Mara nyingi,umuhimu wa vyeti vya kuzaliwa hauji mpaka kuwe na jambo la kisheria linalokukabili. Kutokana na umuhimu wake ni vyema wazazi na vijana mliofikia umri wa kujitegemea kuanza kulifikiria, kwani athari yake unaweza kupoteza haki zako za msingi kama raia na hata kutiliwa shaka uraia wako.
Naandika haya kwa ushahidi mkubwa wa mambo yalivyojitokeza nyuma hasa ukiwa unakumbuka kunyang'anywa uraia wa Jenerali Twaha Ulimwengu na Marehemu Ali Nabwa.
Kuhifadhi cheti cha kuzaliwa ni muhimu kwani ushahidi wake unatambulika kisheria,kumbuka wakati wa mchakato wa kutafuta wagombea wa ubunge wa CCM kulijitokeza mgogoro baada ya Mgombea toka Nzega kukataliwa na chama chake kwa madai ya kutokuwa raia.
Hussein Bashe ilimlazimu si tu kumuhatarisha uanachama wake katika CCM bali kubwa kuliko yote ni haki nzima ya uraia kama Mtanzania, kwa kuwa alithibitisha uraia wake wa kuzaliwa kwa kigezo hicho Idara ya Uhamiaji ilijiridhisha kuwa ni raia halali.
Leo hii,licha ya uthibitisho wa kuzaliwa ,masomo na nyadhifa mbali mbali alizopitia Marekani, Rais Barack Obama wapo watu wanaodai kutaka uthibitisho wake wa kuzaliwa huko Honolulu,Hawaii.
Picha inayonijia ni kuwa kuhifadhi vyeti vya kuzaliwa ni muhimu kwa ajili kupata haki zako za msingi za kisheria kama raia.
Ijapokuwa Obama na familia yake wapo Hawaii ambako ina aminika ndiko alikozaliwa katika mapumziko ya Krismasi,lakini swali la uhalali wa cheti cha kuzaliwa kwake huko Honolulu ,Hawaii bado ni tete.
Mtazamohalisi
Thursday, December 23, 2010
Umuhimu wa Vyeti Vya Kuzaliwa
Benitez apigwa chini Inter
Inter Milan ya Italia imethibitisha kuwa imemfukuza kazi meneja Rafael Benitez, miezi sita tu baada ya kuteuliwa kuiongoza klabu hiyo.
Hatua hiyo imekuja baada ya Benitez kutaka kuungwa mkono ndani ya bodi ya wakurugenzi kununua wachezaji, kufuatia klabu hiyo kushinda kombe la dunia la vilabu, kwa kuifunga TP Mazembe siku ya Jumamosi.
Badala yake, Inter, ambayo inasuasua katika nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi ya Serie A, imeamua kumfukuza kazi Benitez.

'Jino la pembe' Moratti na Benitez
Benitez alichukua kazi hiyo San Siro kutoka kwa Jose Mourinho.
Mourinho, ambaye aliondoka Inter na kwenda Real Madrid ya Uhispania, aliiongoza timu hiyo kuchukua ubingwa wa ligi ya Italia na klabu bingwa Ulaya msimu uliopita na kumuachia Benitez kazi ngumu ya kufuata nyayo zake.
Benitez, alichukua majukumu ya San Siro wiki moja baada ya kuondoka Liverpool ya England Juni 3. Ingawa amekuwa na majeruhi kadhaa, lakini imeonekana kuwa mbinu zake hazijaweza kumsaidia.
Ingawa Inter ina kiporo cha mechi mbili dhidi ya timu zilizo juu yake, imeshinda mechi sita tu kati ya mechi 15 za ligi.
katika kutetea ubingwa wao wa klabu bingwa, Inter imeweza kumaliza katika nafasi ya pili ya makundi, nyuma ya Tottenham ya England, na kuiacha katika wakati mgumu kwani itapambana na Bayern Munich katika raundi ya timu 16.
Ingawa Inter imeshinda Kombe la Dunia la Vilabu kwa kuichapa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, mafaniko hayo hayakumfanya Benitez kutotoa dukuduku lake baada ya mchezo huo wa fainali
Soma zaidi.....BBC
Hatua hiyo imekuja baada ya Benitez kutaka kuungwa mkono ndani ya bodi ya wakurugenzi kununua wachezaji, kufuatia klabu hiyo kushinda kombe la dunia la vilabu, kwa kuifunga TP Mazembe siku ya Jumamosi.
Badala yake, Inter, ambayo inasuasua katika nafasi ya saba kwenye msimamo wa ligi ya Serie A, imeamua kumfukuza kazi Benitez.
'Jino la pembe' Moratti na Benitez
Benitez alichukua kazi hiyo San Siro kutoka kwa Jose Mourinho.
Mourinho, ambaye aliondoka Inter na kwenda Real Madrid ya Uhispania, aliiongoza timu hiyo kuchukua ubingwa wa ligi ya Italia na klabu bingwa Ulaya msimu uliopita na kumuachia Benitez kazi ngumu ya kufuata nyayo zake.
Benitez, alichukua majukumu ya San Siro wiki moja baada ya kuondoka Liverpool ya England Juni 3. Ingawa amekuwa na majeruhi kadhaa, lakini imeonekana kuwa mbinu zake hazijaweza kumsaidia.
Ingawa Inter ina kiporo cha mechi mbili dhidi ya timu zilizo juu yake, imeshinda mechi sita tu kati ya mechi 15 za ligi.
katika kutetea ubingwa wao wa klabu bingwa, Inter imeweza kumaliza katika nafasi ya pili ya makundi, nyuma ya Tottenham ya England, na kuiacha katika wakati mgumu kwani itapambana na Bayern Munich katika raundi ya timu 16.
Ingawa Inter imeshinda Kombe la Dunia la Vilabu kwa kuichapa TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, mafaniko hayo hayakumfanya Benitez kutotoa dukuduku lake baada ya mchezo huo wa fainali
Soma zaidi.....BBC
Wednesday, December 22, 2010
Nundu Aitaka Mamlaka Ya Usimamizi wa Bandari Kufanya kazi Kiufanisi
SERIKALI imeiagiza Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), kwa kushirikiana na Kamati ya Kuboresha huduma bandarini kuhakikisha kwamba kuanzia sasa muda wa uondoshaji wa kontena katika Bandari ya Dar es Salaam unapungua ili TPA iendelee na jukumu lake la kuboresha huduma hiyo na kuleta ufanisi zaidi.
Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu ameitaka TPA kuanza mara moja kujenga na kuimarisha miundombinu ya bandari kwa kuzingatia mpango mkuu wa Mamlaka na kwamba mpango huo ni dira ya kuendeleza na hatimaye kufikiwa kwa lengo la nchi la kuifungua kibiashara ndani na nje ya nchi.
Nundu aliyasema hayo jana Dar es Salaam katika majumuisho ya ziara yake ya siku mbili ya kutembelea TPA ili kuona na kujifunza mambo muhimu ya uendeshaji na uendelezaji wa Bandari ya Dar es Salaam.
Akiongozana na Naibu wake, Dk. Athuman Mfutakamba, Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ephraim Mgawe na viongozi wengine wa bandari, Waziri Nundu alipata pia fursa ya kutembelea baadhi ya kampuni za kuhifadhi mizigo ya bandarini kwa lengo la kufahamu changamoto mbalimbali zinazoikabili mamlaka hiyo.
Alisema wakati ujenzi wa bandari ya Mwambani, Tanga ukiendelea, TPA inununue vifaa vitakavyoongeza ufanisi wa matumizi ya bandari hiyo na kusisitiza shirika lianze mawasiliano na uongozi wa Tanga ili maeneo ya ndani na nje ya bandari yanayotumika kwa shughuli zisizo za kibandari, zichukuliwe na kumilikishwa TPA.
Aidha, alisema mchakato wa kufanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina eneo la Kisarawe kwa ajili ya matumizi ya kuhifadhi mizigo, ufanyike mara moja hata kama ni kwa gharama za serikali na kuongeza kuwa ni vyema hilo likafanyika kabla ya mwaka wa fedha 2011/11 haujamalizika.
Alisisitiza wafanyakazi wa TPA kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma na matakwa ya wateja, na kuwa mawasiliano kati ya mamlaka na wateja yawe ya haraka na yenye tija.
Chanzo: Habari Leo
Waziri wa Uchukuzi, Omar Nundu ameitaka TPA kuanza mara moja kujenga na kuimarisha miundombinu ya bandari kwa kuzingatia mpango mkuu wa Mamlaka na kwamba mpango huo ni dira ya kuendeleza na hatimaye kufikiwa kwa lengo la nchi la kuifungua kibiashara ndani na nje ya nchi.
Nundu aliyasema hayo jana Dar es Salaam katika majumuisho ya ziara yake ya siku mbili ya kutembelea TPA ili kuona na kujifunza mambo muhimu ya uendeshaji na uendelezaji wa Bandari ya Dar es Salaam.
Akiongozana na Naibu wake, Dk. Athuman Mfutakamba, Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Ephraim Mgawe na viongozi wengine wa bandari, Waziri Nundu alipata pia fursa ya kutembelea baadhi ya kampuni za kuhifadhi mizigo ya bandarini kwa lengo la kufahamu changamoto mbalimbali zinazoikabili mamlaka hiyo.
Alisema wakati ujenzi wa bandari ya Mwambani, Tanga ukiendelea, TPA inununue vifaa vitakavyoongeza ufanisi wa matumizi ya bandari hiyo na kusisitiza shirika lianze mawasiliano na uongozi wa Tanga ili maeneo ya ndani na nje ya bandari yanayotumika kwa shughuli zisizo za kibandari, zichukuliwe na kumilikishwa TPA.
Aidha, alisema mchakato wa kufanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina eneo la Kisarawe kwa ajili ya matumizi ya kuhifadhi mizigo, ufanyike mara moja hata kama ni kwa gharama za serikali na kuongeza kuwa ni vyema hilo likafanyika kabla ya mwaka wa fedha 2011/11 haujamalizika.
Alisisitiza wafanyakazi wa TPA kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia maadili ya utumishi wa umma na matakwa ya wateja, na kuwa mawasiliano kati ya mamlaka na wateja yawe ya haraka na yenye tija.
Chanzo: Habari Leo
Tuesday, December 21, 2010
Kulikoni India?
Katika Miezi 6 wanachama wa baraza la usalama la UN wametembelea India
Yaahidiwa kiti cha Uanachama wa baraza la usalama la UN
Yaweka mikataba lukuki ya kibiashara,kijeshi,nishati ya nyuklia na mafuta
Made in .............India
Sikiliza kibao hiki

Made In India
Upload Music
Cameron akiwa India-July 28,2010

Obama akiwa India- Nov 8,2010

Sarkozy(Rais wa Ufaransa)-Dec 6,2010

Wen Jiabao(Waziri Mkuu wa China)-Dec 16,2010

Medvedev(Rais wa Urusi)-Dec 21,2010
Yaahidiwa kiti cha Uanachama wa baraza la usalama la UN
Yaweka mikataba lukuki ya kibiashara,kijeshi,nishati ya nyuklia na mafuta
Made in .............India
Sikiliza kibao hiki
Made In India
Upload Music
Cameron akiwa India-July 28,2010
Obama akiwa India- Nov 8,2010
Sarkozy(Rais wa Ufaransa)-Dec 6,2010
Wen Jiabao(Waziri Mkuu wa China)-Dec 16,2010
Medvedev(Rais wa Urusi)-Dec 21,2010
Hoseah amlipua Kikwete
Asema anaogopa kushughulikia ufisadi wa vigogo
MTANDAO wa Wikileaks wa Marekani umeibua siri nzito kuhusu uwezo na nia ya Rais Jakaya Kikwete katika kushughulikia ufisadi, ukidai kuwa ndiye anayekwamisha kushtakiwa kwa baadhi ya vigogo serikalini wanaotuhumiwa kuhusika katika rushwa kubwa nchini.
Katika taarifa hiyo iliyochapishwa jana na gazeti la The Guardian la Uingereza, likinuu taarifa za kibalozi za Marekani zilizoanikwa na Wikileaks, lilisema Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea, alimweleza mwanadiplomasia mmoja wa Kimarekani kwamba ugumu wa kupambana na ufisadi Tanzania unaanzia Ikulu.
Mtandao huo ulinukuu baadhi ya maelezo ya faragha kuhusu rushwa aliyoyatoa Dk. Hosea kwa mwanadiplomasia wa Kimarekani aitwaye Purnell Delly, walipokutana mwezi Julai mwaka 2007, Dar es Salaam.
Likinukuu mtandao huo, The Guardian liliandika, “Dk. Hosea alidokeza kuwa Rais Kikwete hafurahishwi na sheria kuchukua mkondo wake dhidi ya ufisadi ambao unaweza kuwatia hatiani vigogo wa ngazi za juu serikalini…. Hataki kuweka msingi wa kumwandama kiongozi yeyote miongoni mwa watangulizi wake (wastaafu).”
Linasema mwanadiplomasia huyo alisema: “Hosea alikuwa akisisitiza kwamba akiamua kuwa na makali, usalama wake binafsi utakuwa hatarini…anadai anaamini maisha yake yako hatarini, kwani amekuwa akipokea ujumbe wa vitisho kwa simu na barua na amekuwa akikumbushwa kila siku kwamba anapambana na ‘watu matajiri na wenye nguvu.’”
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Dk. Hosea alitoa maelezo yanayokatisha tamaa juu ya mustakabali wa mapambano dhidi ya ufisadi nchini na ugumu uliopo katika kuwashtaki watuhumiwa wa ufisadi mkubwa.
“Alituambia bila kufafanua... kwamba kesi zinazomhusu waziri mkuu au rais haziwezi kujadiliwa kabisa,” kilisema chombo hicho na kisha kufafanua: “Rais Kikwete hataki kumshughulikia mtangulizi wake yeyote mwenye tuhuma zinazostahili kufikishwa mahakamani.”
Dk. Hoseah anadaiwa kumueleza mwanadiplomasia huyo jinsi rushwa ilivyokithiri katika Benki Kuu ya Tanzania na visiwani Zanzibar, lakini akadokeza ugumu wa kuishughulikia kwa sababu tu wahusika wakuu ni watu ambao “hawahusiki”.
Hoseah alidokeza kuwa mambo yakiwa mabaya angeweza hata kukimbia nchi, kwa mujibu wa taarifa hiyo ikimnukuu mwanadiplomasia huyo wa Marekani.
“Ukihudhuria kwenye vikao vya juu (vya ndani), watu wanataka ujisikie kuwa wao ndio wamekuweka hapo ulipo. Wakiona huenendi na yale wanayotaka wao, basi hapo unakuwa katika hatari,” ilisema sehemu nyingine ya taarifa hiyo ikinukuu maelezo ya Dk. Hoseah.
Aidha, katika mazungumzo yao, Dk. Hoseah alimpa matumaini mwanadiplomasia huyo kwamba TAKUKURU ingeweza kuwachukulia hatua za kisheria watuhumiwa wote waliohusika katika kile alichokiita ‘dili chafu’ ya rushwa katika ununuzi wa rada ya kijeshi kutoka kampuni ya BAE ya Uingereza, hatua ambayo hata hivyo ilionekana isingeweza kutekelezwa na taasisi hiyo.
Wachambuzi wa mambo wanasema kauli hiyo ya Dk. Hoseah ilitokana na ukweli kwamba tayari wapelelezi wa Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa ya Jinai ya Uingereza (SFO) walikuwa wameshampelekea faili lote la watuhumiwa likiwa na ushahidi jambo ambalo lingeweza kumuepusha na hatari ambayo ingeweza kumfika kama uchunguzi huo ungefanywa na TAKUKURU yake.
Katika kashfa hiyo, serikali ya Tanzania inadaiwa kununua rada ya kuongozea ndege za kiraia na za kivita kutoka kampuni ya BAE System ya Uingereza kwa gharama kubwa ya dola 40 milioni, huku taarifa za uchunguzi kutoka SFO na vyanzo mbalimbali zikionyesha kuwa ununuzi huo haukuwa wa lazima na uligubikwa na rushwa.
Kashfa ya rada ilitendeka mwaka 1999, katika mazingira yaliyogubikwa na rushwa kwa watendaji serikalini ili waweze kulainisha watoa maamuzi. Kwa mujibu wa taarifa za maelezo ya Dk. Hoseah kwa mwanadiplomasia huyo, watuhumiwa zaidi wa rushwa ya rada wapo katika Wizara ya Ulinzi na jeshini.
“Dk. Hoseah aliliita suala la rada kuwa ni dili chafu na kusema inawahusu maofisa wa Wizara ya Ulinzi na vigogo wawili au mmoja wa jeshi (hawakutajwa majina),” ilieleza taarifa hiyo.
Kesi ya rada iliendelea kusikilizwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi jijini London, Uingereza .
Chanzo: Tanzania Daima
MTANDAO wa Wikileaks wa Marekani umeibua siri nzito kuhusu uwezo na nia ya Rais Jakaya Kikwete katika kushughulikia ufisadi, ukidai kuwa ndiye anayekwamisha kushtakiwa kwa baadhi ya vigogo serikalini wanaotuhumiwa kuhusika katika rushwa kubwa nchini.
Katika taarifa hiyo iliyochapishwa jana na gazeti la The Guardian la Uingereza, likinuu taarifa za kibalozi za Marekani zilizoanikwa na Wikileaks, lilisema Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Dk. Edward Hosea, alimweleza mwanadiplomasia mmoja wa Kimarekani kwamba ugumu wa kupambana na ufisadi Tanzania unaanzia Ikulu.
Mtandao huo ulinukuu baadhi ya maelezo ya faragha kuhusu rushwa aliyoyatoa Dk. Hosea kwa mwanadiplomasia wa Kimarekani aitwaye Purnell Delly, walipokutana mwezi Julai mwaka 2007, Dar es Salaam.
Likinukuu mtandao huo, The Guardian liliandika, “Dk. Hosea alidokeza kuwa Rais Kikwete hafurahishwi na sheria kuchukua mkondo wake dhidi ya ufisadi ambao unaweza kuwatia hatiani vigogo wa ngazi za juu serikalini…. Hataki kuweka msingi wa kumwandama kiongozi yeyote miongoni mwa watangulizi wake (wastaafu).”
Linasema mwanadiplomasia huyo alisema: “Hosea alikuwa akisisitiza kwamba akiamua kuwa na makali, usalama wake binafsi utakuwa hatarini…anadai anaamini maisha yake yako hatarini, kwani amekuwa akipokea ujumbe wa vitisho kwa simu na barua na amekuwa akikumbushwa kila siku kwamba anapambana na ‘watu matajiri na wenye nguvu.’”
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Dk. Hosea alitoa maelezo yanayokatisha tamaa juu ya mustakabali wa mapambano dhidi ya ufisadi nchini na ugumu uliopo katika kuwashtaki watuhumiwa wa ufisadi mkubwa.
“Alituambia bila kufafanua... kwamba kesi zinazomhusu waziri mkuu au rais haziwezi kujadiliwa kabisa,” kilisema chombo hicho na kisha kufafanua: “Rais Kikwete hataki kumshughulikia mtangulizi wake yeyote mwenye tuhuma zinazostahili kufikishwa mahakamani.”
Dk. Hoseah anadaiwa kumueleza mwanadiplomasia huyo jinsi rushwa ilivyokithiri katika Benki Kuu ya Tanzania na visiwani Zanzibar, lakini akadokeza ugumu wa kuishughulikia kwa sababu tu wahusika wakuu ni watu ambao “hawahusiki”.
Hoseah alidokeza kuwa mambo yakiwa mabaya angeweza hata kukimbia nchi, kwa mujibu wa taarifa hiyo ikimnukuu mwanadiplomasia huyo wa Marekani.
“Ukihudhuria kwenye vikao vya juu (vya ndani), watu wanataka ujisikie kuwa wao ndio wamekuweka hapo ulipo. Wakiona huenendi na yale wanayotaka wao, basi hapo unakuwa katika hatari,” ilisema sehemu nyingine ya taarifa hiyo ikinukuu maelezo ya Dk. Hoseah.
Aidha, katika mazungumzo yao, Dk. Hoseah alimpa matumaini mwanadiplomasia huyo kwamba TAKUKURU ingeweza kuwachukulia hatua za kisheria watuhumiwa wote waliohusika katika kile alichokiita ‘dili chafu’ ya rushwa katika ununuzi wa rada ya kijeshi kutoka kampuni ya BAE ya Uingereza, hatua ambayo hata hivyo ilionekana isingeweza kutekelezwa na taasisi hiyo.
Wachambuzi wa mambo wanasema kauli hiyo ya Dk. Hoseah ilitokana na ukweli kwamba tayari wapelelezi wa Taasisi ya Uchunguzi wa Makosa ya Jinai ya Uingereza (SFO) walikuwa wameshampelekea faili lote la watuhumiwa likiwa na ushahidi jambo ambalo lingeweza kumuepusha na hatari ambayo ingeweza kumfika kama uchunguzi huo ungefanywa na TAKUKURU yake.
Katika kashfa hiyo, serikali ya Tanzania inadaiwa kununua rada ya kuongozea ndege za kiraia na za kivita kutoka kampuni ya BAE System ya Uingereza kwa gharama kubwa ya dola 40 milioni, huku taarifa za uchunguzi kutoka SFO na vyanzo mbalimbali zikionyesha kuwa ununuzi huo haukuwa wa lazima na uligubikwa na rushwa.
Kashfa ya rada ilitendeka mwaka 1999, katika mazingira yaliyogubikwa na rushwa kwa watendaji serikalini ili waweze kulainisha watoa maamuzi. Kwa mujibu wa taarifa za maelezo ya Dk. Hoseah kwa mwanadiplomasia huyo, watuhumiwa zaidi wa rushwa ya rada wapo katika Wizara ya Ulinzi na jeshini.
“Dk. Hoseah aliliita suala la rada kuwa ni dili chafu na kusema inawahusu maofisa wa Wizara ya Ulinzi na vigogo wawili au mmoja wa jeshi (hawakutajwa majina),” ilieleza taarifa hiyo.
Kesi ya rada iliendelea kusikilizwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi jijini London, Uingereza .
Chanzo: Tanzania Daima
Rais Kibaki aahidi kuwalinda Wakenya baada ya watu 3 kuuwawa kwenye mlipuko Nairobi
Rais wa Kenya,MwaiKibaki
Rais wa Kenya, Mwai Kibaki amesema usalama utaimarishwa msimu huu wa sikukuu ya Krisamasi kufuatia mlipuko wa bomu lililotokea jana mjini Nairobi.
Kamishna wa polisi nchini Kenya, Mathew Iteere, amesema uchunguzi umeanza kubaini kama mlipuko uliowaua watu 3 na kuwajeruhi wengine wapatao 40 mjini Nairobi jana jioni, ni shambulio la kigaidi.
Mlipuko huo uliotokea kwenye basi moja la kuelekea Kampala, Uganda. Kamishna Iteere, hakuuleza mlipuko huo kuwa shambulio la kigaidi, lakini amesema umesababishwa na kifaa cha kulipuka kilichokuwa sehemu ya mzigo wa abiria. Bwana Iteere pia amesema uchunguzi umeanza kubaini waliohusika kufanya hujuma hiyo.
Chanzo: Dw
Monday, December 20, 2010
Sitta: Nilitemwa uspika kwa hila za vigogo
Wastaafu wakibadilishana mawazo ya uongozi

Toka shoto Waziri mkuu mstaafu Edward Lowasa
na kulia ni Spika Mstaafu Samuel Sitta.
WAZIRI wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta jana alitoa kauli nyingine inayoweza kukitikisa chama chake cha CCM baada ya kueleza kuwa aliondolewa kwenye kinyang'anyiro cha kiti cha spika wa Bunge la Muungano kutokana na hila za viongozi ambao walishindwa kuhimili kasi ya utendaji wake kwenye chombo hicho cha kutunga sheria.
Sitta, ambaye alipata umaarufu baada ya kuliongoza Bunge la Tisa kwa mafanikio, ametoa kauli hiyo wiki chache baada ya kukaririwa na vyombo vya habari akisema bayana kuwa kuilipa kampuni tata ya Dowans fidia iliyoamuliwa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Kibiashara (ICC) ni sawa na kuhujumu uchumi.
Mbunge huyo wa Urambo Mashariki alijikuta akianguka kwenye kinyang'anyiro cha uspika wa Bunge la Kumi baada ya chama chake cha CCM kuamua kuwapa wanawake nafasi ya kuongoza moja ya mihimili ya nchi na hivyo kupitisha wagombea watatu wanawake katika mchakato uliompa ushindi Anne Makinda.
Jana, Sitta ambaye alikuwa akihojiwa na Mwananchi, alisema utendaji wake wa kasi na viwango uliwatisha viongozi wengi wa serikali na ndio maana wakaamua kutumia kigezo cha jinsia kumwondoa.
"Unajua nataka hili ilieleweke; juzi nilienda jimboni kwangu Urambo Mashariki nikawaeleza wapiga kura wangu kwa nini sasa mimi sio spika tena, maana wanaweza kudanganywa kama kazi imenishinda au nimefukuzwa," alisema Sitta.
"Watanzania lazima wajue mimi sijafukuzwa kazi wala sijashindwa kufanya kazi hiyo, ila kuna viongozi ambao ni wakuu wangu ndani ya chama chetu ambao wameshindwa kuendana na kasi na viwango vyangu ndio maana wakaamua kuweka sharti ambalo kamwe nisingeweza kulitimiza.
"Kigezo hicho cha jinsia walikileta katika hatua za mwisho za mchakato wa kumtafuta spika wakijua kwamba sitaweza kukitimiza na ningejua hilo mapema, nisingepeleka jina langu kuomba kuteuliwa tena."
Sitta alisema ni wazi kamba asingeweza kutimiza sharti kwamba spika aliyetakiwa safari hii ni mwanamke ndio maana hakuweza kuteuliwa tena kuwania nafsi hiyo.
"Mimi ni Sitta na nitabaki kuwa Sitita yule yule kama nilivyozaliwa na kwa vyovyote vile; nisingeweza kufanya chochote ili kuhakikisha sharti hilo nalitimiza," alisema Sitta.
Hata hivyo Sitta alisema kuwa endapo jina lake lingepitishwa, alikuwa na ukakika wa kurudi katika kiti hicho kwa kuwa asilimia kubwa ya wabunge walikuwa wameukubali utendaji wake.
Katika miaka ya mwisho ya uongozi wake wa Bunge la Tisa, Sitta alikuwa akilalamikia kuwepo kwa njama alizodai zinafanywa na mafisadi kutaka kumuangusha kwenye ubunge na wakati fulani alifikia hadi kuomba ulinzi zaidi kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda akisema anatishiwa maisha.
Sitta hajawahi kuwataka hadharani wapinazani wake, lakini baadhi ya vyombo vya habari viliwahi kumuhusisha na vita vya uwaziri mkuu, lakini akakanusha vikali akisema kama angetaka nafasi hiyo asingegombea uspika.
Sitta aliwataka wapigakura wake na Watanzania kwa ujumla kutosikitishwa na kitendo cha kuenguliwa kwenye kinyang'anyiro cha uspika, akisema kuwa anaamini bado Rais Jakaya Kikwete anawapenda watu wa Urambo na kuendelea kuwaheshimu ndio maana amemteua kushika dhamana nyingine.
"Nawaahidi Watanzania huu sio mwisho wa utendaji wangu wa kazi sasa kasi na viwango navihamishia katika Wizara hii muhimu na kwamba wananchi wasiogope tena Tanzania kuingia katika Shirikisho la Afrika Mashariki,"alisema.
Alisema akiwa Waziri wa Afrika Mashariki atahakikisha Watanzania wanafaidika na shirikisho hilo na kwamba suala la ardhi halitakuwepo kwa kuwa tahadhari zote zimechukuliwa.
Sitta alifanya ziara kwenye jimbo lake la Urambo Mashariki ambako pamoja na mambo mengine, alihudhuria mkutano wa uchaguzi wa mwenyekiti wa halmshauri ya Urambo.
Katika mkutano huo, Alhaji Adam Malunkwi wa CCM alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa halmashauri hiyo.
Kabla ya mkutano huo, Sitta, ambaye alipokewa na wapigakura wake kwa msafara wa pikipiki zaidi ya 70, magari zaidi ya 40 na vikundi mbalimbali vya hamasa, alitumia fursa hiyo kuwaeleza wapigakura hao kilichomfanya ashindwe kutetea nafasi yake ya uspika.
Sitta pia alitoa msaada wa mashine ya kusaga na kukoboa nafaka kwa kikundi cha kinamama wa Uyogo kutekeleza ahadi yake kabla ya uchaguzi mkuu
Alisema mashine hiyo itakuwa kitega uchumi chao kwa kile anachoamini kuwa ukimwezesha mama, umeiwezesha jamii.
Mbali na mashine hiyo Sitta pia alitoa msaada wa mashine ya umeme wa sola kwa ajili ya zahanati ya Uyogo.
Akikabidhi msaada huo alisema kabla ya umeme haujasambaa maeneo hayo, atahakikisha zahanati zote zinapata umeme huo kurahisisha huduma zake kwa jamii.
Chanzo: Mwananchi
Toka shoto Waziri mkuu mstaafu Edward Lowasa
na kulia ni Spika Mstaafu Samuel Sitta.
WAZIRI wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta jana alitoa kauli nyingine inayoweza kukitikisa chama chake cha CCM baada ya kueleza kuwa aliondolewa kwenye kinyang'anyiro cha kiti cha spika wa Bunge la Muungano kutokana na hila za viongozi ambao walishindwa kuhimili kasi ya utendaji wake kwenye chombo hicho cha kutunga sheria.
Sitta, ambaye alipata umaarufu baada ya kuliongoza Bunge la Tisa kwa mafanikio, ametoa kauli hiyo wiki chache baada ya kukaririwa na vyombo vya habari akisema bayana kuwa kuilipa kampuni tata ya Dowans fidia iliyoamuliwa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Kibiashara (ICC) ni sawa na kuhujumu uchumi.
Mbunge huyo wa Urambo Mashariki alijikuta akianguka kwenye kinyang'anyiro cha uspika wa Bunge la Kumi baada ya chama chake cha CCM kuamua kuwapa wanawake nafasi ya kuongoza moja ya mihimili ya nchi na hivyo kupitisha wagombea watatu wanawake katika mchakato uliompa ushindi Anne Makinda.
Jana, Sitta ambaye alikuwa akihojiwa na Mwananchi, alisema utendaji wake wa kasi na viwango uliwatisha viongozi wengi wa serikali na ndio maana wakaamua kutumia kigezo cha jinsia kumwondoa.
"Unajua nataka hili ilieleweke; juzi nilienda jimboni kwangu Urambo Mashariki nikawaeleza wapiga kura wangu kwa nini sasa mimi sio spika tena, maana wanaweza kudanganywa kama kazi imenishinda au nimefukuzwa," alisema Sitta.
"Watanzania lazima wajue mimi sijafukuzwa kazi wala sijashindwa kufanya kazi hiyo, ila kuna viongozi ambao ni wakuu wangu ndani ya chama chetu ambao wameshindwa kuendana na kasi na viwango vyangu ndio maana wakaamua kuweka sharti ambalo kamwe nisingeweza kulitimiza.
"Kigezo hicho cha jinsia walikileta katika hatua za mwisho za mchakato wa kumtafuta spika wakijua kwamba sitaweza kukitimiza na ningejua hilo mapema, nisingepeleka jina langu kuomba kuteuliwa tena."
Sitta alisema ni wazi kamba asingeweza kutimiza sharti kwamba spika aliyetakiwa safari hii ni mwanamke ndio maana hakuweza kuteuliwa tena kuwania nafsi hiyo.
"Mimi ni Sitta na nitabaki kuwa Sitita yule yule kama nilivyozaliwa na kwa vyovyote vile; nisingeweza kufanya chochote ili kuhakikisha sharti hilo nalitimiza," alisema Sitta.
Hata hivyo Sitta alisema kuwa endapo jina lake lingepitishwa, alikuwa na ukakika wa kurudi katika kiti hicho kwa kuwa asilimia kubwa ya wabunge walikuwa wameukubali utendaji wake.
Katika miaka ya mwisho ya uongozi wake wa Bunge la Tisa, Sitta alikuwa akilalamikia kuwepo kwa njama alizodai zinafanywa na mafisadi kutaka kumuangusha kwenye ubunge na wakati fulani alifikia hadi kuomba ulinzi zaidi kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda akisema anatishiwa maisha.
Sitta hajawahi kuwataka hadharani wapinazani wake, lakini baadhi ya vyombo vya habari viliwahi kumuhusisha na vita vya uwaziri mkuu, lakini akakanusha vikali akisema kama angetaka nafasi hiyo asingegombea uspika.
Sitta aliwataka wapigakura wake na Watanzania kwa ujumla kutosikitishwa na kitendo cha kuenguliwa kwenye kinyang'anyiro cha uspika, akisema kuwa anaamini bado Rais Jakaya Kikwete anawapenda watu wa Urambo na kuendelea kuwaheshimu ndio maana amemteua kushika dhamana nyingine.
"Nawaahidi Watanzania huu sio mwisho wa utendaji wangu wa kazi sasa kasi na viwango navihamishia katika Wizara hii muhimu na kwamba wananchi wasiogope tena Tanzania kuingia katika Shirikisho la Afrika Mashariki,"alisema.
Alisema akiwa Waziri wa Afrika Mashariki atahakikisha Watanzania wanafaidika na shirikisho hilo na kwamba suala la ardhi halitakuwepo kwa kuwa tahadhari zote zimechukuliwa.
Sitta alifanya ziara kwenye jimbo lake la Urambo Mashariki ambako pamoja na mambo mengine, alihudhuria mkutano wa uchaguzi wa mwenyekiti wa halmshauri ya Urambo.
Katika mkutano huo, Alhaji Adam Malunkwi wa CCM alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa halmashauri hiyo.
Kabla ya mkutano huo, Sitta, ambaye alipokewa na wapigakura wake kwa msafara wa pikipiki zaidi ya 70, magari zaidi ya 40 na vikundi mbalimbali vya hamasa, alitumia fursa hiyo kuwaeleza wapigakura hao kilichomfanya ashindwe kutetea nafasi yake ya uspika.
Sitta pia alitoa msaada wa mashine ya kusaga na kukoboa nafaka kwa kikundi cha kinamama wa Uyogo kutekeleza ahadi yake kabla ya uchaguzi mkuu
Alisema mashine hiyo itakuwa kitega uchumi chao kwa kile anachoamini kuwa ukimwezesha mama, umeiwezesha jamii.
Mbali na mashine hiyo Sitta pia alitoa msaada wa mashine ya umeme wa sola kwa ajili ya zahanati ya Uyogo.
Akikabidhi msaada huo alisema kabla ya umeme haujasambaa maeneo hayo, atahakikisha zahanati zote zinapata umeme huo kurahisisha huduma zake kwa jamii.
Chanzo: Mwananchi
Subscribe to:
Posts (Atom)