Mtazamohalisi

Friday, November 5, 2010

Hongera Rais Jakaya M.Kikwete na Dk.Ali Shein


                               Dk Jakaya Kikwete Pichani akipongezana na Dk Ali Mohamed Shein.

Katik hafla ya kutangaza matokeo ya Urais iliyomalizika hivi karibuni kwenye ukumbi wa Karimjee Jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC Jaji Lewis Makame, ameweza kutoa majumuisho ya matokeo hayo na kutangaza rasmi kuwa Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, aliyekuwa mgombea urais kupitia chama cha Mapinduzi CCM, ameibuka mshindi kwa kupata Asilimia 67.17 na n ameteuliwa kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kipindi cha miaka mitano. Makame alisema kuwa Rais Kikwete ameibuka mshindi baada ya kupata jumla ya kura Milioni 5, 276, 827 ambayo ni sawa na asilimia 61.17 % ya watu wote waliopiga kura, na kufuatiwa na mpinzani wake Dk Willbroad Slaa kupitia chama cha CHADEMA, ambaye ameibuka na jumla ya kura Mil.2, 271, 941 ambayo ni sawa na asilimia 20% ya wapiga kura. Ambapo jumla ya watu waliojiandikisha kupiga kura ilikuwa ni Milioni 20, 137, 303, wakati walijitokeza kupiga kura walikuwa ni Milioni 8, 6261.283 ambayo ni 42% ya waliopiga kura.
Tunategemea toka kwenu kupunguza changamoto zinazolikabili taifa kama vile Umaskini,Ujinga na Maradhi bila kusahau Ufisadi.Usafiri wetu ni ule ule, ila aina ya gari hubadilika kutokana na mazingira na hali ya barabara.

No comments:

Post a Comment

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...