpiki na pia mwaka 2014 wanatarajia kuwa wenyeji wa kombe la dunia.
Mwezi Oktoba 2009 kundi la wahalifu  wa madawa ya kulevya lilitungua ndege ya polisi jirani na uwanja wa Maracana, moja ya viwanja vitakavyotumika katika kombe la dunia 2014,nakuua maafisa wa tatu.
Chanzo:Aljazeera
            

Uongozi si Kuula

Na Hafidh Kido
Wiki hii ndugu Rais wa jamhuri ya Tanzania Jakaya Kikwete, ameteua baraza la mawaziri ambao wataongoza wizara mbalimabali kwa miaka mitano ya mwisho katika uongozi wake. Majukumu ya kufuatilia, kusikiliza na kutekeleza sera za serikali na amri za Rais zitakua juu ya mabega ya wanaadamu hawa.

Cha ajabu na kushangaza akili za wenye busara ni habari za salamu za pongezi kwa wateule hawa; bila kufikiri hawastahiki pongezi hizo, badala yake nilitegemea salamu za pole kwa watu hao walioteuliwa na Rais kushikilia nyadhifa ngumu na zenye kuhitaji moyo mkuu wa kujitolea, tena kwa miaka yote mitano bila kujali sikukuu wala mwisho wa wiki, bila kujali wapo ofisini ama nje ya ofisi, bila ya kujali mwenye kuhitaji msaada unamfahamu ama humfahamu.

Maneno mengi yamevuma na kughariki masikio yetu weye kufikiri, lakini ambalo nimelidaka kwa ngoma zagu za masikio na kuendelea kubaki kwenye ubongo wangu wa kutunzia kumbukumbu ni lile neno ‘wameula.’

Naam! neno hilo limekuwa likijirudia mara kwa mara toka vinywani mwa watu kuwa mtu fulai ameula, ameukwaa uwaziri. Ameula nini? Kuenda kufisidi mali ya umma, ama kuonea wenye kudai haki na kulipiza visasi kwa waliowakosea kabla hawajawa na madaraka makubwa kama hayo ya uwaziri.

Hivyo naomba kueleza jamii kuwa unapoteuliwa na Rais kwa nafasi yoyote si kuwa umeula ama umeukwaa bali unakabiliwa na majukumu mazito ya nchi. Pindi unapoapa kuilinda katiba ya nchi yako si jambo dogo hata chembe, labda uwe na moyo mgumu namna gani. Lazima dhamira itakusuta.

Kumbuka utatumika kuenda kuiwakilisha nchi, ukilala muda wowote tegemea kuamshwa ili ukaitumikie nchi, ulapo sikukuu iwe ya kiserikali au ya kidini, tegemea kupigiwa simu ili ukaitumikie nchi yako. Uwapo na familia yako mnakula raha ufukweni ama mnatembea mandari, tegemea kuitwa ukaitumikie nchi; kifupi muda wako mwingi hutoishi kwa amani wala hakuna raharaha.

Na umalizapo miaka mitano ya utawala kama umefanya madudu ujue jamii itakuhukumu kwa ulichowatendea; wala usidhani watakuacha tu hivihivi ule ulichochuma kwa kutumia jasho na unyonge wao.

Hivyo inapaswa kujilinda na kutazama maendeleo zaidi badala ya kujisifia umeukwaa ukigogo, maana kigogo kikishakauka ndipo utakapojua ulikua unaitumikia jamii ama tumbo lako. Wasaka tonge wanakuandama , hivyo usitegemee kulala usigizi wa pono, kazi kwanza.

Thursday, November 25, 2010

Vita Dhidi Ya Madawa Ya Kulevya,Jeshi La Brazil Laingia Mitaani

Ndani viungo ya mitaa ya watu maskini kwenye makaazi ya Cruzeiro katika Jiji La Rio De Janeiro wakati jeshi likijiandaa  kupambana na magenge ya watu wa madawa wa kulevya.

Waamuzi Kugoma Scotland

Ratiba za mechi mbalimbali nchini Scotland zinakabiliwa na hatari ya kuvurugika wiki ijayo baada ya waamuzi wa daraja la kwanza kupiga kura kuidhinisha mgomo wao.

Waamuzi hao wa Scotland wamekatishwa tamaa na jinsi wanavyoandamwa msimu huu na hata kutishiwa maisha.
BBC nchini Scotland imegundua kuwa waamuzi wana wasiwasi na pia kushushwa heshima yao na baadhi ya vilabu na hata watu binafsi.
Kumekuwa na ongezeko la vitisho kwa usalama wao kutokana na kuchukiwa na jamii.
Uamuzi wa kugoma ulifikiwa na katika mkutano wa chama cha waamuzi uliofanyika siku ya Jumapili mchana, wengi wakiunga mkono.
Kuna mechi sita za Ligi Kuu ya Scotland zilizopangwa kuchezwa mwishoni mwa wiki ijayo.
Chanzo:BBC

Wakubwa Wakiwa Ugenini

Malikia Elizabeth Akiwa Abu dhabi 
Malikia Elizabeth na Mumewe Prince Philip
wakiwasili Katika Msikiti Mkuu
wa kumbukumbu wa Zayed
State visit: The Queen emerges after removing her footwear as a mark of respect before going in
Malikia Akiingia Msikiti wa Zayed Bila Viatu Kama Ishara Ya Heshima
Toeing the line: The Queen removed her shoes before entering
Miguu Ya Malikia Ikiwa na Soksi Ndani Ya Msikiti Wa Zayed-Abudhabi
(Picha zimepigwa 24 Nov,2010)
Mke wa Rais Gorge Bush, Bi Laura Bush Alipotembelea Saudi Arabia

Laura Bush Alipotembelea Saudi Arabia
Okt,2007


 Ziara ya Rais Barack Obama Nchini Indonesia
Barack na Michelle Obama pamoja na Imam Mkuu wa Msikiti wa Istiqlal, Jakarta.
Nov, 2010.

Wednesday, November 24, 2010

Wazungu Wa Unga Kukiona Cha Moto Z'bar


Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar,
      Maalim Seif Sharif Hamad

VIGOGO wa dawa za kulevya Zanzibar watakabiliwa na hali ngumu, baada ya Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohammed Shein, kumkabidhi jukumu la kudhibiti dawa hizo msaidizi wake, Maalim Seif Sharif Hamad.

Hayo yalibainika jana, baada ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif, kukabidhiwa rasmi ofisi yake katika mtaa wa Migombani mjini Zanzibar na baadaye kuzungumza na waandishi wa habari.

Maalim Seif alisema amekabidhiwa majukumu manne na Dk. Shein ambayo ni mapambano dhidi ya dawa za kulevya, ukimwi, mazingira na kushughulikia kero za walemavu visiwani humo.
Hatua ya Dk. Shein kumkabidhi majukumu hayo msaidizi wake ni kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar Ibara ya 20 ambayo imebainisha wadhifa wa Makamu wa Kwanza kuwa ni mshauri mkuu wa Rais na atatekeleza majukumu atakayopangiwa.
“Suala la dawa za kulevya ni tatizo katika nchi yetu, hivi karibuni imeripotiwa kukamatwa watu wanaojihusisha huko Tanzania Bara na Zanzibar,” alisema Maalim Seif.

Hatua ya Dk. Shein kumkabidhi jukumu hilo Seif, imekuja huku wananchi wengi wakiwemo viongozi wa serikali za mitaa (Masheha) kulalamikia udhibiti finyu wa dawa za kulevya kuwa mgumu kwa sababu hata wanapowaripoti wahusika hawakamatwi.

Alisema, katika kutekeleza majukumu yake suala la mazingira atalisimamia kwa karibu, kutokana na ukweli kwamba eneo hilo ni muhimu kwa maisha ya binadamu na viumbe wengine.
Alisisitiza kuwa uharibifu wa maziungira ni ajenda kuu duniani na Zanzibar itatoa kipaumbele katika suala la kudhibiti uchafuzi wa mazingira

Aidha, alisema serikali ya awamu ya saba itafanya kazi kwa karibu katika kusaidia kupunguza kasi ya maambukizi ya ukimwi, ikiwemo kutoa elimu ya kutosha.


Hata hivyo, Maalim Seif, ambaye alijijengea sifa ya uwajibikaji kazini alipokuwa Waziri Kiongozi wa Zanzibar miaka ya 1980, alisema mafanikio ya serikali yatapatikana iwapo kila mtumishi atawajibika ipasavyo.

Alisema ni wajibu wa kila mtumishi kufika kazini mapema na kutekeleza majukumu yake na kuwataka watendaji kuondoa urasimu.

Maalim Seif, alisema atakuwa mtiifu kwa serikali yake na kuhakikisha anafika ofisini saa 1:30 asubuhi huku akisisitiza wafanyakazi wengine kuwahi kufika kazini.
“Kila mmoja ajue tuko hapa kwa ajili ya wananchi, wananchi wetu wanataka huduma bora, taratibu za kazi zifuatwe na viongozi tusimamie majukumu, mambo ya kusumbua wananchi njoo kesho, kesho kutwa yakomeshwe,” alionya Maalim Seif.

Tayari Makamu wa Pili wa Rais, Balozi Seif Ali Idd, ambaye kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar ibara ya 20 (7) ndiye kiongozi wa shughuli za serikali katika Baraza la Wawakilishi amekabidhiwa ofisi yake katika mtaa wa Vuga mjini Zanzibar.
Katika hafla ya makabidhiano hayo, Balozi Seif Ali Idd aliwahimiza watendaji kuheshimu mipaka ya kazi zao na kujiepusha na vitendo vya ubadhirifu wa mali za umma.
Chanzo: Tanzania Daima, 23 Novemba 2010

Nigeria Yakamata Shehena Ya Madawa Ya Kulevya



Maofisa wa kupambana na madawa ya kulevya wanigeria wamekamata shehena ya madawa ya kulevya ambayo yalikuwa yamefichwa ndani ya spea za magari kwenye gari iliyosajiliwa iran,maafisa hao walipata msaada wa kijasusi wa shehena hiyo toka Marekani.Inakisiwa thamani ya madawa hayo ni dola milioni 9.9 ambao ulikuwa unasafirishwa kuelekea Ulaya.

Mwezi uliopita serikali ya Nigeria ilikamata shehena 13 za silaha haramu zikiwemo roketi,mizinga na bunduki zinazosemekana toka Iran. Baada ya kukamata shehena hizo Serikali ya Nigeria iliwasilisha malalamiko dhidi ya Iran katika Umoja wa Mataifa.
Umoja wa mataifa umeiwekea Iran vikwazo vya kusafirisha silaha nje ya nchi.

Nigeria imekuwa ndiyo njia kuu ya kusafirisha madawa kwa nchi za Amerika, Ulaya na Afrika .

Wakati huo huo, Serikali ya Gambia mekatisha uhusiano wake na serikali ya Iran nakuwataka maafisa wa ubalozi wa Iran kuondoka ncho hiyo katika muda wa masaa 48.Haijaelezwa sababu ya hatua hiyo nini lakini duru za habari zinahusisha na tukio la mwezi uliopita la serikali ya Nigeria kukamata shehena 13 za silaha zilizosafirishwa kiharamu , ambazo zinadaiwa zikipelekwa Gambia.
Hata hivyo Afisa wa ngazi ya juu wa Iran Alaeddin Borujerdi amesema hatua hiyo ya Gambia imechukuliwa kutokana na shinikizo kutoka Marekani.

 Chanzo:CNN, BBC-Swahili

Baraza Jipya La Mawaziri

Rais Jakaya Kikwete akitangaza Baraza Jipya
Ikulu,Dar-es -Salaam
                                                                       

Rais :Jakaya Kikwete
Makamu wa Rais, Dk.Mohamed Gharib Bilal
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda
Wizara (Waziri na Naibu Waziri)
1. Ofisi ya Rais (Utawala Bora) Mathias Chikawe
2. Ofisi ya Rais – Mahusiano na Uratibu:  Stephen Wassira
3.Ofisi ya Rais  – Menejimenti ya Utumishi wa Umma Hawa Ghasia
4. Ofisi ya Makamu wa Rais – ( Muungano):  Samia Suluhu
5. . Ofisi ya  Makamu wa Rais – (Mazingira) Dr. Terezya Luoga Hovisa
6. Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge): William Lukuvi
7.  Uwekezaji na Uwezeshaji Dr. Mary Nagu
8. Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) George Huruma Mkuchika
Naibu: Aggrey Mwanri
Naibu: Kassim Majaliwa
9. Wizara ya Fedha Mustapha Mkulo
Naibu: Gregory Teu
Naibu: Pereira Ame Silima
10. Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Shamsi Vuai Nahodha
Naibu: Balozi Khamis Suedi Kagasheki
11. Wizara ya Katiba na Sheria Celina Kombani
12. Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard K. Membe Naibu: Mahadhi Juma Mahadhi
13 . Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Dr. Hussein Ali Hassan Mwinyi
14. Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dr. Mathayo David Mathayo
Naibu: Benedict Ole Nangoro
15. Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mnyaa Mbarawa
Naibu: Charles Kitwanga
16. Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka Naibu: Goodluck Ole Madeye
17. Wizara ya Maliasili na Utalii Ezekiel Maige
18. Wizara ya Nishati na Madini William Mganga Ngeleja 1. Adam Kigoma Malima
19. Wizara ya Ujenzi Dr. John Pombe Magufuli
Naibu: Dr. Harrison Mwakyembe
20. Wizara ya Uchukuzi Omari Nundu
Naibu: Athumani Mfutakamba
21. Wizara ya Viwanda na Biashara Dr. Cyril Chami
Naibu: Lazaro Nyalandu
22. Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Dr. Shukuru Kawambwa
Naibu: Philipo Mulugo
23. Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Haji Hussein Mpanda
Naibu: Dr. Lucy Nkya
24. Wizara ya Kazi na Ajira Gaudensia Kabaka Makongoro Mahanga
25. Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto Sophia Simba
Naibu: Umi Ali Mwalimu
26. Wizara ya Habari, Vijana na Michezo Emmanuel John Nchimbi
Naibu:Dr. Fenella Mukangara
27. Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Samuel John Sitta
Naibu Dr. Abdallah Juma Abdallah
28. Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika Prof. Jumanne Maghembe
Naibu: Christopher Chiza
29. Wizara ya Maji: Prof. Mark James Mwandosya
Naibu: Eng. Gerson Lwinge

Rais Atangaza Muundo wa Wizara na Mawaziri

Marekebisho ya Muundo wa Wizara


Majina Ya Baraza la Mawaziri

Tuesday, November 23, 2010

Mahakama Kuu Nchini India Imemtaka Waziri Mkuu Kujileza

Kufuatia kutomfungulia mashtaka waziri wake wa mawasiliano                
Kutokana na utoaji wa leseni za biashara kwa bei ya mwaka 2001
Uamuzi wowote wa mahakama utakaomtia hatiani huenda ukahatarisha nafasi yake

Waziri Mkuu wa India
Dk.Manmohan Singh
                                  

Duru za siasa nchini India zimeingia katika sura mpya, baada ya Jumanne hii kwa Waziri Mkuu wake Bwana Manmohan Singh kutakiwa na mahakama kuu kujibu maswali ya kwanini imemchukua miezi 16 bila kumfungulia mashtaka Waziri wa mawasiliano aliyejiuzulu hivi karibuni kwa kile kinachoitwa kashfa ya uuzaji wa leseni kwa makampuni ya mawasiliano kwa bei ya mwaka 2001.Ombi la kumtaka waziri mkuu kumchukulia hatua za kisheria waziri wa mawasiliano lilitolewa na Mbunge wa upinzani.Uamuzi wowote wa mahakama utakaomtia hatiani Bwana Singh huenda ukamuia vigumu kubaki katika nafasi yake.

Kati ya mwaka 2007 na 2008, waziri wa mawasiliano Bw.Raja alitoa leseni kwa makampuni 85 kati ya 122 yaliyo omba kwa bei ya chini iliyopelekea hazina kupata hasara ya dola bilioni 39,kwa mujibu wa maafisa waliochunguza. Hata hivyo Bwana Raja alijiuzulu kwa shinikizo lakini amekana kuwa na makosa.
Kwa mujibu wa mkaguzi mkuu wa mahesabu anasema makampuni mengi ya mawasiliano yalificha habari,kughushi nyaraka na pia kutumia njia za ulaghai kupata leseni.

Bunge la India limesimama kwa kile upande wa upinzani unachodai tume ya uchunguzi wa kashfa ya utoaji wa leseni ya mawasiliano.Shughuli za serikali haziathiriki kutokana na kusimama kwa bunge.
India ndio inayoongoza duniani katika sekta ya mawasiliano ambayo inakuwa kwa kasi kwa takribani ya watumiaji milioni 700
Chanzo : http://english.aljazeera.net/news/asia/2010/11/20101123751335817.html

Uongozi wa Chadema Kuweni Makini

Mara nyingi nimetokea kupenda kile ninachokiita mabadiliko ya kisiasa Tanzania,kwa sababu mabadiliko hayo yatamsaidia Mtanzania mnyonge kwa sauti yake kusikika. Ni miaka takribani 19 toka mwaka 19991 uliporuhusiwa mfumo wa vyama vingi. Wakati asilimia 20 ilikubali kuanzishwa kwa vyama vingi asilimia 80 ilipinga suala hilo,hayo ni kwa mujibu wa matokea ya Tume ya Jaji Nyalali.Lakini kwa kuendana na mabadiliko ya dunia ,Serikali kwa wakati huo chini ya Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi iliamua kwa moyo mmoja kuruhusu mfumo wa vyama vingi nakumbuka Rais Mwinyi maarufu kama Mzee Ruksa aliwahi kudokezea kuwa kutakuja utitiri wa vyama lakini hivyo vyote vitajichuja vyenyewe kutokana na sera zao kwa wananchi nakuita utitiri huo wa vyama kuwa ni "riziki dudu"  kwani kuwepo kwake kuna watakopata kula humo humo.

Nikija kwenye mada yangu nina wasiwasi na baadhi ya wanasiasa kwa  kutupa wakati mgumu hasa linapokuja suala la kiongozi wa chama kuhama chama kimoja kwenda chengine na huku nyuma akitoa kashfa nzito za kwanini amehama na wakati huo huo mwengine anatoka chama hicho na kuhamia chengine na kutoa kashfa kama hizo.Ni haki ya kiraia kuamua kuwa mfuasi wa chama unachokipenda lakini haingii akilini kuwa ni mtu makini unapokuwa ni mtu wa kuhama hama.

Hivi karibuni, baada ya Uchaguzi mkuu na kwa mara ya kwanza vyama vya upinzani hasa Chadema kupata viti vingi bungeni kwa kweli ni jambo la kujifahari. Ila nina patwa na wasi wasi kwanini kuna malalamiko kwa baadhi ya viongozi waliokuwa wa Chadema kulalamikia Uongozi Mkuu unawatupa mkono linapokuja suala la kuwasaidia wakati wanapokabiliwa na matatizo. Wiki hii Mwenyekii wa Chadema mkoa wa Mbeya  Bwana Sambwee Shitabala ametangaza  kujiuzulu ili kupisha uchunguzi ufanyike wa madai ya kupokea mlungula wa milioni 600 ili kukihujumu chama."Nimeamua kuachia ngazi kwa hiari yangu, nimetuhumiwa kuhujumu chama. Nimeambiwa nimehongwa mamilioni ya fedha na CCM ili nikikoseshe ushindi chama changu, naachia ngazi ili uchunguzi dhidi ya tuhuma hizi ufanyike," alisema Bw. Shitambala. Aliendelea kwa kusema inaonesha chuki hii imepandwa kwa wanachama wa ngazi ya mkoa hadi Taifa nakutoatela mfano wa mwenyekiti wake Bwana Freeman Mbowe kutpokea simu yake"Inaonesha mbegu hii imepandwa na kukubalika kwa wanachama….nimempigia simu mwenyekiti wangu wa Taifa mara kadhaa lakini hapokei simu yangu, hili si jambo la kawaida, bora niachie ngazi," alisisitiza Bw. Shitambala.

Tukiachana na huyo leo hii Mwenyekiti wa baraza la wanawake Chadema Bi Leticia Ghati Mosore ametangaza kujiuzulu kwa kile anachodai kutotahaminiwa cheo chake.Akizungumza na waandishi wa habari waliofika leo katika makao makuu ya  chama cha NCCR-Mageuzi  kumsikiliza akitangaza nia yake ya kukihama chama cha CHADEMA na kujiunga na NCCR-Mageuzi kwa madai kwamba amechoshwa  na taratibu nzima za uongozi wa juu wa chama hicho na kutopewa umuhimu wa cheo chake katika shughuli mbali mbali za kichama zikiwemo za baraza la wanawake ambalo yeye ndio mwenyekiti wake.
Hivyo basi ningeomba kwa uongozi mkuu wa Chadema kujiangalia tena kabla ya kushutumu kuwa kina hujumiwa kwani badala ya kujijenga na kuwa imara kisije tokea kama yale yaliyosababisha kusambaratika kwa chama kama NCCR-Mageuzi.Hakuna adui anaefurahia adui wake kufanikiwa lakini kabla huja toka nje hebu tizama ndani kwako au wewe mwenyewe kuwa hakuna makosa yatakayopelekea adui yako kutumia mwanya huo kukusambaratisha.

 Video hapo chini inaonesha mwenyekiti wa Chadema wilaya ya Muheza alipojiunga na CCM,JE! Uongozi wa Chadema kuna nini nyuma ya pazia?.

Monday, November 22, 2010

Tarik Aziz Ahaha Kutaka Msamaha wa Rais wa Iraq


Toka shoto ni Tarik Aziz
akiwa na Saddam Hussein
wakati wa utawala wao
  
























Mawakili wa Tarik Aziz wamuomba Rais wa Iraqkumsamehe mshirika wa Saddam Hussein,aliyehukumiwa kunyongwa kwa mauaji ya mashia.

Aziz alikuwa mwakilishi wa kimataifa katika utawala wa Saddam Hussein na mkristo pekee katika baraza la mawaziri akiwa anashikilia vyeo vya waziri wa mambo ya nje na naibu waziri mkuu.

Wakili wake,Giovanni Di Stefano,amesema ana matarajio ya mteja wake kupata msamaha, kutokana na kuombewa msamaha na mataifa ya ulaya na Vatican, na pia kitendo cha rais wa Iraq Jalal Talabani kukataa kuweka sahihi ya kuruhusu kunyLakini kuna utata kama Talabani anaweza kumsamehe Aziz,kwani msamaha wa rais kwa mujibu wa katiba ya Iraq lazima kupata ridhaa ya waziri mkuu ambaye ni shia.

Chanzo: http://gulfnews.com/news/region/iraq/tarek-aziz-seeks-pardon-from-iraqi-president-1.716113

Urusi Ya Laani Bwana Bout(Merchant Of Death) Kupelekwa Amerika


Bwana Victor Bout akiwa chini ya ulinzi nchini Thailand
                                                                                        
Baraza la mawaziri la Thailand limefikia muafaka wa kumpeleka uhamishoni  nchini Amerika ,mfanyabiashara wa silaha raia wa Urusi Bwana Victor Bout  maarufu kama Merchant of Death baada ya mvutano wa kisheria wa muda mrefu wa ama kumsimamisha kujibu mashtaka  au kumuachia huru.

Bwana Victor Bout ,43  afisa wa zamani katika jeshi la anga la urusi alikamatwa Hotelini mjini Bangkok mnamo  mwezi march 2008 kwa ushirikiano wa maafisa wa usalama wa Thailand na Mawakala wa ujasusi toka Amerika.

Anashutumiwa   kusambaza silaha zilizo chochea vita ya kiraia katika nchi za kusini mwa Amerika,Mashariki ya Kati na Afrika miongoni mwa wateja wake ni Rais wa zamani wa Liberia Charles Taylor,na kiongozi wa Libya Muumar Gadhafi- na pia Angola pande zote mbili(MPLA na UNITA) .

Kitendo hicho cha uhamisho wake toka Thailand kwenda Amerika kumeibua vita ya kidiplomasia baina ya Urusi na Amerika.Wakati serikali ya Amerika imefurahia kumpata Bwana Bout ambaye yupo katika orodha ya watu hatari duniani,Urusi wamelaani kitendo hicho nakusema haki haikutendeka kwani Bwana Bout ni mtu safi.


Baada ya hilo tukio hebu angalia movie hii utajua ni hatari gani ya wafanyabiashara wa silaha wasivyojali watu maskini hasa Afrika. Angalia trailer kisha click link hapo chini uangalie full movie.

                              LORD OF WAR BY NICOLAS CAGE
           
Na hii link ni vipande vya filamu nzima:   http://www.youtube.com/watch?v=1KGu0FMDJfk&feature=related                                                                                                             

Kesi Ya Uhalifu Wa Vita Dhidi ya Bemba ni Jumatatu Hii

Kiongozi wa chama cha upinzani MLC, Jean-Pierre Bemba akipiga kura Kinshasa, DRC 2006.
 Kiongozi wa chama cha upinzani MLC, Jean-Pierre Bemba akipiga kura Kinshasa, DRC 2006.
 
"Jean-Pierre Bemba atafikishwa mahakamani Jumatatu, Novemba 22, kwa mashtaka ya uhalifu wa vita na uhalifu dhidi ya ubinadamu ulotendwa CAR kati ya 2002 na 2003." amesema bi Daphne Anayiotos
Kesi ya uhalifu wa vita dhidi ya makamu rais wa zamani wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Jean Pierre Bemba, inanaza The Hague, Uholanzi Jumatatu kufuatana na Mahkama ya Uhalifu wa Kimataifa, ICC.
Msemaji wa ICC Daphne Anayiotos, ameiambia Sauti Ya Amerika kwamba Bermba anashtakiwa kwa tuhuma za uhalifu ulotendwa na wapiganaji wake huko Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Bi Anayiotos amesema, "Jean-Pierre Bemba atafikishwa mahakamani Jumatatu, Novemba 22, kwa mashtaka ya uhalifu wa vita na uhalifu dhidi ya ubinadamu ulotendwa CAR kati ya 2002 na 2003."
Serikali ya Jamhuri ya Afrika ya Kati, iliwasilisha mashtaka hayo mbele ya ICC 2004. Wakosowaji wanashuku na mashtaka hayo wakidai kwamba Rais Ange-Felix Patasse ndiye aliyemualika Bembe kumsaidia kuzima uwasi nchini mwake.

 Chanzo:Voa  swahili

Rais wa Comoro Amtembelea JK Ikulu Leo

                        Rais Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Ikulu jijini Dar es Salaam ,
                        Rais wa Muungano wa Visiwa vya Comoro Ahmed Abdallah Mohamed
                        Sambi leo mchana.Viongozi hao wawili baadaye walifanya mazungumzo
                        (picha na Freddy Maro)

Sunday, November 21, 2010

Wafurahia Papa Kuruhusu Kondomu

Wapenda mabadiliko katika Kanisa Katoliki na makundi ya kupambana na UKIMWI yamefurahia matamshi ya Papa Benedikt kuwa matumizi ya kondomu sio mara zote ni ya nia mbaya.
Papa
Ruksa... Ingawa katika mazingira fulani tu.

Papa amesema matumizi ya mipira hiyo ya kiume inaweza kuhalalishwa kutokana na hali ilivyo, ili kuzuia kusambaa kwa maambukizi ya virusi vya HIV/UKIMWI.
Matamshi hayo yanayotarajiwa kuchapishwa katika kitabu wiki ijayo, yanaashiria kulegeza msimamo wake mkali wa zamani dhidi ya matumizi wa kondomu kupambana na HIV.
Vatikana kwa muda mrefu imekuwa ikipinga matumizi ya kondomu, kama njia ya kupanga uzazi.
Condom
Wanaharakati wamefurahishwa na uamuzi wa Papa

Hatua hiyo ilizua shutuma kali, hasa kutoka kwa wanaharakati wa kupambana na UKIMWI, ambao wanasema kondomu ni moja ya njia ambazo zimethibitishwa katika kupambana na maambukizi ya HIV.
Papa Benedikt katika ziara yake nchini Cameroon mwaka jana alisema kugawa kondomu kunaweza kuchochea maambukizi ya HIV, matamshi ambayo yalizua shutuma kutoka kwa nchi kadhaa za Umoja wa Ulaya.
Hata hivyo, katika matamshi yake ya hivi karibuni, amesema matumizi wa kondomu yanaweza kuhalalishwa katika mazingira fulani ya kipekee.
Ametoa mfano wa makahaba wa kiume, ambapo amesema matumizi wa kondomu kuzuia maambukizi ya UKIMWI yanaweza kuonekana kama kitendo cha mtu kuwa na majumuku, ingawa amesema kondomu "sio njia halisi ya kupambana na uovu wa kuambukiwa HIV".

Chanzo: BBC

50 Cent anakuja na kali"Things Fall Apart"

Sanaa ni kazi hasa pale unapotakiwa kuivaa tabia halisi ya kile unachoigiza, na kazi kubwa ni kuwa tayari kwa gharama yoyote hata iwe kujibadilisha muonekano na hadhi yako.
                              
Mathalani tumeshuhudia mara nyingi kwa kuona waigizaji kama Will Smith alivyofanikiwa kuigiza kama Mohamed Ali na Beyonce kupunguza uzito kwa pauni 20 kwa siku 10.
Lakini wote hao tisa, kumi ni curtis"50 cent" Jackson mwenye uzito wa pauni 214 alipojipunguza kwa pauni 54 ili kufikia lengo la pauni 160 kwa ajili ya filamu yake mpya "Things Fall Apart". Kwa muda wa wiki 9 amekuwa katika mlo maalumu ili kuuvaa uhalisi wa mchezaji wa American Football ambaye aliugua ugonjwa wa kansa.

Hebu angalia picha alizotoa wakati akiitangaza filamu hiyo mpya, kisha ujiulize kama itawezekana kwa msanii wa bongo kuweza kuigiza mathalani hata sehemu ya harakati za Mwalimu Nyerere.
                                                                                 
                                                                                            50_cent_things_fall_apart_skinny_02

50_cent_things_fall_apart_skinny_01


  50_cent_buff                      

Katika picha ya kwanza na ya pili ndivyo atakavyoonekana katika filamu hiyo.
Na picha ya tatu jinsi 50 cent akiwa katika muonekano halisi.
Kazi kwenu wasanii, ujumbe umefika  .                    
                                                  
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...